Wapiga makachu wapigwa msasa, kufunguliwa kesho

Wapiga makachu wapigwa msasa, kufunguliwa kesho

Wapiga makachu wapigwa msasa, kufunguliwa kesho

Unguja. Wakati mchezo wa makachu ukifunguliwa kesho Desemba 31, 2024 Jumuiya ya  Waratibu na Waendesha Misafara ya watalii Zanzibar (Zato), imewapa mafunzo maalumu vijana hao ili kuendana na matakwa na miongozo ya utalii.

Mwenyekiti wa Zato, Khalifa Mohamed Makame amesema wamefikia hatua hiyo baada ya bodi ya Zato kuona kuna haja ya kuwapa elimu vijana hao, kwani wamekuwa sehemu ya bidhaa za utalii.

“Sisi makachu tunaichukulia kama bidhaa ya ziada iliyoongezeka katika huduma tunazozitoa kwenye utalii, hivyo inatakiwa ilindwe, ijengwe  ili iwe na mustakabali mwema kwa Wazanzibari,” amesema.

Amesema ndani ya kipindi kifupi yametokea matukio matano kwa wakati mmoja mambo ambayo yakiachwa yaendelee yanaweza kuleta tatizo.

Amesema wamebaini kinachokosekana kwa vijana hao ni weledi wanapofanya shughuli hizo na msaada wa kuwa na wanachama waadilifu na waaminifu wenye maadili.

“Kwa hiyo tunapowaangalia hawa vijana tunajiangalia kama sisi, tukiona wanachopitia tunawajibika kutia uso tuwasaidie hata katika kuchagua mtu sahihi katika uongozi wetu.”

Baadhi ya vijana hao wamekiri kuna baadhi ya matukio ambayo yalitokea kwa sababu ya kukosekana weledi wa kitaaluma.

Rais wa makachu, Hanafiy Said Salim amesema wamejifunza kutokana na makosa lakini watazingatia mafunzo waliyopewa yakiwamo ya kuzingatia maadili.

Naye kiongozi wa nidhamu wa kundi hilo, Omar Bakar Khalfan amesema, “tunakutana pale kila mmoja na tabia zake, jamii isituchukulie kama ni watu wasiokuwa na uadilifu isipokuwa ni watu wachache wanaotaka kuharibu taswira ya mchezo huo.

Katibu wa kundi hilo, Ali Saleh amesema “tunaweza kusema tunashukuru kutokana na kosa lile kwani kuna mambo mengi tulikuwa hatuyajui, lakini baada ya tukio hili tumefahamu na tumepewa mafunzo, hivyo lazima tusijisahau kufanya vitu visivyofaa,” amesema.

Mamlaka ya Uhifadhi na Uendeshaji Mji Mkongwe ilisitisha kwa muda mchezo wa makachu Forodhani tangu Desemba 22, 2024 baada ya kusambaa picha mjongeo iliyoonyesha mwanamke akiruka akiwa amevalia nguo ambazo ni kinyume na maadili ya utamaduni wa Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa kwa umma na kuthibitishwa na mkurugenzi wa Mji Mkongwe, Ali Abubakar, ilieleza wamechukua hatua hiyo kutokana na matukio ya ukiukwaji wa sheria na miongozo.

Akielezea wanapofunguliwa kesho nini kifanyike, Ali amesema watakaoruhusiwa ni wale watakaokubaliana na miongozo iliyowekwa kwa kufuata misingi ya maadili

Matukio hayo ni pamoja na upigaji makachu kwa kutumia mavazi yanayokwenda kinyume na utamaduni, uharibifu mkubwa wa mifereji na miundombinu mingine pamoja na matumizi ya debe za taka kwa michezo ya vichekesho.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’
Top News
Chief Editor

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Monrovia — The Rwanda Minister of State responsible for Health, Dr. Yvan Butera, cautioned that while the country is beginning to see positive signals in its fight against the Marburg virus, the outbreak is “not yet over”. He, however, expressed hope that  “we are headed in that direction”. The minister said the epidemiology trend, since the disease was first discovered in the country more than a month ago, is moving towards fewer cases.

Dr. Butera, who was giving updates during an online briefing yesterday, said in the past two weeks, only two deaths were recorded while 14 people recovered from the disease. He said Rwanda was expanding its testing capacity with 16,000 people already inoculated against the disease.

The priority right now, Butera said, is “rapid testing and detection”.

Marburg is a highly virulent disease transmitted through human-to-human contact or contact with an infected animal. The fatality rate of cases, which has varied over the period, is more than 50%, according to the World Health Organization.  WHO said the highest number of new confirmed cases in Rwanda were reported in the first two weeks of the outbreak. There’s been a “sharp decline” in the last few weeks, with the country now tackling over 60 cases.

At Thursday’s briefing, a senior official of the Africa Centers for Disease Control, Dr. Ngashi Ngongo, said mpox – the other infectious disease outbreak that countries in the region are fighting – was been reported in 19 countries, with Mauritius being the latest country to confirm a case. He said although no new cases have been recorded in recent weeks in several countries where outbreaks occurred previously –  including Cameroon, South Africa, Guinea, and Gabon – Uganda confirmed its first Mpox death. This, he said, is one of two fatalities reported outside Central Africa.

Dr. Ngashi revealed that there was an increase in cases in Liberia and Uganda. He said mpox cases were still on an upward trend.

“The situation is not yet under control.”

Source: allafrica.com

Continue Reading