Zungu: Jamii ijitenge na taarifa zisizo sahihi

Zungu: Jamii ijitenge na taarifa zisizo sahihi

Zungu: Jamii ijitenge na taarifa zisizo sahihi

Dar es Salaam.  Jamii imeaswa kutofungama na makundi ya watu yenye lengo la kubomoa umoja uliojengeka baina yao kwa kusambaza taarifa zisizo sahihi na kuibua chuki na taharuki.

Wito huo umetolewa leo Septemba 28, 2024 jijini Dar es Salaam na Naibu Spika wa Bunge, Mussa Zungu katika siku ya pili ya mkutano wa 53 wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania.

Zungu amesema kila mtu katika jamii anapaswa kujiona ana wajibu wa kulinda amani na kuisaidia Serikali katika kuhakikisha wanaofanya vitendo vya uvunjifu wa amani wanachukuliwa hatua za kisheria.

Ametoa wito kwa viongozi wa dini kuiombea nchi na kuendelea kuhubiri masuala ya amani na upendo kwa waumini.

Vilevile ameipongeza jumuiya hiyo kwa kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya athari ya kuchanganya masuala ya dini na siasa.

“Kuchanganywa kwa masuala ya dini na siasa kunaweza kuleta mkanganyiko na kuzalisha mianya ya ama wanasiasa kuitumia dini vibaya au watu wa dini kutumia siasa vibaya kwa ajili ya masilahi yao binafsi,” amesema.

Katika mkutano huo, Zungu pia amezungumzia mmomonyoko wa maadili hasa kwa vijana, akitaja utandawazi na matumizi yasiyo sahihi ya mitandao kama baadhi ya visababishi.

Amesema ili kuondokana na changamoto hiyo ni muhimu wazazi kuhakikisha wanahimiza na kusimamia watoto kupata elimu ya darasani pamoja na ya dini.

Vilevile amewataka viongozi wa dini kuhakikisha jamii inapata mafunzo sahihi ya dini ili kuwajenga kuwa na hofu ya Mungu.

“Elimu sahihi ya kimaadili mnayowapa watoto wenu ndiyo inayojenga jamii imara yenye kujenga waumini wenye maadili. Mtu hawezi kuwa mpenzi wa Mungu kisha akaacha kufanya wema kwa viumbe wengine hasa wanadamu,” amesema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Elimu Msingi, Abdi Maulid amesema mtoto akipata elimu ya darasani na ya dini itasaidia kuzalisha wanataaluma katika fani mbalimbali wenye maadili.

Amir wa jumuiya hiyo, Khawaja Ahmad amesema madhehebu hayo yamekuwa yakifanya mkutano kila mwaka kwa lengo la kuwakutanisha waumini na kuwakumbusha wajibu wao kama binadamu hapa duniani ikiwemo kumcha Mungu.

Amesema mkutano huu unalenga kuongeza hofu ya Mwenyezi Mungu, kuhimiza kuepukana na maovu, kuchochea moyo wa huruma na upendo na kuwakumbusha waumini kuendeleza tamaduni ya kuisaidia jamii katika nyanja mbalimbali, ikiwemo utoaji wa huduma za afya, elimu na misaada ya kibinadamu kwa wenye uhitaji bila ya kujali itakadi ya imani zao.

“Vilevile  kuwaelimisha na kuwahimiza vijana kuwa na mienendo bora ya kimaisha na kuwa raia wawajibikaji kwa nchi yao, na kuwa viongozi waadilifu katika jamii kwa mustakabali wa jamii na Taifa bora,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading