TMA yatoa tahadhari ya upepo mkali kwa siku tatu mfululizo

TMA yatoa tahadhari ya upepo mkali kwa siku tatu mfululizo

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya uwezekano wa kutokea kwa upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa, kwa siku tatu mfululizo kuanzia leo Jumapili Septemba 1 hadi 3, 2024 katika baadhi ya mikoa nchini.

Upepo huo unatarajiwa kutokea katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa kusini mwa Ziwa Tanganyika ikiwemo mikoa ya Rukwa na Katavi na kugusa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi ikiwemo mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani na kujumuisha visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.

Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa ya utabiri wa hali ya hewa kwa siku tatu zijazo  kuanzia leo Jumapili Septemba Mosi, 2024 uliotolewa na TMA.

Taarifa hiyo imeyataja baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya kusini mwa bahari ya Hindi yatakayoguswa ni mikoa ya Lindi na Mtwara.

“Athari zinazoweza kujitokeza ni kuathirika na kughairishwa kwa baadhi ya shughuli za baharini na kuharibika kwa miundombinu ya bahari, hivyo ni vyema kuchukua tahadhari,” imeeleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, siku ya leo limetolewa angalizo la upepo mkali unaotarajiwa kufikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili,  huku ukitajwa kugusa baadhi ya maeneo ya ukanda wa kusini mwa ziwa Tanganyika ikiwemo mikoa ya Katavi na Rukwa.

Pia angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi inayohusisha mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, visiwa vya Mafia,Unguja na Pemba.

“Athari zinazoweza kujitokeza ni kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi, uvuvi na usafirishaji baharini,” imeeleza taarifa hiyo.

Kesho Jumatatu Septemba 2, 2024, taarifa hiyo inatoa tahadhari ya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa, mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili  katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kusini mwa bahari ya Hindi hasa mikoa ya Lindi na Mtwara.

Uwezekano wa kutokea kwa upepo huo unatajwa kuwa mkubwa licha ya athari zake kuwa kiwango cha wastani.

“Angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili  limetolewa pia kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi  ikiwemo mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.”

 “Pia ukanda wa kusini mwa Ziwa Tanganyika katika mikoa ya Katavi na Rukwa na ukanda wa Ziwa Nyasa ikiwemo mikoa ya Ruvuma na Njombe,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Septemba 3, 2024 tahadhari ya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili,  imetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kusini mwa bahari ya Hindi ikiwemo mikoa ya Lindi na Mtwara.

Pia angalizo la upepo huo limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Kaskazini mwa bahari ya Hindi ambayo ni mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia, Unguja, Pemba, Lindi na Mtwara.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading