Wanasheria Tanzania wapewa ujuzi kukabili uhalifu mtandao

Wanasheria Tanzania wapewa ujuzi kukabili uhalifu mtandao

Dar es Salaam. Ili kuimarisha utaalamu na mbinu za kisheria katika kukabiliana na uhalifu wa mtandao, Serikali inashirikiana na Russia kubadilishana uzoefu na elimu juu ya masuala hayo.

Katika kufanikisha hilo, wataalamu kutoka Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Russia wamewasili nchini na kutoa mafunzo kwa wanafunzi na wanataaluma ya sheria kuhusu masuala hayo.

Ushirikiano wa mataifa hayo kuhusu masuala ya kisheria ni matokeo ya ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mawaziri wengine walioenda Russia Julai mwaka jana.

Katika ziara hiyo, pamoja na mambo mengine viongozi hao walisaini hati mbalimbali za makubaliano ikiwamo ya ushirikiano wa kisheria katika kukabiliana na uhalifu wa mtandao na ugaidi.

Mafunzo kuhusu masuala hayo yamefanyika jana katika ukumbi wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST), jijini Dar es Salaam.

Akifungua mhadhara wa wakufunzi hao kutoka Russia, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Pindi Chana amesema hiyo ni hatua muhimu katika kuyafikia malengo ya dunia.

Amesema mafunzo hayo yanalenga kujenga uwezo wa utaalamu wa kisheria kwa wanataaluma hiyo waliopo nchini, ili wamudu kukabiliana na uhalifu ukiwemo wa mtandao na ugaidi.

“Mafunzo haya yanalenga kuondoa changamoto za kisheria zinazoyakabili mataifa mbalimbali duniani na kwamba, hii ni fursa ya kubadilishana uzoefu. Hili ni jambo muhimu kwa sababu mwelekeo wa dunia ni mmoja, dunia yote inapambana dhidi ya kukandamizwa kwa haki za binadamu na uhalifu,” amesema.

Amesisitiza kinachofanyika ni matokeo ya makubaliano kati ya Tanzania na Russia na kwamba, kuna maeneo mengine ya ushirikiano yatakayoongezwa.

Dk Chana alisema msingi wa mafunzo na ushirikiano huo ni kuimarisha misingi ya haki na usawa katika jamii ya Tanzania.

Awali, akihutubia mhadhara huo, Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST), Profesa Sisty Mramba alisema kunahitajika ushirikiano wa kimataifa ili kukabili ugaidi na uhalifu wa kimtandao.

“Changamoto zinazoikabili dunia kwa sasa ni ugaidi na uhalifu wa mtandao, kunahitajika ushirikiano wa mataifa mbalimbali katika kupeana ujuzi ili kukabiliana na changamoto zilizopo,” amesema Profesa Mramba.

Amesema ni muhimu kujenga uelewa wa kisheria juu ya kukabiliana na majanga ya uhalifu ukiwamo wa mtandao.

Balozi wa Russia nchini, Andrey Avetisyan alieleza kufurahishwa na hatua kubwa za kimageuzi katika mifumo ya kisheria zilizopigwa Tanzania.

Amesema anafurahishwa na mazingira rafiki na mazuri yanayowekwa na Serikali na Tanzania katika uwekezaji na biashara, huku akiwahimiza wawekezaji kutoka Russia kuwekeza nchini.

Hata hivyo, amesema ushirikiano wa Russia na Tanzania hasa katika masuala ya kisheria utajenga uelewa na mbinu bora za kukabiliana changamoto zilizopo.

Balozi Avetisyan amesema kuna umuhimu mkubwa wa ushirikiano wa kisheria kwani unawezesha kujua mifumo ya kisheria ya kila Taifa na hata kufahamu sheria zilizopo.

Alisema ushirikiano wa kisheria ni muhimu hasa kwa sasa kwa mustakabali wa uhusiano baina ya mataifa hayo.

Balozi Avetisyan alisema Russia ipo Tanzania kuendelea kufurahia ushirikiano, huku akimwalika Dk Chana kwenye Jukwaa la Kisheria la St. Peter litakalofanyika Juni, nchini humo.

Amesisitiza ushirikiano huo hautaishia hapo, utaenda mbali zaidi hadi katika kubadilishana wanafunzi wa sheria kati ya Tanzania na Russia.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns

Several airports have since locked Air Tanzania, dealing a severe blow to the Tanzanian national carrier that must now work overtime to regain its certification or go the wet lease way

The European Commission has announced the inclusion of Air Tanzania on the EU Air Safety List, effectively banning the airline from operating in European airspace.

The decision, made public on December 16, 2024, is based on safety concerns identified by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), which also led to the denial of Air Tanzania’s application for a Third Country Operator (TCO) authorisation.

The Commission did not go into the specifics of the safety infringement but industry experts suggest it is possible that the airline could have flown its Airbus A220 well past its scheduled major checks, thus violating the airworthiness directives.

“The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards for passengers in Europe and worldwide,” said Apostolos Tzitzikostas, EU Commissioner for Sustainable Transport and Tourism.

“We strongly urge Air Tanzania to take swift and decisive action to address these safety issues. I have offered the Commission’s assistance to the Tanzanian authorities in enhancing Air Tanzania’s safety performance and achieving full compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania has a mixed fleet of modern aircraft types including Boeing 787s, 737 Max jets, and Airbus A220s.

It has been flying the B787 Dreamliner to European destinations like Frankfurt in Germany and Athens in Greece and was looking to add London to its growing list with the A220.

But the ban not only scuppers the London dream but also has seen immediate ripple effect, with several airports – including regional like Kigali and continental – locking out Air Tanzania.

Tanzania operates KLM alongside the national carrier.

The European Commission said Air Tanzania may be permitted to exercise traffic rights by using wet-leased aircraft of an air carrier which is not subject to an operating ban, provided that the relevant safety standards are complied with.

A wet lease is where an airline pays to use an aircraft with a crew, fuel, and insurance all provided by the leasing company at a fee.

Two more to the list

The EU Air Safety List, maintained to ensure passenger safety, is updated periodically based on recommendations from the EU Air Safety Committee.

The latest revision, which followed a meeting of aviation safety experts in Brussels from November 19 to 21, 2024, now includes 129 airlines.

Of these, 100 are certified in 15 states where aviation oversight is deemed insufficient, and 29 are individual airlines with significant safety deficiencies.

Alongside Air Tanzania, other banned carriers include Air Zimbabwe (Zimbabwe), Avior Airlines (Venezuela), and Iran Aseman Airlines (Iran).

Commenting on the broader implications of the list, Tzitzikostas stated, “Our priority remains the safety of every traveler who relies on air transport. We urge all affected airlines to take these bans seriously and work collaboratively with international bodies to resolve the identified issues.”

In a positive development, Pakistan International Airlines (PIA) has been cleared to resume operations in the EU following a four-year suspension. The ban, which began in 2020, was lifted after substantial improvements in safety performance and oversight by PIA and the Pakistan Civil Aviation Authority (PCAA).

“Since the TCO Authorisation was suspended, PIA and PCAA have made remarkable progress in enhancing safety standards,” noted Tzitzikostas. “This demonstrates that safety issues can be resolved through determination and cooperation.”

Another Pakistani airline, Airblue Limited, has also received EASA’s TCO authorisation.

Decisions to include or exclude airlines from the EU Air Safety List are based on rigorous evaluations of international safety standards, particularly those established by the International Civil Aviation Organization (ICAO).

The process involves thorough review and consultation among EU Member State aviation safety experts, with oversight from the European Commission and support from EASA.

“Where an airline currently on the list believes it complies with the required safety standards, it can request a reassessment,” explained Tzitzikostas. “Our goal is not to penalize but to ensure safety compliance globally.”

Airlines listed on the EU Air Safety List face significant challenges to their international operations, as the bans highlight shortcomings in safety oversight by their home regulatory authorities.

For Air Tanzania, this inclusion signals an urgent need for reform within Tanzania’s aviation sector to address these deficiencies and align with global standards.

The path forward will require immediate and sustained efforts to rectify safety concerns and regain access to one of the world’s most critical aviation markets.

Source: allafrica.com

Continue Reading