ZRA inavyojipanga kudhibiti rushwa Zanzibar

ZRA inavyojipanga kudhibiti rushwa Zanzibar

Unguja. Wakati Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) ikitunukiwa tuzo ya udhibiti vitendo vya rushwa, imesema hatua hiyo imeongeza morali kuendelea kupambana na vitendo hivyo ili kufikia malengo ya kukusanya zaidi ya Sh800 bilioni mwaka 2024/25.

Tuzo hiyo imetolewa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu  Uchumi Zanzibar (Zaeca), ikiwa ni kutambua mchango wa ZRA katika kudhibiti vitendo vya rushwa na uhujumu wa uchumi kisiwani humo.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo Julai 15 2024, Kaimu Kamishna Mkuu wa ZRA, Said Ali Mohamed amesema ZRA, imejipanga kuhakikisha hakuna mianya ya rushwa katika utendaji kazi na huduma inazotoa.

“ZRA imejijengea utaratibu mzuri kuhakikisha jukumu la ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya Serikali linasimamiwa ipasavyo, huku ikitilia maanani udhibiti wa mianya yote ambayo inaweza kuvujisha mapato ya Serikali,” amesema.

Katika misingi hiyo, amesema ZRA itaendeleza weledi katika usimamizi wa mapato na kwamba, taasisi hiyo itadumisha ushirikiano na taasisi zingine ili kuhakikisha vitendo vya rushwa vinapigwa vita na kuchukiwa na kila mmoja.

Kamishna Said amesema pamoja na kutekelezwa kwa kanuni imara za kiutumishi, ZRA inayo mikakati iliyoandaliwa mahususi kwa lengo la kupambana na rushwa ili kudhibiti usimamizi wa mapato.

Amesema Mamlaka hiyo ina mkakati wa kupambana na rushwa 2022/2023 hadi 2024/2025, kanuni ya maadili ya kiutendaji kwa watendaji, na dira ya utoaji wa taarifa za masuala ya kimaadili.

Pamoja na mikakati hiyo, Kaimu Kamishna Mkuu wa ZRA amesema kwa kufahamu na kuyapa uzito masuala ya kimaadili kwa watendaji na walipakodi, muundo wa ZRA umeanzisha kitengo maalumu kinachosimamia upelelezi na maadili ya wafanyakazi.

Amesema hatua ya taasisi hiyo kuanzisha njia mbalimbali za mawasiliano kama programu ya ZRA Funguka na kituo cha mawasiliano ya walipakodi, ni miongoni mwa jitihada za kuona taasisi inajisogeza karibu zaidi na jamii ili kuweka wazi mianya ya upotevu wa mapato.

Mkurugenzi wa Zaeca, Ali Abdallah Ali amesema hatua hiyo ni kutoa motisha kwa taasisi ili kuongeza ushirikiano na kudhibiti vitendo hivyo.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading