Wataalamu wapendekeza udhibiti bidhaa za mafuta Tanzania

Wataalamu wapendekeza udhibiti bidhaa za mafuta Tanzania

Dar es Salaam. Wataalamu wa afya nchini Tanzania wamependekeza udhibiti wa uingizwaji wa mafuta na bidhaa zake, kama mbinu ya kuepuka magojwa yasiyo ya kuambukiza kwa wananchi.

Mafuta waliyopendekeza yadhibitiwe ni yale yasiyoandaliwa vizuri na yenye hatari kubwa kwa matumizi ya binadamu.

Sambamba na hilo, wataalamu hao wamesema kama inawezekana itafutwe namna ya kuongezwa kodi kwa aina hiyo ya mafuta, wakati yale yaliyo salama yapunguziwe kodi.

Wataalamu hao wamesema hayo leo, Jumatatu Julai 8, 2024 walipokuwa wakichangia kwenye mjadala wa Mwananchi Space, uliojadili ‘Ulaji wa vyakula vya mafuta mengi na athari zake ulioandaliwa kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC).

Ofisa Lishe na Mtafiti Mwandamizi TFNC, Maria Ngillisho amesema vyakula vinavyopikwa kwa mafuta mengi vinavutia na vitamu, lakini vina madhara makubwa mwilini.

Amesema kupika kwa mafuta ni njia rahisi, lakini ina athari kiafya hasa vyakula hivyo vikitumiwa kwa wingi na mara kwa mara.

“Tuna vyakula tunavyopika kwenye mafuta mengi na hivi tunaweza kuviepuka kwa kupika kwa kutumia mbinu nyingine ikiwemo kuoka,” amesema.

Maria ameeleza vyakula vyenye mafuta mengi ni vile vyenye asili ya mafuta na vinavyopikwa kwa mafuta mengi.

Amevitaja vyakula hivyo ni karanga, mbegu za alizeti, korosho na vile vyenye asili ya mimea.

Naye Mkuu wa kitengo cha Utafiti na daktari bingwa kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dk Pedro Pallangyo amesema kiwango kikubwa cha mafuta kinasababisha mwili ushindwe kuyatumia katika shughuli za kawaida.

Hatua hiyo, amesema inasababisha yajihifadhiwe sehemu mbalimbali na hivyo kusababisha magonjwa.

“Dalili ya kuakisi kuwa mafuta ni namna anavyoongezeka uzito, kiribatumbo na mabadiliko hayo yanakuwa ndani ya mili yetu, hasa mafuta yanapoingia katika mfumo wa moyo na mishipa ya damu,” amesema.

Amesema binadamu walivyoumbwa mili yao ina mishipa ya damu yenye upenyo mdogo ambao damu inapita na ukubwa wake ni sahihi katika kukidhi mahitaji.

“Mafuta yakitanda katika mishipa mikubwa ya damu ukubwa wake unapungua, sasa inategemeana imetanda katika mishipa ipi ina maana hayo maeneo yatapokea kiwango kidogo cha damu kuliko inavyotakiwa,” amesema.

Amesema kutokana na wimbi la mafuta katika jamii hata vijana wanaanza kuonekana na magojwa hayo, huku akieleza wengi wanakuja na malalamiko ya magonjwa ya miguu na kuanza kubadilika rangi.

“Tafsiri ya haraka maeneo yaliyobadilika rangi hayapati kiwango cha damu ya kutosha na ukifanya uchunguzi wa miguu ya hao wahusika unaona mishipa midogo midogo inayolisha miguu inakuwa imeziba,” amesema.

Amesema kumekuwa na ongezeko la watu wengi kuziba mishipa mitatu ya moyo inayosababisha vifo vya ghafla kwa kuwa wanakosa hewa ya oskjeni kwenye moyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kitengo cha Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza wa Wizara ya Afya, Dk Omary Ubuguyu amesema kutokana na ukubwa wa tatizo hilo, kwa mwaka Serikali huitaji Sh1.1 trilioni kukabiliana na magonjwa hayo.

“Sisi tukiangalia mkakati wetu wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza tunahitaji Sh1.1 trilioni kwa mwaka kutoa huduma stahiki kutoa huduma stahiki kwa magonjwa sawa na bajeti nzima ya Wizara ya Afya inayotolewa sasa,” amesema Dk Ubuguyu.

Dk Ubuguyu amesema nchi imefika katika kiwango cha ukubwa wa tatizo kwa sababu walichelewa kuanza kupambana na magonjwa hayo, kwani  waliamini ni tatizo linalowapata zaidi watu wa ukanda wa Afrika Magharibi.

Naye Mtaalamu wa lishe wa TFNC, Elizabeth Lyimo amesema mafuta ni moja ya kundi la chakula lenye kazi maalumu mwilini kutokana na virutubisho vilivyopo.

“Kundi hili linapaswa liliwe kwa kuangaliwa kwa sababu linatoa kiwango kikubwa cha nishati lishe, laikini kuna aina mbili za mafuta ya kimiminika (yasiyo ganda) ni yale yanayotokana na mimea  na yanayoganda yanatokana na wanayama,” amesema.

Awali, Mhariri wa Jarida la Afya Gazeti la Mwananchi, Herieth Makwetta akichokoza mada amesema ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi ni chanzo cha magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ikiwemo shinikizo la damu na saratani.

“Utafiti wa mwisho uliofanywa na Wizara ya Afya mwaka 2018 unaonyesha asilimia 33 ya vifo vyote vilivyotokea nchini vilisababishwa na magonjwa yasiyoambukizwa,” amesema.

Katika maelezo yake Makwetta, amefafanua wataalamu wanaonya kuwa ifikapo mwaka 2027, huenda vifo vinavyotokana na hayo magonjwa vitafikilia asilimia 54.

“Wataalamu wanasema mafuta yanahitaji kiwango kidogo mwilini kwa kazi ya kumpatia nguvu kiasi cha dole gumba, lakini wengi wamekuwa wakikiuka na kujikuta wakiongeza uzito kupita kiasi,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading