Walilia uraia pacha, kisa kudhulumiwa na ndugu zao

Walilia uraia pacha, kisa kudhulumiwa na ndugu zao

Walilia uraia pacha, kisa kudhulumiwa na ndugu zao

Dar es Salaam. Watanzania wanaoishi nje ya nchi (diaspora) wamesisitiza haja ya kuwa na uraia pacha ili kuepuka usumbufu, ikiwa ni pamoja na uhalifu wanaofanyiwa na ndugu na jamaa zao wanapowatumia fedha kwa ajili ya kuwekeza kwenye vitega uchumi.

Mara kadhaa Serikali imetoa msimamo suala la uraia pacha, ikisema linasimamiwa na Sheria ya Uraia ya Tanzania sura ya 357, rejeo la mwaka 2002 inayotoa uraia pacha kwa watoto pekee na si kwa watu wazima.

Msimamo huo wa Serikali ulitolewa bungeni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo Aprili mwaka huu, akijibu swali la mbunge wa viti maalumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Suma Fyandomo aliyehoji sababu za Tanzanaia kutoruhusu uraia pacha.

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akijibu swali hilo alisema kama Serikali itaoa haja ya uwepo wa uraia pacha mchakato wake utafanyika.

Diaspora wanavyolizwa

Akizungumza na Mwananchi hivi karibuni, Michael Mlowe, diaspora wa Tanzania aliyeko Uingereza, amesema mkasa ambao hatausahau katika maisha yake ni kudhulumiwa mali zake na mtu anayemtaja kuwa mpenzi wake.

Mlowe anadai kuwa mtu huyo amemtapeli nyumba na viwanja baada ya kuwa anatuma fedha kwa nyakati tofauti kwa ajili ya kuvinunua.

“Ilikuwa mwaka jana tulitofautiana kidogo tu akaenda kukata RB polisi nikamatwe nitakapofika nchini, wakati sifahamu lolote. Nilirudi Tanzania nikakamatwa kwa kile kilichoelezwa nimekuja kumfanyia fujo,” amesema.

Mlowe anasema mtu wake huyo, alitoa maelezo yeye ni raia wa kigeni na anapofika nchini humsababishia fujo.

“Ninachoomba Serikali iangalie suala la uraia pacha ni muhimu sana, sisi tunaonekana sio raia na watu wanaiba mali zetu, hatuwezi kuwafanya lolote kwa sababu ya uongo wanaoutengeneza,” amesema.

Diaspora mwingine, Hamidu Mwasanyage anayeishi Marekani amesema wengi wanadhulumiwa na ndugu na marafiki wanapowatumia fedha za kununua mali nchini.

Amesema diaspora wanawaamini ndugu zao kwa uwekezaji kwenye mashamba na ujenzi wa nyumba, wanapodhulumiana wengine wana shtakiana na kifikishana mahakamani au kusamehe.

“Mimi rafiki yangu ninayeishi naye huku ndugu yake tumbo moja yupo Dar es Salaam alimsomesha hadi akamaliza chuo kikuu akaajiriwa, wakashauriana wanunue mashamba Morogoro.

“Basi akawa anamtumia fedha za kununulia, lakini ikawa kinyume mdogo wake akachukua fedha akaenda kuoa wake wawili kwa wakati mmoja,” amesema.

Tukio la pili, Mwasanyage amesimulia mke wake alikubaliana na marafiki zake kuchanga Sh10 milioni kununua viwanja Kigamboni na mwisho alidhulumiwa kiwanja.

Akisimulia tukio hilo Mwasanyage anasema kuna mtu alimtumia fedha mdogo wake baada ya kumwambia shamba ekari 10 linauzwa Sh25 milioni wilayani Kibaha (Pwani), alitumiwa Sh27 milioni, shamba lililonuliwa lilikuwa ekari tano.

Naye Mars Lyimo diaspora wa Tanzania nchini Norway amesema changamoto iliyomkumba nayo ni kudhulumiwa fedha zake hapa nchini.

“Rafiki yangu yupo Tanzania kanitafuta akaniomba nimsaidie fedha atanirejeshea, tangu nilipompa hadi sasa nikimtafuta simpati, uaminifu ni mdogo sana hata kwenye mashamba, tatizo ndio kubwa watu kudhulumiwa,” amesema.

Kwa upande wake, Adinani Milanzi diaspora wa Tanzania Afrika kusini, amesema alinunua shamba la ekari tano Kata ya Vianzi wilayani Mkuranga (Pwani) akimshirikisha kaka yake na mdogo wake.

“Niliamua kwenye hati ya shamba niweke jina la kaka yangu na langu ili iwe rahisi kufuatiia, kila nikirudi nchini kwenda kuangalia hilo shamba hakuna kinachofanyika, nikajaribu kuuza ikashindikana, nilivyoondoka na kurudi tena shamba tayari limeuzwa,” amesema.

 Milanzi amesema baada ya kufuatilia aliambiwa aliyeliuza shamba lile ameshafariki dunia na mwenyekiti wa Serikali za Mitaa alishakimbia ofisi.

Amesema hata alipouliza kwa kaka yake, alijibiwa atafuatilia bila utekelezaji, kitendo alichodai kilimfedhehesha hivyo kuamua kunyamaza ili kutoibua ugomvi na ndugu zake.

Akizungumzia jinsi ya kuondokana na changamoto hiyo kwa diaspora, Oscar Mkude mchambuzi wa masuala ya uchumi amesema malalamiko hayo pia wanayapata watu wengi wanoishi mbali na sehemu zao za asili.

“Tatizo hasa ni hali duni za kipato za hao wanaoombwa kusimamia fedha zinazotumwa, wanajikuta wanakosa uaminifu na kuanza kutumia fedha vibaya na hivyo kuathiri utekelezaji wa lengo kusudiwa,” amesema. 

Mkude amesema diaspora wanapaswa kutambua ni hatari kutumia mfumo wa kufahamiana kwenye utekelezaji wa miradi.

 “Nashauri watu, pamoja na diaspora, waanze kutumia taasisi zilizosajiliwa zinazofanya kazi kama hizo za usimamizi wa miradi na kulipwa ada ya huduma. Hii itawapa uwezo wa kuwawajibisha kisheria wanapofanya kinyume na makubaliano ya kimkataba,”

“Lazima kuanza kuchukulia uwekezaji wowote tunaoufanya kibiashara na kisheria zaidi, tuingie mikataba ya usimamizi ili tuwe na nguvu ya kuwawajibisha wale tuliowapa kazi na tunaowalipa fedha kwa kazi hizo, wanaposhindwa kutekeleza kwa mujibu wa mkataba,”amesema.

Mchango wa diaspora nchini

Ripoti ya mifumo kitaifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ya mwaka 2022 inaonyesha mwaka 2023 diaspora waliichangia Tanzania Sh829 bilioni.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading