Wakopaji wanaodhalilishwa mitandaoni wapewa mbinu

Wakopaji wanaodhalilishwa mitandaoni wapewa mbinu

Wakopaji wanaodhalilishwa mitandaoni wapewa mbinu

Dodoma. Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imewataka watu wanaomba mikopo kidijitali, kusoma maelekezo vizuri ili kuepuka kuruhusu kampuni hizo kuingia katika orodha ya namba za simu (phone book) na kuwadhalilisha. 

Kauli hiyo imekuja wakati baadhi ya kampuni zinazotoa mikopo kwa njia ya kidijitali, kutuma ujumbe mfupi wa maneno unaodhalilisha na wakati mwingine kutuma picha za vitambulisho vya wanaowadai.

Hatua hiyo imekuwa ikiibua malalamiko kwa jamii na hadi imekuibuliwa bungeni ambapo Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson alionyesha kukerwa na udhalilishaji unaofanywa kwa kuwashirikisha wasiohusika na mikopo hiyo.

Spika Tulia alieleza hayo Juni 27, 2024, bungeni wakati wa kipindi cha maswali na majibu akiitaka Serikali ieleze suala hilo ambalo lilikuwa likijadiliwa zaidi nje ya Bunge, “sijui kama kuna mwongozo wowote na Serikali mnalipokea na mnalifanyia kazi, hilo limekuaje.”

Aliyekuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alijibu suala hilo akikiri kuwepo kwa changamoto hiyo ya watu ambao wanakopeshana mitandaoni na baadaye wanatuma taarifa kwa watu wanaomzunguka mkopaji.

Nape alisema Serikali imeiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na Kitengo cha Kudhibiti Wizi Mtandaoni na Jeshi la Polisi kulifanyia kazi.

Aprili 1, 2024 Mwananchi iliripoti malalamiko ya baadhi ya watu wanaotumiwa ujumbe wa kuwataka kuwakumbusha waliokopa kulipa madeni yao, na jinsi kampuni zinavyopata namba hizo za simu. 

“Ndugu wa karibu/jamaa/rafiki/jirani wa (jina la mkopaji na namba ya simu) aliyechukua mkopo kwa nia ya mtandao kupitia application ya… unafahamishwa kuwa mtu huyu amekiuka makubaliano kwa kutolipa deni siku husika ya marejesho na kutopokea simu za ofisi, hivyo tutamchukulia hatua kwa kosa hilo.

“Unaombwa kumpigia simu muhusika na kumjulisha kuwa ana masaa mawili ya kulipa deni kabla ya hatua kali hazijachukuliwa dhidi yake. Fanya hivyo kuepuka usumbufu.”

Leo Jumatatu, Novemba 25, 2024, Mkurugenzi Mkuu wa PDPC, Dk Emmanuel Mkilia akizungumzia maandalizi ya warsha ya kuongeza uelewa kuhusu dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi jijini Dodoma amegusia suala hilo la udhalilishaji. 

“Kimsingi tumeona kuna uvunjifu mkubwa wa sheria ya ulinzi wa Taifa, hasa watu wanaotumia mitandao wanapata nafasi kutumia picha na vitambulisho vya watu na wanatumia sms (ujumbe mfupi wa maneno) kwa watu wote walioko ndani ya simu husika hilo ni kosa kisheria,” amesema. 

Amesema suala hilo wamekuwa wakilishughulikia kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kuhakikisha taasisi ndogo za fedha ziwe zimesajiliwa kisheria na BoT. 

Amesema wanaofanya biashara hiyo wanatakiwa kuzingatia sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi na ndio maana wengi wamefungiwa hivi karibuni kujishughulisha na biashara hiyo. 

Amesema mwananchi anapoomba mkopo kupitia programu tumizi ‘application’ hizo kwa kujua ama kwa kutokujua inakuwa ni sharti kama hutalipa deni hilo ambalo wanawataka aruhusu ili waweze kuingia kwenye orodha ya namba za simu (phone book) na kuangalia anwani ya watu unaowasiliana nao. 

Dk Mkilia amesema bila kujua mwananchi anapoweka alama ya tiki, application hiyo inakuwa na ruhusa ya kuingia katika orodha ya namba za simu, hivyo hata wakati mwingine kabla ya muda wa kulipa kufika taarifa zinapelekwa za kumkashifu huyo mtu kwa watu wote anawasiliana nao. 

“Kuwaasa wananchi kupitia vizuri maelekezo yanayoelekezwa mle ile usijikute kuwa ni mwathirika,” amesema. 

Tayari BoT imezifungia kutoa mikopo programu tumizi (application) 69 baada ya kuzibaini zinaendesha shughuli hiyo kidijitali bila kuwa na leseni wala idhini.

BoT ilitangaza uamuzi huo Novemba 21, 2024 kupitia taarifa iliyosainiwa na Gavana wa Bot, Emmanuel Tutuba ikiutahadharisha umma wa Watanzania kutojihusisha na majukwaa na programu tumizi zilizofungiwa.

Kuhusu warsha ya kuongeza uelewa juu ya dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi, Dk Mkilia amesema warsha hiyo itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 17 hadi 18, 2024 ambapo washiriki ni maofisa ulinzi wa taarifa binafsi (DPOs) wa taasisi za umma na binafsi. 

Amesema lengo ni kuelimisha wadau wa ulinzi wa taarifa binafsi nchini na kutoa elimu pamoja na maarifa muhimu kwa taasisi za umma na binafsi kuhusu utekelezaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya mwaka 2022 na kanuni zake.  

Dk Mkilia amesema katika kutekeleza agizo la Rais Samia Suluhu Hassan alilolitoa Aprili 3,2024 wakati akizindua tume hiyo taasisi 700 za umma na binafsi zimejisajili katika tume hiyo.

Mwakilishi wa Kampuni ya Hilton Law Group ambao wanashirikiana na PDPC katika warsha hiyo, Wakili Dorothy Ndazi amesema ni muhimu kwa taasisi zote kuelewa wajibu wao kuhusu dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi. 

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading