Ushuru kwenye ‘tomato sauce’ wapingwa

Ushuru kwenye ‘tomato sauce’ wapingwa

Dar es Salaam. Hatua ya Serikali kupendekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha Sh300 kwa kilo ya tomato sauce na tomato ketchup, chilli sauce na chilli ketchup zinazotoka nje ya nchi, imeelezwa na wadau wa uchumi kuwa inatokana na kukosekana ubunifu wa vyanzo vya mapato.

Akiwasilisha bajeti ya Serikali kwa mwaka 2024/25 bungeni Juni 13, 2024, Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba alisema lengo la hatua hiyo ni kuongeza mapato ya Serikali na kupata fedha za fidia ya athari hasi zinazotokana na matumizi ya sukari na chumvi iliyopo katika bidhaa hizo, hatua ambayo alisema inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa Sh634 milioni.

Baadhi ya wachumi na wataalamu wa lishe waliozungumza na Mwananchi Juni 15, 2024 wamesema kama Serikali imekusudia kudhibiti matumizi ya bidhaa hizo haipaswi kuzungumzia suala la makusanyo.

Wamehoji ni kwa namna gani mtu aliyeathiriwa na bidhaa hizo anapatiwa fidia.

Dk Godfrey Malisa, mchambuzi wa masuala ya siasa na uchumi, amesema ushuru unaopendekezwa ni kutokana na bajeti kuwa tegemezi kwa kiasi kikubwa, akisisitiza Tanzania ina vyanzo vingi vya mapato lakini hakuna ubunifu wa kupata vipya badala yake vitu vidogo ambavyo tayari vina kodi vinaenda kuongezewa mzigo.

“Zipo nyingi zina athari na hazijaguswa, ukisema unaweka kodi hizi kwa sababu hiyo, ukiingia sokoni zipo bidhaa zina athari kubwa kuliko hizo na hazijaguswa, ukiongeza hizo hela ndiyo suluhu ya kupunguza athari?”amehoji Dk Malisa.

Amesema wananchi wa kawaida hivi sasa wamekatishwa tamaa kulipa kodi kwa hiari kutokana na matumizi yake kutoendana na mahitaji yao.

Profesa Haji Semboja, mwanataaluma ya uchumi amesema nchi yoyote, kutokana na sera zake, inaweza kuweka mbinu ya kutekeleza sera kutokana na sababu za kimaisha, mazingira, kisiasa na kiuchumi.

“Kuongeza ushuru kwenye bidhaa maana yake hutaki mtu huyo atumie kitu hicho kutokana na sababu za kiafya, mfano sigara na vilevi na hii inaweza kutekelezwa kupitia sera za nchi au nje ya nchi, tatizo ni kwamba ukisema unatekeleza hilo kupata fedha si sahihi, ulipaswa tuishie kuzuia athari,” amesema.

Amesema uwekaji wa ushuru kwenye bidhaa hizo iwe ni kwa sababu za kiafya pekee na si kuongeza mapato.

Mtaalamu wa lishe, Emmanuel Maganga amesema kuweka ushuru kwa bidhaa zinazotoka nje kwa lengo la kufidia athari kiafya, haina maana.

“Kwa hiyo fidia mtu aliyeathirika anasaidiwaje? Sioni kama ina mantiki kwa sababu tayari umeruhusu na watu wanaathirika na unapokea fidia hiyo, ina maana gani?” amehoji.

Hata hivyo, mtaalamu wa lishe kutoka Shirika la Chakula la Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), Stella Kimambo amesema kiafya matumizi ya vyakula vilivyosindikwa viwandani si salama kwa afya.

Amesema hatua ya kuwekwa ushuru ni moja ya mikakati ya kuwasaidia wananchi kuondokana na matumizi ya bidhaa hizo ambazo zimekuwa na mchango mkubwa wa maradhi yasiyo ya kuambukiza kama kisukari, maradhi ya moyo na kiharusi.

“Hata nchi zingine zinapoona chakula kina madhara, zinaweza kuongeza ushuru.  Tuna nyanya nyingi na zinapotea kutokana na kutokuwa na viwanda, hatua hizi za kutoza ushuru bidhaa za nje ni sehemu ya kuimarisha soko la ndani,” amesema.

Akizungumzia madhara ya chumvi, mtaalamu wa lishe, Fatma Mwasora amesema japo bidhaa hiyo ina umuhimu mwilini, matumizi yake yanapaswa kuwa madogo.

“Watu wenye matatizo ya maradhi ya kudumu wanapaswa kupata ushauri kwa daktari,” amesema.

Miongoni mwa hatari za matumizi ya chumvi na sukari ni kuchangia shinikizo la juu la damu, kisukari, moyo, kiharusi na saratani, magonjwa ambayo kwa mujibu wa Wizara ya Afya, bajeti ya kuhudumia magonjwa yasiyoambukiza iliongezeka mara tatu mwaka 2021/22 hadi kufikia Sh99.08 bilioni ukilinganisha na Sh35.65 bilioni mwaka 2016/17.

Takwimu zinaonyesha shinikizo la juu la damu lipo kati ya asilimia 20 hadi 30 ikiwa na maana kuwa katika kila wananchi 10, wawili hadi watatu wana tatizo hilo.

Uhalisia ulivyo

Kwa mujibu wa tovuti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kiwango cha chumvi ambacho ni salama kinachopendekezwa kutumika kwa siku ni miligramu 1,500 takribani nusu kijiko cha chai na isizidi miligramu 2,000.

Bidhaa ya tomato Ketchup kwa mujibu wa Taasisi ya Moyo ya British Heart Foundation ya nchini Uingereza, kuna gramu 0.3 za chumvi na gramu 4.1 ya sukari kwenye kijiko kikubwa cha chakula cha bidhaa hiyo.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal

Ruling party Chama Cha Mapinduzi-Zanzibar has said it is ready to task state organs to investigate some of the claims against its government that have been raised by opposition politicians on the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA).Continue Reading