Zitto na Othman wapania kuongoza dola 2025

Zitto na Othman wapania kuongoza dola 2025

Kigoma. Chama cha ACT Wazalendo kimeweka wazi mpango wa kuhakikisha katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, kinampa nafasi Zitto Kabwe kuwa Rais wa Tanzania na Masoud Othman kushika wadhifa huo visiwani Zanzibar.

Kabwe ambaye ni kiongozi mstaafu wa chama hicho, mara kadhaa amesikika akitangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Kigoma Mjini alilowahi kuliongoza mwaka 2015 hadi 2020.

Lakini, mwanasiasa huyo pia amewahi kuweka wazi nia yake ya kuwania urais katika uchaguzi wa mwaka 2025, ingawa baadaye alibadili msimamo akiutaka ubunge wa Kigoma kwa kile alichoeleza analenga kwenda kuweka mambo sawa bungeni.

Kwa upande wa Othman ambaye kwa sasa ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, aliushika wadhifa huo akimrithi Maalim Seif Sharif Hamad aliyefariki Februari mwaka 2021.

Hayo yameelezwa mkoani Kigoma leo Jumapili Mei 5, 2024 na Kabwe katika mkutano wa hadhara uliofanyika kuhitimisha sherehe za kuadhimisha miaka 10 ya kuzaliwa kwa ACT Wazalendo.

Mkakati wa Kabwe

Katika hotuba yake, mwanasiasa huyo aliyestaafu uongozi wa juu ndani ya chama hicho, amesema yupo tayari kwa kila namna na wakati wowote kuwa Rais wa Tanzania.

Uamuzi wake wa kuingia katika kinyang’anyiro hicho, amesema utatokana na matakwa ya wananchi.

“Nataka niwaambie na nataka nimwambie ndugu Jussa, nimejiandaa kisaikolojia, kiakili na kimaarifa, kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Kwa hiyo wakati wowote mkinihitaji hatuna shida ya Jimbo hapa vijana wapo tunaweza kumleta yeyote agombee,” amesema. Mzizi wa kauli hiyo ya Kabwe ni hoja iliyoibuliwa na Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Zanzibar, Ismail Jussa aliyesema mwaka 2025 wanamtaka mwanasiasa huyo awe Rais wa Tanzania.

“Adhma ya ACT Wazalendo ni Rais wa awamu ya saba wa Tanzania awe Zitto Kabwe,” amesema huku akiahidi kuhakikisha Othman anakuwa Rais kwa upande wa Zanzibar.

Katika mwendelezo wa hotuba yake, Kabwe amesema pamoja na kuweka msingi kwa miaka 10, bado chama hicho hakijatimiza lengo lake.

Kwa mujibu wa mbunge huyo wa zamani wa Kigoma Mjini, miaka 10 ijayo ni kwa ajili ya chama hicho kushika dola na kuleta mabadiliko serikalini.

Amegusia safari ya chama hicho, akisema kilianza kwa kuitwa cha watu wa Kigoma, lakini sasa kimeenea kila kona ya Tanzania na viongozi wake ni kielelezo cha hilo.

“Kiongozi wa chama ni mtu wa Kilimanjaro, Mwenyekiti ni mtu wa Pemba, Makamu Mwenyekiti Bara ni mtu wa Lindi, Makamu Zanzibar ni mtu wa Unguja, Katibu Mkuu mtu wa Tunduru.

“Wanachama mjivunie mbegu mliyoipanda kwa miaka 10 iliyopita kwa sasa imeenea Tanzania nzima mnapaswa kutembea kifua mbele,” amesisitiza.

Mkakati wa Othman

Katika hotuba yake, Jussa amesema mwaka 2025 atahakikisha Othman anakuwa Rais wa Zanzibar.

Amesisitiza ahadi yake kwamba atakabidhi Serikali itakayotokana na chama hicho katika uchaguzi wa mwakani.

“Othman atakuwa Rais wa Zanzibar mwaka huo,” amesema.

Hata hivyo, ahadi hiyo imeonekana kupokelewa vema na Othman aliyesema pamoja naye katika uchaguzi huo, Kabwe anapaswa kuwa Rais wa Tanzania.

“Mungu akipenda 2025 tunataka tushindane na Kigoma, mkikabidhiwa Serikali kule huku Kigoma pia mtukabidhi kwa sababu ng’ombe hachinjwi mkiani,” amesema.

Amesema kufanya hivyo kutawezesha kupatikana kwa uongozi bora na kuuondoa ule aliodai umeshindwa kusimamia vema rasilimali za nchi.

Ameielekeza hotuba yake hiyo katika hoja kuwa, Tanzania ina rasilimali nzuri isipokuwa imekosa viongozi bora.

Othman amesema hilo lipo hata Kigoma, Mkoa ambao umejaa rasilimali, lakini wenyewe umebaki kuwa masikini.

“Unaweza kuwa hodari na madhubuti, lakini ukiwa na dereva mbovu hutafika mjini,” amesema.

Amesema ni muhimu kubadili dereva ili kuweka mambo yote sawa.

Lakini, amesema haitawezekana kumbadilisha dereva iwapo wananchi hawataamua kupitia uchaguzi wa mwaka 2025.

Amesisitiza ili kuepuka ya mwaka 2020 na udhalimu ni vema kuwa na Katiba Mpya itakayowapa wananchi haki na uhuru wa kuchagua.

Amesema kabla ya Katiba Mpya, lazima itangulie kupatikana tume huru ya uchaguzi itakayosimamia maoni ya wananchi.

Katika ufunguzi wa mkutano huo, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mkoa wa Kigoma, Kizza Mayeye ameielekeza hotuba yake kwa kutaja changamoto tano zinazoufanya mkoa huo uwe mahali pagumu pa kuishi.

Kwa mujibu wa Mayeye, Serikali mkoani humo imezuia matumizi ya Ziwa Tanganyika kwa madai ya upungufu wa samaki, akisema kitendo hicho kinaumiza wananchi.

Amesema Serikali inafanya hivyo ilhali tegemeo kubwa la maisha ya wananchi wa Mkoa huo ni shughuli za uvuvi.

Mwenyekiti huyo ameeleza hatua hiyo imewafanya wananchi wakose uhakika wa milo mitatu, kadhalika wazazi kushindwa kuhudumia familia.

Amesisitiza kitendo hicho ni kukosa huruma dhidi ya wananchi na kwamba ACT Wazalendo haiungi mkono.

“Sisi hatuungi mkono ufungaji wa ziwa kwa sababu unahatarisha maisha ya wananchi wa Kigoma,” amesema.

Lingine alilolitaja kuwa changamoto kwa wananchi hao ni usumbufu wa kushukiwa uraia wao.

Kinachosababisha usumbufu huo, amesema ni Mkoa huo kupakana na nchi jirani.

“Maisha ya wananchi wa Kigoma ni magumu, tunashukiwa kutokuwa raia, hili linafanya tuishi kwenye ardhi yetu bila amani,” amesema.

Kwa mujibu wa Mayeye, pamoja na uwepo wa vyanzo vya maji katika Mkoa huo, bado wananchi wa Kigoma hawana uhakika wa maji safi na salama.

 Hata hivyo, Mayeye amesema Suluhu ya changamoto hiyo ni wananchi kuchagua viongozi kutoka katika chama hicho katika chaguzi zijazo.

“Mkoa huu ndiyo ngome ya chama hiki, tutashinda uchaguzi wa Serikali za mitaa, Uchaguzi Mkuu kwa maana majimbo ya kutosha, madiwani na wabunge,” amesema.

Pamoja na hilo, amesema matamanio ya wananchi ni kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi isiyoishia kwenye nyaraka pekee, bali iwe na uhalisia.

“Hatutaki kuwa na tume huru lakini bado tunaendelea kukamata kura za wizi katika chaguzi,” amesema.

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ya chama hicho, Abdul Nondo amegusia dalili ya kuendelea kwa changamoto katika chaguzi zijazo.

Hisia zake hizo zinatokana na kile alichoeleza, bado mabadiliko ya sheria yanaikingia kifua tume ya uchaguzi iliyoteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan iendelee kubaki madarakani.

Msimamo wa chama hicho kwa mujibu wa Nondo, ni kujiuzulu kwa watendaji hao na kamati ya usaili itekeleze wajibu wake kama sheria mpya inavyoeleza.

“Sisi tunataka ahadi ya Rais Samia kwamba atafanya mabadiliko ya siasa, tuone anatekeleza kwa vitendo na sio maneno tupu,” amesema.

Ushahidi wa kutoimarika kwa mifumo ya uchaguzi, amesema kumeshuhudiwa katika uchaguzi mdogo wa Kasingilima ambao dhuluma imeendelea kufanywa.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading

Popular
Chief Editor

Zanzibar airport operators decry job losses over Dubai deal

Tanzania air operators say over 600 workers are set to lose their jobs after the semi-autonomous government of Zanzibar awarded a Dubai-based company exclusive rights to handle ground services at a refurbished airport.

The Tanzania Air Operators Association (Taoa) said in a statement that the contract awarded to Dnata, which is registered at the London Stock Exchange, was in breach of the law banning any company from having exclusive rights to ground-handling services at major airports.Continue Reading

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading