Ukuaji wa watoto nchini waiibua serikali

Ukuaji wa watoto nchini waiibua serikali

Ukuaji wa watoto nchini waiibua serikali

Dodoma. Zaidi ya nusu ya watoto nchini hawako katika ukuaji sahihi unaotakiwa huku ikielezwa kuwa hali hiyo inaweza kuongezeka ikiwa juhudi za makusudi hazitachukuliwa.

Takwimu hizo zimetolewa leo Februari 28,2025 jijini Dodoma na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dk Dorothy Gwajima wakati akifungua mafunzo ya waandishi wa habari wanaojisisha na taarifa za mtoto.

Dk Gwajima amesema takwimu za kitafiti zinaonyesha asilimia 47 ya watoto nchi Tanzania ndiyo walionekana kuwa ukuaji sahihi uliotimilika, huku asilimia 53 hawakuwa kwenye ukuaji sahihi uliotimilika.

Kwa mujibu takwimu za mwaka 2022 za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha idadi ya watoto wenye umri wa kuanzia miaka 0-8 ambao wanatajwa walikuwa 16,694,763 ambayo ni asilimia 27.0 ya Watanzania hivyo kwa asilimia 53 inayoelezwa ni watoto 8.8 milioni.

Katika mafunzo hayo ambayo yameandaliwa na Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari nchini (UTPC) kwa kushirikiana na taasisi nyingine, yamewakusanya waandishi wa habari wanaoandika habari za mtoto kutoka mikoa 26 ya Tanzania Bara na yanafanyika kwa siku tatu.

Kwa mara ya kwanza mpango huo ulizinduliwa Desemba 23, 2021 na umetajwa kuwa na mafanikio makubwa kwa kutumia waandishi na radio za kijamii.

“Hali hii tunayoiona kwa sasa itakuwa mbaya zaidi kwa siku zijazo kama hatutaweza kuchukua hatua za makusudi, lazima tubadili mtazamo kuanzia mtu anapokuwa na mimba hadi mtoto atakapofikisha miaka minane,” amesema Dk Gwajima.

Waziri amesema wazazi wengi wanadanganywa na unene wa watoto wao wakiamini ndiyo wapo kwenye afya nzur, wakati hakuna ukweli kwenye jambo hilo.

Amewataka waandishi wa habari kutumia kalamu zao vema kulisaidia Taifa la kesho hasa kuwaelimisha watu watambue afya  za watoto wao tangu wakiwa wadogo,  huku akisisitiza zaidi hatari zinazowapata watoto wa vijijini.

Mratibu wa Ubora wa huduma za Tiba kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi, Dk Pius Kagoma amesema ulinzi na usalama ni kwa mtoto ni sehemu ya makuzi. “Lakini jambo kubwa ni lishe toshelevu.

Dk Kagoma amewaambia waandishi wa habari kwamba Serikali itaendelea kuweka mkakati wa kuwalinda watoto,  ambapo matokeo yatakuwa chanya iwapo waandishi watatumia zaidi kalamu zao kufikisha ujumbe kwa jamii.

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Jamii, Mathia Haule amesema watoto wengi wamekuwa waathirika wa ukatili na mara nyingine kesi zinamalizwa ngazi ya kaya na familia, jambo ambalo limekuwa chanzo na kichaka cha kuficha uhalifu.

Haule amesema kalamu pekee zinaweza kufichua mambo hayo hivyo waandishi wanahimizwa kujengewa uwezo kuhusu malezi na makuzi ya awali ya mtoto.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading