Zanzibar yapiga ‘stop’ upigaji makachu Forodhani

Zanzibar yapiga ‘stop’ upigaji makachu Forodhani

Zanzibar yapiga ‘stop’ upigaji makachu Forodhani

Dar es Salaam. Mamlaka ya Mji Mkongwe Zanzibar imepiga marufuku upigaji wa makachu katika eneo la bustani ya Forodhani, baada ya kudaiwa kufanyika vitendo vinavyokiuka maadili.

Taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo jana Jumapili, Desemba 22, 2024 imeeleza uamuzi huo umefikiwa baada ya kuona kuna ukiukwaji wa sheria, kanuni na miongozo yaliyojitokeza kwa vijana wa makachu katika eneo hilo.

Imetaja pia ukiukwaji huo inahusisha upigaji makachu kwa kutumia mavazi yanayokwenda kinyume na utamaduni, uharibifu wa mifereji na miundombinu mengine, ikiwa ni pamoja na kutumia madebe taka kufanyia vichekesho (comedy).

Aidha, mamlaka hiyo imesema imesimamisha shughuli hizo hadi kukamilika na kuandaa utaratibu wa kuimarisha utendaji kazi hizo, kwani Serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na vijana hao katika kuutangaza Utalii wa Zanzibar kimataifa.

Vilevile, mamlaka hiyo imeeleza inafanya uchunguzi wa matukio hayo na kuwachukulia hatua wale wote waliobainika kutenda makosa hayo, ikiwemo uharibifu wa miundombinu.

Hivi karibuni ilisambaa video ikionyesha baadhi ya watu ambao ni wa raia wa kigeni wakipiga makachu eneo hilo wakiwa na nguo ambazo haziendani na maadili ya Zanzibar.

Endelea kufuatilia Mwananchi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Zanzibar Commerce
Top News
Investment News Editor

Zanzibar Airports Authority enforces Dnata monopoly

. Airlines that have not joined the Zanzibar Airports Authority’s (ZAA) preferred ground handler, Dnata, at the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA) face eviction from the Terminal Three building Dnata is the sole ground handler authorised to provide services for flights that operate at Terminal 3.Continue Reading

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading