Wananchi Paje wataka ushirikishwaji ujenzi uwanja wa ndege

Wananchi Paje wataka ushirikishwaji ujenzi uwanja wa ndege

Unguja. Wananchi zaidi ya 400 katika Kijiji cha Paje Mkoa wa Kusini Unguja, wameingiwa wasiwasi kuhusu kuhamishwa eneo hilo,  kupisha ujenzi wa uwanja wa ndege wakidai hawajashirikishwa.

Wasiwasi huo unatokana na kuwapo mpango wa Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kutaka kujenga uwanja wa ndege katika eneo hilo.

Wamesema wamekuwa wakiona wataalamu wanaenda kupima maeneo yao lakini hawana taarifa yoyote wala kushirikishwa.

Mkazi wa eneo hilo, Haji Nuru Said amesema wao hawapingani na mipango ya Serikali, lakini wanachotaka ni ushirikishwaji ili watambue iwapo wakihamishwa wapi wanakwenda au vinginevyo.

“Kuna utata unaojitokeza watu wanakuja kupima kwenye maeneo yetu lakini hatuna taarifa na hatushirikishwi, tunaomba mchakato wote tushirikishwe na kujua kinachoendela,” amesema. 

Kauli hiyo imeungwa mkono na Abubakar Mtumwa anayesema: “Sisi hatupingi maendeleo lakini tunasikia huko tu hatushirikishwi kwenye hatua zote ili kuridhia au kama tutatakiwa kuondoka tujue ni wapi tunakwenda na katika misingi gani.”

Hata hivyo, Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Dk Khalid Salum Mohamed  amewataka wananchi hao walio karibu na eneo hilo linalotarajiwa kujengwa uwanja wa ndege,  kuondoa wasiwasi kwani Serikali haiwezi kufanya uamuzi bila kuwashirikisha wananchi wa eneo husika.

Dk Khalid amesema bado mchakato huo upo kwenye hatua za awali, kwa hiyo iwapo kukiwa na uamuzi wa kujenga uwanja huo, lazima wananchi watashirikishwa na ikiwezekana hata watakaotakiwa kupisha watalipwa fidia.

“Serikali haiwezi kufanya jambo bila kuwashirikisha na hakuna mwananchi atakayeondolewa kwenye eneo lake. Kinachofanyika kwa sasa bado ni upembuzi yakinifu iwapo uamuzi ukifikiwa kila kitu kitakuwa sawa,” amesema Dk Khalid.

Kwa sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ina mipango ya kujenga viwanja vya ndege katika maeneo ya utalii ili kurahisisha ufikaji.

Miongoni mwa maeneo hayo ni Paje Mkoa wa Kusini Unguja na Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading