Utafiti: Marekani huchangia misaada ya Sh7.3 trilioni Tanzania kila mwaka

Utafiti: Marekani huchangia misaada ya Sh7.3 trilioni Tanzania kila mwaka

Dar es Salaam. Wakati uhusiano kati ya Tanzania na Marekani ukifikisha miaka 63, imebainika Tanzania imekuwa ikipokea misaada inayofikia Sh7.32 trilioni kila mwaka kwa miaka 10 mfululizo tangu mwaka 2012.

Ripoti ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya William and Mary’s Global Research institute na Taasisi ya Utafiti wa Kundoa Umasikini (Repoa) imetaja sekta zilizoguswa na msaada huo ni afya, elimu, kilimo, biashara na utalii.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Juni 18, 2024 jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa ripoti ya Kuwekeza kwa Watu Tanzania, iliyokusanya takwimu za miaka 10 iliyopita kuanzia mwaka 2012 hadi 2023.

Akitoa matokeo ya utafiti huo, mtaalamu mwandamizi wa sera wa taasisi ya AidData, Divya Mathew amesema umejikita katika ushirikiano wa kifedha kati ya Tanzania na Marekani.

“Tumechukua takwimu za misaada na biashara iliyofanyika ikihusisha Serikali na sekta binafsi ikiwa pamoja na mtu mmoja mmoja zikiwamo fedha zilizotolewa na Watanzania waishio Marekani.

“Tumeona kuna wastani wa Dola2.8 bilioni (Sh7.32 trilioni) zinazoingia kwenye uchumi wa Tanzania kwa miaka kwa miaka 10 mfululizo,” amesema Mathew.

Akizungumzia utafiti huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Repoa, Dk Donald Mmari amesema utafiti huo umeonyesha kuwepo kwa mafanikio kwa pande zote mbili.

“Kwa mfano katika sekta ya afya kumekuwa na msaada ya takribani Dola 394 milioni (Sh1 trilioni) hususani katika magonjwa ya Ukimwi na malaria na kumekuwa na mafanikio ya kupunguza vifo vitokanavyo na magonjwa hayo,” amesema Dk Mmari.

Ametaja pia maeneo ya usalama wa chakula na sekta binafsi akisema yameguswa.

“Kuna eneo la miundombinu, Shirika la Millenium Challenge liliwekeza takribani Dola 700 milioni (Sh1.83 trilioni) katika barabara na umeme.

“Kuna maeneo ya ulinzi na usalama, kuna biashara na uwekezaji katika madini na utalii. Kuna kampuni za Tanzania zimeuza bidhaa zake katika soko la Marekani, fursa iliyotokana na Sheria ya Agoa inayotoa fursa kwa wazalishaji wa Afrika kuuza bidhaa bila kutozwa ushuru,” amesema Dk Mmari.

Ametaja pia ubadilishanaji wa wataalamu, akisema kuna walimu wa Marekani wanaokuja kufundisha Tanzania na kufanya utafiti na pia wapo wanafunzi wanaokwenda kusoma Marekani kwa ufadhili.

Mkurugenzi wa uchambuzi wa sera wa AidData, Samantha Custer amesema licha ya uhusiano wa muda mrefu wa nchi hizo mbili, viongozi na wananchi wengi wa Tanzania hawana taarifa za kutosha, hasa wakati huu ambao Tanzania inatathmini mafanikio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025.

“Ni matumaini yetu, ripoti hii itasaidia kuwaelewesha watunga sera kuona kama ushirikiano wa Marekani na Tanzania unachangia ukuaji wa uchumi wa Tanzania,” amesema Dk Mmari.

Akizungumzia mchango wa Marekani katika sekta ya kilimo na usalama wa chakula nchini, Profesa David Nyange amesema miongoni mwa miradi iliyoonyesha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili ilikuwa ni ujenzi wa Chuo cha Kilimo cha Morogoro kilichobadilishwa kuwa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA).

“Chuo hiki kimechangia katika kuzalisha rasilimali katika sekta mama ya kilimo kinachozalisha chakula,” amesema Profesa Nyange.

Ametaja miradi mingine ni ushirikiano katika utafiti wa kilimo uliohusisha vyuo vikuu mbalimbali vya Marekani.

“Ushirikiano pia umeonekana kwa ushirika wa wahitimu wa Chuo Kikuu cha SUA (Sugeco) kwa kuwezesha kupeleka zaidi ya wahitimu 200 nchini Marekani na kuwaunganisha na programu za kilimo biashara,” amesema Profesa Nyange.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

High Court rejects Transworld’s application
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

High Court rejects Transworld’s application

The High Court in Dar es Salaam has struck out an application in which Transworld Aviation, a ground handler at the Abeid Aman Karume International Airport (AAKIA) was seeking permission to sue the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA).Continue Reading

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading