ZEC kuandikisha wapigakura wapya 78,922

ZEC kuandikisha wapigakura wapya 78,922

ZEC kuandikisha wapigakura wapya 78,922

Unguja. Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), inatarajia kuandikisha wapigakura wapya 78,922 waliotimiza umri wa miaka 18 kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 katika uandikishaji wapigakura awamu ya pili kwa mwaka huu wa 2025.

Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji George Kazi ametoa kauli hiyo leo Januari 17, 2025 alipofungua mkutano wa wadau wa uandikishaji wapigakura wapya awamu ya pili kwa mwaka 2025 katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, Pemba.

Shughuli hiyo inatarajiwa kuanza Februari Mosi katika Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba na kumalizikia Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini na Magharibi Machi, 2025.

“Uandikishaji huo ni matayarisho ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 pia ni wa mwisho kuelekea uchaguzi huo,” amesema.

Akizungumzia lengo la mkutano huo amesema ZEC ina utaratibu wa kukutana na wadau kila linapotokea jambo muhimu ambalo linahitaji kuwashirikisha.

Amesema tume kupitia mikutano hiyo pia inasikiliza maoni, hoja na mapendekezo yatakoyosaidia kuendesha shughuli hiyo kwa ufanisi.

Amesisitiza kwamba, uandikishaji utawahusu wapigakura wapya ambao hawajaandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapigakura.

Kazi hiyo amesema itafanyika kwa muda wa siku tatu kwa kila wilaya na kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa na Tume.

Amewataka wananchi waliotimiza sifa kujitokeza kutumia haki yao waweze kushiriki uchaguzi mkuu na kuwakumbusha huduma za uendelezaji wa daftari zinaendelea katika ofisi za Tume ya Uchaguzi za wilaya muda na saa zote za kazi.

Hata hivyo, amewataka wananchi na wadau wa uchaguzi Zanzibar kudumisha amani katika kipindi chote cha uandikishaji kama walivyofanikisha katika Kisiwa cha Pemba.

Amesema matumaini yake ni kwamba, wataendelea kushirikiana.

Awali, akiwasilisha taarifa na utaratibu wa uandikishaji wapigakura wapya na uendelezaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Thabit Idarous Faina, amesema wanatarajia kuweka wazi orodha ya wapigakura waliopoteza sifa na wanaohamisha taarifa zao kama inavyoelekezwa katika kifungu cha 19 na 31 cha Sheria ya uchaguzi na 4 ya mwaka 2018.

Hatua hiyo amesema itaenda sambamba na uwekaji wazi orodha ya wapigakura walioandikishwa katika uandikishaji wa awamu ya pili.

Amesema ZEC inaendelea kutoa huduma ya ujumbe mfupi wa maneno (sms) ambao wapigakura wanaweza kujua taarifa zao kwa kutumia simu ya mkononi kwa mitandao yote iliyosajiliwa Tanzania na huduma hiyo ni bure haina makato.

Amewaomba wananchi na wadau wa uchaguzi kwa ngazi tofauti kushirikiana na Tume kufikisha ujumbe huo ili kuwahamasisha wenye sifa za kujiandikisha kufika vituoni wakiwa na kitambulisho cha Mzanzibari mkazi.

“Kila mwananchi ana wajibu wa kwenda kituoni kuangalia jina lake, kuona jina la mtu ambaye hahusiki kuwemo kwenye daftari hilo, ama kwa kufariki dunia au kwa namna nyingine yoyote,” amesema.

Maulid Ame Mohammed, Mkuu wa Kurugenzi ya Huduma za Sheria akiwasilisha mada ya nafasi ya sheria katika uandikishwaji na uendelezaji wa daftari la wapigakura amesema kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kila Mzanzibari aliyetimiza miaka 18 ana haki ya kujiandikisha na kupiga kura katika uchaguzi unaofanyika Zanzibar.

Akifunga mkutano huo wa wadau, Kamishna wa Tume hiyo, Awadh Ali Said amewataka wadau kutambua majukumu yao na kuwa wa kweli katika changamoto zinazojitokeza wakati wa uandikishaji ili kazi hiyo ifanyike kwa ufanisi bila ya uvunjifu wa amani.

Mratibu kutoka Umoja wa Watu wenye Ulemavu Zanzibar (UWZ), Juma Kombo Hijja amevishauri vyama vya siasa kuwahamasisha wapigakura kwa kauli za kistaarabu na siyo kutoa kauli ambazo zinaviashiria vya uvunjifu wa amani kwani viashiria hivyo vitasababisha kundi la watu wenye ulemavu kutojitokeza na kushiriki kikamilifu.

Mkutano huo wa siku moja, umeshirikisha wadau wa uchaguzi, zikiwemo taasisi za Serikali na binafsi, vyama vya siasa, makundi maalumu, vyombo vya ulinzi na usalama na vya habari.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Popular
Chief Editor

Insecurity prompts Zanzibar to review its lucrative island leasing

The Tanzanian central government is planning to boost its security presence in the Zanzibar archipelago. A commission tasked with auditing the country’s security forces was appointed in July by President Samia Suluhu Hassan. It says it is concerned about the situation in the country’s Indian Ocean islands that are under the control of the semi-autonomous Zanzibar local government.Continue Reading

Muslims in Pemba conduct special prayer against ZAA decision
Popular
Investment News Editor

Muslims in Pemba conduct special prayer against ZAA decision

ZANZIBAR: More than 200 Muslims in Vitongoji Village, South Pemba Region over the weekend conducted a special prayer to condemn the Zanzibar Airports Authority (ZAA) move to appoint DNATA as the sole ground handler in Terminal III of the International Airport of Zanzibar. Abeid Amani Karume.Continue Reading

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading