Uchaguzi, amani vyasisitizwa maadhimisho miaka 85 ya TAG

Uchaguzi, amani vyasisitizwa maadhimisho miaka 85 ya TAG

Dar es Salaam. Waumini wa Kanisa Tanzania Assemblies Of God (TAG) wameadhimisha miaka 85 tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo, huku wakisisitizwa kulinda amani na kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa baadaye mwaka huu.

Ibada ya maadhimisho hayo imefanyika leo Jumapili, Julai 14, 2024 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini hapa, ikihudhuriwa na maelfu ya waumini kutoka mataifa 11 akiwamo Rais mstaafu wa Benin, Thomas Boni Yayi.

Akizungumza katika ibada hiyo, Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, amewasisitiza waumini na Watanzania wote waliofikia umri wa kupiga kura, kujitokeza kushiriki hatua hiyo muda ukifika.

Amesema, Julai 20 watakapozindua uboreshaji wa daftari la mpiga kura, watu wajitokeze kujiandikisha na kuboresha taarifa zao.

“Jambo muhimu ambalo ni haki yenu, mwaka huu kuna uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kila Mtanzania anayo haki kuchagua au kugombea, tutakapozindua maboresho ya daftari la mpiga kura Julai 20, kila mmoja aende kuhakiki jina lake.

“Waliobadili makazi pia waende kuhamisha taarifa zao na kila Mtanzania ajiweke tayari kwa uchaguzi na wenye sifa za kugombea wakagombee,” amesema Majaliwa.

Waziri Mkuu pia aligusia umuhimu wa amani na kuwasisitiza waumini hao na Watanzania kuendelea kuilinda.

“Sote tunafahamu umuhimu wa amani tuendelee kuliombea Taifa, tumuombee Rais wa nchi yetu,” amesema Waziri Mkuu wakati akitoa salamu za Rais akieleza amemuagiza kumwakilisha kwa kuwa yeye (Rais) ana majukumu mengine ya kitaifa.

Majaliwa pia amelipongeza kanisa hilo kwa kufanya waumini kuwa wamoja, pia kusapoti juhudi za Serikali katika elimu na afya.

“Serikali inatambua michango ya taasisi za dini katika jamii na kuchochea maendeleo ikiwamo TAG, pia tunawategemea katika kuimarisha maadili na umoja.”

“Nchi zetu za Afrika zinapata athari ya kuiga utamaduni wa nje, makanisa yameendelea kukemea na kama Serikali tunawategemea katika kampeni hii ya maadili kwa kuendelea kutumia mahubiri yenu kuijenga jamii,”amesema.

Awali, Askofu Mkuu wa makanisa ya TAG, Mchungaji Barnabas Mtokambali aliipongeza Serikali katika sekta ya usafirishaji, akielezea namna ambavyo treni ya umeme imekuwa mkombozi.

“Tangu nikiwa Askofu msaidizi hadi nilipokuwa Askofu Mkuu nilikuwa nasafiri na mabasi wakati mwingine hadi napanda malori kutoka Morogoro ninapoishi kuja Dar es Salaam au kwenda Dodoma, ilipoanza treni ya umeme, imeleta unafuu sana, haya ni maendeleo,” amesema.

Ibada hiyo ilihudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wakiwamo maaskofu wakuu kutoka nchi mbalimbali, baadhi ya wabunge na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila.

Akitoa taarifa ya kanisa Katibu Mkuu wa TAG, Mchungaji Joseph Marwa amesema tangu kuanzishwa mwaka 1939, limefanya mambo mbalimbali ya maendeleo.

Amesema, Askofu Mkuu Mtokambali, ameiongoza TAG ilipokuwa na mikoa 10 ya kikanisa hadi sasa.

Amesema tangu wakati huo, TAG imetoa huduma za kijamii katika sekta ya elimu kwenye shule za msingi 17 za sekondari saba na za chekechea 117 na inaendelea  na ujenzi wa shule nyingine nane.

“Kanisa pia lina vyuo vya ualimu viwili, linatoa huduma za zahanati na vituo vya afya na vingine vinaendelea kujengwa ili kuihudumia jamii,” amesema.

Ibada hiyo ilianza saa 11 Alfajiri kwa waumini kutoka maeneo mbalimbali kuanza kuwasili hadi saa 1 asubuhi ilipozinduliwa na iliyofikia tamati saa 8:41 mchana.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’
Top News
Chief Editor

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Monrovia — The Rwanda Minister of State responsible for Health, Dr. Yvan Butera, cautioned that while the country is beginning to see positive signals in its fight against the Marburg virus, the outbreak is “not yet over”. He, however, expressed hope that  “we are headed in that direction”. The minister said the epidemiology trend, since the disease was first discovered in the country more than a month ago, is moving towards fewer cases.

Dr. Butera, who was giving updates during an online briefing yesterday, said in the past two weeks, only two deaths were recorded while 14 people recovered from the disease. He said Rwanda was expanding its testing capacity with 16,000 people already inoculated against the disease.

The priority right now, Butera said, is “rapid testing and detection”.

Marburg is a highly virulent disease transmitted through human-to-human contact or contact with an infected animal. The fatality rate of cases, which has varied over the period, is more than 50%, according to the World Health Organization.  WHO said the highest number of new confirmed cases in Rwanda were reported in the first two weeks of the outbreak. There’s been a “sharp decline” in the last few weeks, with the country now tackling over 60 cases.

At Thursday’s briefing, a senior official of the Africa Centers for Disease Control, Dr. Ngashi Ngongo, said mpox – the other infectious disease outbreak that countries in the region are fighting – was been reported in 19 countries, with Mauritius being the latest country to confirm a case. He said although no new cases have been recorded in recent weeks in several countries where outbreaks occurred previously –  including Cameroon, South Africa, Guinea, and Gabon – Uganda confirmed its first Mpox death. This, he said, is one of two fatalities reported outside Central Africa.

Dr. Ngashi revealed that there was an increase in cases in Liberia and Uganda. He said mpox cases were still on an upward trend.

“The situation is not yet under control.”

Source: allafrica.com

Continue Reading