Wenye betri ya moyo ushauri hii inawafaa

Wenye betri ya moyo ushauri hii inawafaa

Wenye betri ya moyo ushauri hii inawafaa

Dar es Salaam. Kama una shida ya moyo na umepandikizwa betri ya moyo,  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeshauri matumizi ya simu yasiwe karibu na eneo lenye kifaa hicho kuepusha mawasiliano baina ya vifaa hivyo.

Kitaalamu, betri ya moyo (Pacemaker) ni kifaa maalumu kinachosaidia kurekebisha mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida, kifaa hiki hufanya kazi kama jenereta, kikirejesha mfumo wa umeme wa moyo ili kuhakikisha unafanya kazi kwa mpangilio sahihi.

Ushauri huo wa TCRA wa kuepuka matumizi ya simu karibu na eneo lenye kifaa hicho ni kufuatilia swali la mwandishi wa habari juu ya nadharia zinazoelezwa kwenye jamii kuwa matumizi ya simu karibu na kifua husababisha matatizo ya moyo.

“Kama utakuwa na suala la kiafya peacemaker si vizuri simu au kifaa cha mawasiliano kukaa karibu  na ile kwa sababu nayo inawasiliana, kama ambavyo tunavyosema masafa hii na hii inawasiliana vikiingiliana vinaweza kuleta shida,” amesema Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dk Jabiri Bakari.

Dk Bakari ametoa ushauri huo leo Machi 28, 2025 wakati akizungumza na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyotembelea mradi wa maabara ya uidhinishaji wa vifaa vya mawasiliano vya kielektroniki.

Wakati Dk Bakari akitoa ushauri huo kwa wagonjwa wa moyo wenye betri, takwimu za  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) zinaonyesha Watanzania takriban 25 wanapandikizwa betri ya moyo kila mwezi, sawa na watu 300 kwa mwaka. Hili ni ongezeko kutoka watu 150 waliopandikizwa betri hiyo mwaka 2015/16,

Akizungumza  kuhusu usalama wa vifaa vya mawasiliano nchini Dk Bakari amesema kutokana na uwepo wa maabara hiyo vifaa feki vya mawasiliano havitafanya kazi nchini.

“Vifaa feki vitakuwa vimepungua sana, lakini ukikiwasha kifaa cha namna hiyo hapa (Tanzania) kinazima, kifaa hicho hatukusomi kama kimepita kwenye maabara yetu pia hakijazingatia viwango vya kimataifa hivyo hakiwezi kufanya kazi unaweza kuwasha simu ikazimika hapohapo,” amesema.

Dk Bakari amesema vifaa vyote vya mawasiliano vinavyotarajiwa kuingizwa nchini kwa ajili ya matumizi lazima wahakiki ubora wake lazima mzalishaji awasilishe sampuli ndani ya mamlaka hiyo kwa ajili ya kuangaliwa ubora.

“Kwanza kuangalia hakitakuwa hatarishi kwa mtumishi, jambo la pili tunahakikisha kifaa kinacholetwa nchini kina viwango na vinafanya kazi kulingana na masafa yaliyotengenezwa kwa ajili hiyo na isiingilie masafa mengine,” amesema.

Pia, amesema mamlaka hiyo inatarajia kuongeza mitambo ya kupima namna vifaa vya mawasiliano ya kielektroniki vinavyoweza kujikinga au kusababisha mwingiliano wa sumaku -umeme na vifaa vingine.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa PAC Nagenjwa Kaboyoka amesema ujenzi wa maabara hiyo umeniweka Tanzania katika hatua ya kimataifa.

“Watu wamekuwa na wasiwasi kwamba simu wanazotumia hazina ubora ‘feki’ lakini wataalamu wametuhakikisha simu wanazotumia wananchi haziwezi kuwadhuru,

“Maabara hii ni ya kimataifa na nchi zingine zinakuja kujifunza kuona namna ambavyo mitambo ya kielektroniki haiwezi kuingizwa nchini, pia yapo mitambo mbalimbali iliyopo hapa ni rahisi mtu mwenye mtambo wake ambao haukubaliki kukamatwa,” ameeleza.

Kutokana na uwepo wa maabara hiyo, Nagenjwa amesema Tanzania haina hofu ya kuingizwa vifaa feki’ nchini akisisitiza TCRA ijikite kujitangaza ili mataifa mengine yahamasike kufika nchini kutumia maabara hiyo.

Mbali na Tanzania mataifa mengine yenye maabara hiyo ni Tunisia, Afrika Kusini, Ghana, Nigeria, Cameroon, Benin, Guinea, Togo, Senegal, Mali na Mauritania.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading