TMA yatoa tahadhari ya upepo mkali kwa siku tatu mfululizo

TMA yatoa tahadhari ya upepo mkali kwa siku tatu mfululizo

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya uwezekano wa kutokea kwa upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa, kwa siku tatu mfululizo kuanzia leo Jumapili Septemba 1 hadi 3, 2024 katika baadhi ya mikoa nchini.

Upepo huo unatarajiwa kutokea katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa kusini mwa Ziwa Tanganyika ikiwemo mikoa ya Rukwa na Katavi na kugusa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi ikiwemo mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani na kujumuisha visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.

Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa ya utabiri wa hali ya hewa kwa siku tatu zijazo  kuanzia leo Jumapili Septemba Mosi, 2024 uliotolewa na TMA.

Taarifa hiyo imeyataja baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya kusini mwa bahari ya Hindi yatakayoguswa ni mikoa ya Lindi na Mtwara.

“Athari zinazoweza kujitokeza ni kuathirika na kughairishwa kwa baadhi ya shughuli za baharini na kuharibika kwa miundombinu ya bahari, hivyo ni vyema kuchukua tahadhari,” imeeleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, siku ya leo limetolewa angalizo la upepo mkali unaotarajiwa kufikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili,  huku ukitajwa kugusa baadhi ya maeneo ya ukanda wa kusini mwa ziwa Tanganyika ikiwemo mikoa ya Katavi na Rukwa.

Pia angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi inayohusisha mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, visiwa vya Mafia,Unguja na Pemba.

“Athari zinazoweza kujitokeza ni kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi, uvuvi na usafirishaji baharini,” imeeleza taarifa hiyo.

Kesho Jumatatu Septemba 2, 2024, taarifa hiyo inatoa tahadhari ya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa, mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili  katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kusini mwa bahari ya Hindi hasa mikoa ya Lindi na Mtwara.

Uwezekano wa kutokea kwa upepo huo unatajwa kuwa mkubwa licha ya athari zake kuwa kiwango cha wastani.

“Angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili  limetolewa pia kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi  ikiwemo mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.”

 “Pia ukanda wa kusini mwa Ziwa Tanganyika katika mikoa ya Katavi na Rukwa na ukanda wa Ziwa Nyasa ikiwemo mikoa ya Ruvuma na Njombe,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Septemba 3, 2024 tahadhari ya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili,  imetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kusini mwa bahari ya Hindi ikiwemo mikoa ya Lindi na Mtwara.

Pia angalizo la upepo huo limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi ambayo ni mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia, Unguja, Pemba, Lindi na Mtwara.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading

High Court rejects Transworld’s application
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

High Court rejects Transworld’s application

The High Court in Dar es Salaam has struck out an application in which Transworld Aviation, a ground handler at the Abeid Aman Karume International Airport (AAKIA) was seeking permission to sue the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA).Continue Reading

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading