Utafiti kufanyika kubaini sumu ya samaki aina ya kasa

Utafiti kufanyika kubaini sumu ya samaki aina ya kasa

Unguja. Baada ya kutokea vifo vya mara kwa mara vinavyotokana na ulaji wa samaki aina ya kasa, sasa utafanyika utafiti wa sumu asili (Biotoxin) zilizomo ndani ya samaki huyo kuzitambua na athari zake.

Baada ya kutambua sumu hizo, elimu itakayopatikana kutokana na utafiti huo itatumika katika kuelimisha jamii kuhusu athari zitokanazo na ulaji wa kasa. 

Hatua hiyo inakuja baada ya kutokea vifo na  wengine kulazwa hospitalini baada ya kula nyama ya kasa katika visiwa vya Unguja na Pemba ambapo tukio la Machi 5, mwaka huu walikufa watu tisa na wengine 98 kulazwa hospitalini baada ya kula kasa katika Kisiwapanza Pemba. 

Hayo yamebainishwa leo Jumanne, Mei 21, 2024 na Waziri mwenye dhamana, Shaaban Ali Othman katika Mkutano wa Bajeti wa 15 wa Baraza la wawakilishi unaoendelea Chukwani mjini hapa. Hata hivyo, hakusema utafiti huo unatarajia kuanza lini. 

Shaaban alikuwa akijibu swali la mwakilishi wa Kiwani, Mussa Foum Mussa aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali kudhibiti vifo inavyotokana na ulaji wa samaki huyo. 

Kwa mujibu wa kifungu cha saba, sheria namba saba ya mwaka 2010 inapiga marufuku kuvua samaki huyo na ulaji wake,  lakini wavuvi wamekuwa wakiendelea kumvua na wananchi kumla bila kujali athari zake. 

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Shaaban Ali Othman akijibu maswali ya Wawakilishi katika mkutano wa 15 wa Bajeti Chukwani Unguja.

Alipouliza kitu gani kinafanyika kwa watu wanaobainika kufanya makosa hayo licha ya sheria kukataza, mwakilishi wa nafasi za wanawake, Shadya Mohamed Suleiman, Waziri Shaabani amesema wanawakamata na kuchukuliwa hatua. 

Amesema mpaka sasa kuna wavuvi wanne wameshikiliwa katika Mkoa wa Kusini Unguja na kesi zao zinaendelea kusikilizwa. Kwa mujibu wa sheria hiyo, mtu anayevua kasa anatozwa faini kati ya Sh100,000 na Sh5 milioni au kifungo. 

Hata hivyo, Waziri Shaaban amesema wavuvi wanaoendelea kuvua kasa wanapata nguvu kutoka kwa Wawakilishi hao ambao pindi wakikamatwa wanawatumia kutaka waachiliwe, hivyo aliwataka kuacha tabia hiyo na sheria ichukue mkondo wake.

 “Hapa lazima tuseme ukweli, wapo baadhi ya wawakilishi wanaochangia suala hili liendelee kwani tunapochukua hatua za kuwakamata, tunapigiwa simu kuwa tuwaachie sasa tusaidiane tuache kufanya hivyo,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading