Watanzania 24 washikiliwa na Mamlaka ya uhamiaji Marekani

Watanzania 24 washikiliwa na Mamlaka ya uhamiaji Marekani

Watanzania 24 washikiliwa na Mamlaka ya uhamiaji Marekani

Dar es Salaam. Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani umesema Serikali ina taarifa rasmi ya watu 24 wanaoaminika kuwa Watanzania wanaoshikiliwa na Mamlaka ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE) kwa kuishi nchini humo kinyume cha sheria.

“ICE imetuarifu kwamba, watu wanne kati ya hao wameshakamilisha taratibu zote za kimahakama za kuondoshwa nchini Marekani, hivyo watarejeshwa Tanzania muda wowote kuanzia sasa. Watu 20 waliobaki wapo kwenye hatua mbalimbali za kesi zao za uhamiaji huko Marekani,” umeeleza ubalozi huo.

Ubalozi huo katika majibu ya maswali yaliyoulizwa na Mwananchi kuhusu Watanzania waishio Marekani kinyume cha sheria umesema:

“Bado hatujaelezwa ni lini Watanzania hao watarejeshwa nyumbani lakini tayari ubalozi wetu nchini Marekani umeombwa na mamlaka husika za nchi hiyo, nyaraka za kusafiria za Watanzania wawili kati ya wanne ambao wameshapewa amri ya kuondoshwa nchini Marekani. Hivyo, tunatarajia watasafirishwa wakati wowote kurejeshwa nyumbani.”

Hatua ya kuwarejesha Watanzania hao imetokana na mkakati wa Rais wa Marekani, Donald Trump wa kutaka watu wote wanaoishi nchini humo bila vibali kuondolewa mara moja.

Hivi karibuni, taarifa ya ICE ilisema hadi Novemba 24, 2024, wahamiaji 1,445,549 kutoka mataifa mbalimbali waliorodheshwa kwa ajili ya kurejeshwa makwao.

Idadi hiyo ni ya watu kutoka mataifa mbalimbali wanaoishi Marekani bila vibali.

Katika orodha ya ICE, kwa nchi za Afrika Mashariki, Kenya imetajwa kuwa na wahamiaji wengi wapatao 1,282, ikifuatiwa na Burundi (462), Uganda (393), Rwanda (338) na Tanzania ikiwa na watu 301.

Katika majibu ya ubalozi huo kwa Mwananchi leo Februari 4, 2025 kwa maswali yaliyowasilishwa kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, umesema Watanzania watakaorejeshwa nyumbani kutoka Marekani wataruhusiwa kusafiri kwenda nchi nyingine bila kizuizi chochote, lakini kwa upande wa Marekani, kwa sheria zilizopo sasa, wanaweza kuomba viza na kuruhusiwa kuingia nchini humo baada ya miaka 10.

Kwa mujibu wa ubalozi huo, Watanzania wanaorejeshwa nchini baada ya kuishi Marekani kinyume cha sheria watakapofika nyumbani watapokewa na Idara ya Uhamiaji.

Umesema taratibu za kiuhamiaji zitakapokamilika watakuwa huru kuendelea na maisha yao kama raia wengine wa Tanzania.

“Kwenye suala hili la Watanzania waliokamatwa kwa kuishi kinyume cha sheria nchini Marekani, Ubalozi wetu nchini humo unashirikiana na mamlaka husika za uhamiaji nchini Marekani kuthibitisha uraia wa waliowekwa vizuizini na mamlaka hizo na kutoa nyaraka za kusafiria wanapothibitisha kuwa watu hao ni raia wa Tanzania. Ikumbukwe kwamba, kuishi nchi yoyote bila vibali maalumu ni kosa la kisheria,” umesema ubalozi huo.

Mkurugenzi wa Diaspora Tanzania, Kelvin Nyamori akizungumza na Mwananchi leo Februari 4, 2025 amesema itakuwa changamoto kwa watu wanaorudishwa kama walidanganya mataifa yao ili wapate haki ya ukimbizi.

“Kuna sheria za uhamiaji za kila nchini na hawa waliondoka kwa utaratibu, ukitokea Tanzania huwezi kusingizia vita au ukimbizi, kwa kuwa Tanzania hatuna matukio hayo, wapo wengine wanajitafutia nchi ili apewe nyaraka.

“Matokeo yake ikitokea tatizo kama hili wanasakwa waliingiaje na hakuna nchi ina usalama wa juu kama Marekani, sasa kama uliingia ukiitwa Judy ukiwa Mtanzania na pasipoti yako inaonyesha tangu umeondoka hujawahi kurudi halafu sasa ni Kuruthumu wa Somalia, hii itakuwa changamoto nyingine,” amesema.

Ameshauri watu kufuata taratibu na kuwa na vibali wanapotoka nje ya nchi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’
Top News
Chief Editor

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Monrovia — The Rwanda Minister of State responsible for Health, Dr. Yvan Butera, cautioned that while the country is beginning to see positive signals in its fight against the Marburg virus, the outbreak is “not yet over”. He, however, expressed hope that  “we are headed in that direction”. The minister said the epidemiology trend, since the disease was first discovered in the country more than a month ago, is moving towards fewer cases.

Dr. Butera, who was giving updates during an online briefing yesterday, said in the past two weeks, only two deaths were recorded while 14 people recovered from the disease. He said Rwanda was expanding its testing capacity with 16,000 people already inoculated against the disease.

The priority right now, Butera said, is “rapid testing and detection”.

Marburg is a highly virulent disease transmitted through human-to-human contact or contact with an infected animal. The fatality rate of cases, which has varied over the period, is more than 50%, according to the World Health Organization.  WHO said the highest number of new confirmed cases in Rwanda were reported in the first two weeks of the outbreak. There’s been a “sharp decline” in the last few weeks, with the country now tackling over 60 cases.

At Thursday’s briefing, a senior official of the Africa Centers for Disease Control, Dr. Ngashi Ngongo, said mpox – the other infectious disease outbreak that countries in the region are fighting – was been reported in 19 countries, with Mauritius being the latest country to confirm a case. He said although no new cases have been recorded in recent weeks in several countries where outbreaks occurred previously –  including Cameroon, South Africa, Guinea, and Gabon – Uganda confirmed its first Mpox death. This, he said, is one of two fatalities reported outside Central Africa.

Dr. Ngashi revealed that there was an increase in cases in Liberia and Uganda. He said mpox cases were still on an upward trend.

“The situation is not yet under control.”

Source: allafrica.com

Continue Reading