Wakulima wa parachichi wafunguliwa soko China

Wakulima wa parachichi wafunguliwa soko China

Dar es Salaam. Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (Fao), kwa kushirikiana na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), limesaidia kampuni tatu za Tanzania kupata soko la parachichi nchini China.

Mafanikio hayo yanatokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau katika sekta ya kilimo na biashara.

Soko hilo limepatikana baada ya TPHPA kuwezeshwa kufuata utaratibu unaohitajiwa na Mamlaka Kuu ya Forodha wa China (GACC).

Msaada huo ulitolewa kuypitia mradi wa Kuimarisha Afya ya Mimea Tanzania kwa Usalama wa Chakula Ulioboreshwa, (STREPHIT), unaolenga kuboresha upatikanaji wa mazao ya kilimo salama na ya ubora wa juu kwa masoko ya kitaifa na kimataifa.

Akizungumzia soko hilo kupitia taarifa iliyotolewa na Fao leo Jumatano Septemba 4, 2024, Meneja wa Ufuatiliaji wa Afya ya Mimea na Uwezeshaji wa Biashara wa TPHPA, Mdili Katemani amesema,”kwa msaada kutoka kwa mshirika wetu Fao, tumekamilisha kwa mafanikio taratibu zinazohitajika na soko la China na kuruhusu wakulima na wazalishaji kuuza aina tatu za parachichi mbichi ambazo ni Hass, Fuerte na Pinkertons.”

Katemani ambaye pia ni Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa STREPHIT amesisitiza kuwa,  mafanikio haya ni matokeo ya juhudi za pamoja za Serikali ya Tanzania, ikiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan  na msaada wa kiufundi kutoka kwa Fao.

Ili wazalishaji wa ndani waweze kuuza parachichi China, wanapaswa kusajiliwa na GACC kupitia TPHPA.

Aidha, mashamba ya uzalishaji, vituo vya upakiaji na kampuni za kuondoa vijidudu lazima zisajiliwe na TPHPA ili kupata nambari za ufuatiliaji zinazohitajika kwa utambulisho wa wauzaji.

Zaidi ya hayo, mashamba haya yanapaswa kuzingatia mbinu bora za kilimo na usimamizi wa wadudu ili kudhibiti wadudu wa karantini kama vile nzi wa matunda, viwavi jeshi na vidukari.

Ufungaji, uhifadhi na usafirishaji wa parachichi lazima pia ufuate itifaki zote zilizokubaliwa kati ya Tanzania na China.

Mbali na parachichi, China imekuwa ikipokea mazao ya kilimo kutoka Tanzania, ikiwamo kahawa, soya, ufuta, korosho na mazao ya baharini.

Wakati wa ziara yake ya kidiplomasia nchini China mwaka 2023, Rais Samia alitia saini Itifaki ya Mahitaji ya Usafi wa Mimea kwa Mauzo ya Parachichi Mbichi kutoka Tanzania kwenda China, hatua iliyofungua njia kwa upatikanaji huu wa soko kihistoria.

Chini ya mradi wa STREPHIT, unaotekelezwa na Fao kupitia Umoja wa Ulaya (EU) na Serikali ya Tanzania, juhudi zinaendelea kuhakikisha mahitaji yote muhimu yanatimizwa ili kuweka mazao ya kilimo ya Tanzania katika soko la kimataifa.

Tanzania tayari inauza parachichi kwa nchi mbalimbali, zikiwamo India, Uholanzi, Kenya, Uingereza, Umoja wa Falme za Kiarabu, Afrika Kusini na Ufaransa.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading