TTPHPA kuongeza nguvu mikoa inayovamiwa na visumbufu mimea

TTPHPA kuongeza nguvu mikoa inayovamiwa na visumbufu mimea

Arusha. Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) inatarajia kuongeza nguvu katika mikoa inayoonekana kuvamiwa zaidi na visumbufu mimea hasa wadudu na ndege waharibifu, ili kukabiliana na hasara wanayoipata kutokana na uharibifu wa mazao unaofanywa na wadudu pamoja na ndege hao.

Hayo yamebainishwa leo Juni 17, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Profesa Joseph Ndunguru alipozungumza na watafiti wa taasisi hiyo kuhusu kuimarisha utendaji kazi, sambamba na kutambulisha tuzo waliyopewa na Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kuibuka mshindi wa kwanza wa mamlaka iliyotoa gawio kubwa serikalini.

Amesema changamoto kubwa kwa sasa kwa wakulima ni ndege aina ya kweleakwelea na kwamba wamefanikiwa kuwadhibiti zaidi ya milioni 40 na kuokoa zaidi ya tani 5,675 za nafaka hasa mpunga, mtama na alizeti.

“Ndege hao tumewadhibiti katika mikoa ya Morogoro, Tabora na Manyara kwa kutumia viuatilifu kwa njia ya ndege nyuki, lakini bado kuna mikoa wanasumbuliwa, hivyo mamlaka iko nyuma yao, watoe taarifa na sisi tutaweka kambi huko,” amesema Profesa Ndunguru.

Akizungumzia tuzo hiyo, Professa Ndunguru amewataka wafanyakazi kuendelea kufanya kazi itakayosaidia nchi kutimiza malengo yake ya kujitosheleza kwa chakula, kuongeza mchango wa sekta ya kilimo kiuchumi.

“Tusiridhike na tuzo hii bali tuongeze nguvu ya kufanya kazi na sisi kama mamlaka tutahakikisha tunaboresha miundombinu ya kazi, ikiwemo ununuzi wa magari zaidi ya tisa yatakayokuja hapa Agosti na kusambazwa kwenye idara zenu.

“Mkaongeze nguvu kwenye kufikia maeneo yote, ili kupambana na visumbufu vya mimea, lakini pia kurahisisha ukaguzi wa viuatilifu visivyo na ubora mikoani,” amesema Profesa Ndunguru.

Amesema katika ukusanyaji wa maduhuri ya mwaka 2023/2024, mamlaka imekusanya Sh19.7 bilioni kama mapato ya ndani na kufanikiwa kutoa Sh3.7 bilioni kama gawio serikalini na fedha zilizobaki zitakwenda kuimarisha utendaji kazi katika idara zote.

Kwa upande wake, mwenyekiti wa wafanyakazi kutoka TPHPA, John Elia ameupongeza uongozi wa mamlaka kwa kupewa tuzo hiyo na kuitaka Serikali kuboresha mazingira na maslahi ya wafanyakazi, ili kuongeza ufanisi zaidi kazini.

“Ni kongole kwetu wote maana utendaji na kujitoa kwetu ndio umeleta mafanikio ya upatikanaji wa fedha hiyo iliyotolewa gawio, hivyo Serikali ione ni wakati mwafaka sasa wa kuongeza maslahi ya wafanyakazi, ili mafanikio haya yaonekane zaidi,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading