Watanzania 56 waliozamia Afrika Kusini, wahukumiwa kulipa faini Sh50,000 kila mmoja

Watanzania 56 waliozamia Afrika Kusini, wahukumiwa kulipa faini Sh50,000 kila mmoja

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewahukumu Watanzania 56 kulipa faini ya Sh50,000 kila mmoja au kwenda jela miezi mitatu, baada ya kupatikana na hatia ya kwenda Afrika Kusini bila kufuata taratibu za uhamiaji.

Wamehukumiwa adhabu hiyo katika kesi ya jinai namba 9930/2024. Wote  wamelipa faini.

Hukumu imetolewa jana Jumatano  Aprili 17, 2024 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Gwantwa Mwankuga baada ya washtakiwa kukiri kosa na mahakakama kutiwa hatiani kwa kosa hilo.

Hakimu Mwankuga amesema washtakiwa wametiwa hatiani kama walivyoshtakiwa na wamekiri shtaka lao, hivyo anawahukumu kila mshitakiwa kulipa faini Sh50,000 na wakishindwa kulia watatumikia kifungo cha miezi mitatu jela kila mmoja.

Awali, wakili wa Serikali kutoka Idara ya Uhamiaji, Raphael Mpuya akishirikiana na Wakili Ezekiel Kibona, waliwasomea washtakiwa mashtaka.

Wanadaiwa Aprili 11, 2024 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), wilayani Ilala walitenda kosa hilo.

Inaelezwa washtakiwa wakiwa raia wa Tanzania, waliondoka isivyo halali nchini kueleleka Afrika Kusini.

Baada ya kusomewa shtaka walikiri kutenda kosa ndipo upande wa mashtaka ulipowasomewa hoja za awali.

Mpuya alidai kwa nyakati tofauti waliondoka nchini bila kufuata utaratibu, bila kuwa na hati ya kusafiria au nyaraka yoyote na pia walishindwa kupita kwenye mipaka rasmi iliyoainishwa na sheria za uhamiaji ikishirikiana na Serikali ili kujua madhumuni ya safari zao.

Wanadaiwa kuingia Afrika Kusini isivyo halali wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Alidai baada ya kurejeshwa nchini na kuhojiwa na Uhamiaji, washtakiwa walikiri kuondoka nchini wakiwa hawana hati za kusafiria, hivyo walifikishwa mahakamani.

Wakili Mpuya, baada ya kuwasomea maelezo alidai upande wa mashtaka hauna rekodi za makosa ya nyuma dhidi ya washtakiwa. Aliiomba Mahakama itoa adhabu ili iwe fundisho kwa vijana wengine.

“Tunaiomba Mahakama itoe adhabu kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwa vijana wengine wenye nia ovu wanaoenda Afrika Kusini bila kufuata utaratibu, jambo ambalo ni kinyume cha sheria,” amesema Mpuya.

Kabla ya hakimu kutoa adhabu, washtakiwa kwa nyakati tofauti waliomba kupunguziwa adhabu kwa wakidai wamekaa mahabusu muda mrefu nchini Afrika Kusini, hivyo wamejifunza na wanajutia kosa walilotenda.

Akitoa hukumu, Hakimu Mwankuga amesema amezingatia maelezo yaliyotolewa na upande wa mashtaka kuwa washtakiwa hawana rekodi za makosa ya jinai na jinsi washtakiwa walivyokiri kwa dhati shtaka.

“Kutokana na mazingira hayo na jinsi washtakiwa walivyojutia kosa lao, Mahakama hii inawahukumu kulipa faini ya Sh50,000 kila mmoja au kutumikia kifungo cha miezi mitatu jela kila mmoja,” ameamuru Hakimu Mwankuga.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading