Waliomba kazi TRA, kufanyiwa usaili hapa

Waliomba kazi TRA, kufanyiwa usaili hapa

Dar es Salaam. Watu 112,952 wameitwa kwenye usaili wa mchujo wa kuandika (Written Interview), baada ya kukidhi vigezo vya maombi ya ajira katika nafasi 1596 zilizotangazwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania( TRA).

Februari 6, 2025, TRA ilitangaza nafasi za ajira 1596  katika fani mbalimbali, ambapo watu 135,027 waliomba nafasi hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jioni, Machi 21, 2025, kuhusiana na mchakato wa kuwapata waombaji hao, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala kutoka TRA, Moshi Kabengwe,  amesema TRA ilipitia kwa umakini maombi ya kazi 135,027 na kupata maombi 112,952 ambao ndio wenye vigezo vya kuitwa kwenye usaili.

Amesema majina ya watu hao waliokidhi vigezo hivyo, yatatangazwa kesho Machi 22, 2025 katika tovuti ya Mamlaka hiyo ya mapato.

“TRA imepitia kwa umakini mkubwa maombi yote 135,027 yaliyopokelewa na kupata waomba kazi 112,952 ambao wamekidhi vigezo vilivyowekwa na hivyo wanastahili kuitwa kwenye usaili wa mchujo wa kuandika( Written Interview) unaotarajia kufanyika Machi 29 na Machi 30, 2025 katika kanda tisa zilizoanishwa na TRA,” amesema Kabengwe na kuongeza.

“Mbali na majina kuwekwa kwenye tovuti ya TRA, pia taarifa itatumwa moja kwa moja kwa kila muombaji kupitia barua pepe yake aliyotumia wakati wa kuomba kazi, vilevile tarehe, mahali na muda wa usaili zimeonyeshwa kwenye wito huo” amefafanua.

Amesema mwitikio wa watu kuomba nafasi za kazi umekuwa mkubwa,  kwani TRA ilitangaza nafasi za kazi 1,596, lakini hadi Februari 19, 2025 walipokamilisha siku ya mwisho ya kupokea maombi walioomba walikuwa ni 135,027.

Kabengwe amebainisha kuwa usaili wa mchujo huo utafanyika katika mikoa tisa, ambapo Dar es Salaam itahusisha waombaji kutoka Dar es Salaam na Pwani.

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali watu na Utawala kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania( TRA) Moshi Kabengwe, akizungumza na waandishi wa habari ( hawapo pichani) wakati akitangaza idadi ya watu walioitwa kwenye usaili wa mchujo wa awali, baada ya kukidhi vigezo vya maombi ya kazi yaliyotangazwa na Mamlaka hiyo. Picha na Hadija Jumanne

“Kituo cha usaili cha Zanzibar itahusisha waombaji kutoka Unguja na Pemba, wakati kituo cha usaili cha Dodoma itahusisha waombaji kutoka mikoa ya Morogoro, Dodoma, Singida, Iringa na Tabora” amesema.

Amesema kwa upande wa kaskazini, kituo cha usaili kutakuwa Arusha, ambapo kitahusisha waombaji kutoka mkoa wa Manyara, Kilimanjaro, Arusha yenyewe na Tanga.

Kwa upande wa mikoa ya Kusini, eneo la usajili litakuwa Mtwara ambapo itahusisha waombaji kutoka Lindi, Mtwara na Ruvuma.

“Pia Mwanza itakuwa ni kituo cha usaili kwa waombaji kutoka mikoa ya Shinyanga, Mara, Mwanza na Simiyu,” amesema.

Vilevile kwa upande wa Nyanda za Juu Kusini, kituo cha usaili kitakuwa Mbeya ambapo kitahusisha waombaji kutoka Songwe, Mbeya na Rukwa.

Vilevile kituo cha usaili cha Kigoma, kitahusisha waombaji kutoka mkoa wa Katavi na Kigoma yenyewe wakati kwa kituo cha usaili cha Kagera kitahusisha waombaji kutoka Geita na Kagera yenyewe.

“Utaratibu maalum umeandaliwa kwa waombaji kazi wenye mahitaji maalum waliofanikiwa kuitwa kwenye usaili wa mchujo wa kuandika ili waweze kufanya usaili huo bila usumbufu” amesema.

Kabengwe alifafanua kuwa mchakato huo wa ajira utaendeshwa na Mshauri mtaalamu na Mamlaka itasimamia kwa karibu ili kuhakikisha haki inatendeka kwa waombaji wote.

“Waombaji watakao faulu kwenye usaili wa mchujo wa kuandika wataitwa kwenye usaili wa mahojiano kwa tarehe itakayopangwa” amesema.

Vilevile, ameitaka jamii pamoja na waombaji wa nafasi hizo za kazi kuepuka utapeli unaoweza kufanywa na watu ambao sio waaminifu na kwamba TRA itaweka namba maalumu kwa ajili ya mawasiliano baina ya waombaji ili kuepuka utapeli.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns

Several airports have since locked Air Tanzania, dealing a severe blow to the Tanzanian national carrier that must now work overtime to regain its certification or go the wet lease way

The European Commission has announced the inclusion of Air Tanzania on the EU Air Safety List, effectively banning the airline from operating in European airspace.

The decision, made public on December 16, 2024, is based on safety concerns identified by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), which also led to the denial of Air Tanzania’s application for a Third Country Operator (TCO) authorisation.

The Commission did not go into the specifics of the safety infringement but industry experts suggest it is possible that the airline could have flown its Airbus A220 well past its scheduled major checks, thus violating the airworthiness directives.

“The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards for passengers in Europe and worldwide,” said Apostolos Tzitzikostas, EU Commissioner for Sustainable Transport and Tourism.

“We strongly urge Air Tanzania to take swift and decisive action to address these safety issues. I have offered the Commission’s assistance to the Tanzanian authorities in enhancing Air Tanzania’s safety performance and achieving full compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania has a mixed fleet of modern aircraft types including Boeing 787s, 737 Max jets, and Airbus A220s.

It has been flying the B787 Dreamliner to European destinations like Frankfurt in Germany and Athens in Greece and was looking to add London to its growing list with the A220.

But the ban not only scuppers the London dream but also has seen immediate ripple effect, with several airports – including regional like Kigali and continental – locking out Air Tanzania.

Tanzania operates KLM alongside the national carrier.

The European Commission said Air Tanzania may be permitted to exercise traffic rights by using wet-leased aircraft of an air carrier which is not subject to an operating ban, provided that the relevant safety standards are complied with.

A wet lease is where an airline pays to use an aircraft with a crew, fuel, and insurance all provided by the leasing company at a fee.

Two more to the list

The EU Air Safety List, maintained to ensure passenger safety, is updated periodically based on recommendations from the EU Air Safety Committee.

The latest revision, which followed a meeting of aviation safety experts in Brussels from November 19 to 21, 2024, now includes 129 airlines.

Of these, 100 are certified in 15 states where aviation oversight is deemed insufficient, and 29 are individual airlines with significant safety deficiencies.

Alongside Air Tanzania, other banned carriers include Air Zimbabwe (Zimbabwe), Avior Airlines (Venezuela), and Iran Aseman Airlines (Iran).

Commenting on the broader implications of the list, Tzitzikostas stated, “Our priority remains the safety of every traveler who relies on air transport. We urge all affected airlines to take these bans seriously and work collaboratively with international bodies to resolve the identified issues.”

In a positive development, Pakistan International Airlines (PIA) has been cleared to resume operations in the EU following a four-year suspension. The ban, which began in 2020, was lifted after substantial improvements in safety performance and oversight by PIA and the Pakistan Civil Aviation Authority (PCAA).

“Since the TCO Authorisation was suspended, PIA and PCAA have made remarkable progress in enhancing safety standards,” noted Tzitzikostas. “This demonstrates that safety issues can be resolved through determination and cooperation.”

Another Pakistani airline, Airblue Limited, has also received EASA’s TCO authorisation.

Decisions to include or exclude airlines from the EU Air Safety List are based on rigorous evaluations of international safety standards, particularly those established by the International Civil Aviation Organization (ICAO).

The process involves thorough review and consultation among EU Member State aviation safety experts, with oversight from the European Commission and support from EASA.

“Where an airline currently on the list believes it complies with the required safety standards, it can request a reassessment,” explained Tzitzikostas. “Our goal is not to penalize but to ensure safety compliance globally.”

Airlines listed on the EU Air Safety List face significant challenges to their international operations, as the bans highlight shortcomings in safety oversight by their home regulatory authorities.

For Air Tanzania, this inclusion signals an urgent need for reform within Tanzania’s aviation sector to address these deficiencies and align with global standards.

The path forward will require immediate and sustained efforts to rectify safety concerns and regain access to one of the world’s most critical aviation markets.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Popular
Swahili News Editor

MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.Continue Reading