TIC yatabiri 2024 kuwa mwaka wa rekodi ya uwekezaji

TIC yatabiri 2024 kuwa mwaka wa rekodi ya uwekezaji

TIC yatabiri 2024 kuwa mwaka wa rekodi ya uwekezaji

Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Taifa cha Uwekezaji (TIC) Gilead Teri amesema huenda mwaka huu Tanzania ikavunja rekodi ya kujasili miradi mingi ya uwekezaji iliyodumu kwa miaka 11.

Teri alisema hadi Novemba 29, 2024 TIC ilikuwa imesajili jumla ya miradi 800, idadi ambayo ni kubwa ikilinganishwa na miaka ya hivi karibuni lakini pungufu ya rekodi iliyowekwa mwaka 2013 ambapo kituo kilisajili miradi 865.

Kiongozi huyo mwenye dhamana ya kuvutia na kusajili miradi nchini alisema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 20 ya kampuni ya vinywaji ya Mega Beverages iliyoenda sambamba na kutambulishwa kwa toleo maalumu la bidhaa yake ya K-Vant.

“Mwaka huu utakuwa mwaka wa rekodi, tangu mwaka 1997 tulipoanza kusajili rasmi miradi mwaka 2013 ndiyo unaoshikiria rekodi lakini sasa kuna uwezekano mkubwa wa kuivunja kutokana na ongezeko kubwa la miradi mwaka huu,” alisema Teri.

Teri aliongeza kuwa jambo zuri ni zaidi ni kuwa kati ya miradi iliyokuwa imesajili hadi Novemba 29, 260 ni ya wazawa na zaidi ya nusu ya miradi yote ina ushiriki wa Wazawa.

Teri alisema katika miradi iliyosajiliwa mingi ni ya uzalishaji wa bidhaa za mahitaji ya kila siku, sekta ya ujenzi, majengo, uchukuzi, kilimo na utalii.

Alisema mafanikio hayo ni matokeo ya mageuzi yaliyofanywa katika kuvutia uwekezaji kwa kubadilisha mazingira huku akisema kuwa yako thabiti na yanavutia kuliko wakati wowote ule katika nchi.

“Mbali na mazingira ya kisera yanayovutia pia Tanzania ina rasilimali nyingi, nishati ya uhakika, soko kubwa na nguvu kazi ya kutosha kufanya uzalishaji wenye tija na kumfanya mwekezaji kukua na kupata faida,” alisema.

Akizungumzia kuhusu miaka 20 ya Mega Teri alisema ni mafanikio makubwa kwani sekta waliyopo ni ngumu na ina ushindani mkubwa.

Hali ya sekta ya vinywaji

Katika hafla hiyo ambayo ilihudhuria na wadau mbalimbali, wafanyakazi wa Mega na baadhi ya wateja wao Teri alisema kusimama kwa kampuni hiyo ni ishara kuwa wazawa wanaweza.

“Mauzo ya sekta ya viwanjwa kwa mwaka 2023 yalifikia Dola za Marekani 3 bilioni (Sh8 trilioni), kati ya kiwango hicho vinywaji vikali vilikuwa na thamani ya mauzo ya Dola 721 milioni (1.8 trilioni),” alisema Teri.

Aidha Teri alisema kati ya vinywaji vyote vya Sh8 trilioni vilivyouzwa hapa nchini katika mwaka huo asilimia 80 hadi 90 vilikuwa vimezalishwa hapa nchini hususani bia.

“Tuna Imani kuwa ndani ya miaka miwili ijayo hiyo asilimia ya vinavyozalishwa nje ya nchi nayo itapungua au kumaliza kabisa na wazalishaji wa ndani. Tunavutia uwekezaji wa wanaozalishaji nje ya nchi waje zalishe hapa,” alisema.

Awali akizungumza katika hafla hiyo Meneja wa Chapa ya K-Vant Awatif Bushiri alisema mpaka sasa kinywaji chao kinauzwa katika mataifa manne nje ya nchi, ambayo ni Kenya, Rwanda, Congo DRC na Malawi.

Kuhusu toleo maalumu la chapa yake Bushiri alisema ni mahususi kwa ajili ya zawadi msimu huu wa sikukuu ndiyo maana imewekwa kwenye mwonekano wa kipekee huku ikipewa radha mpya na rangi ya dhahabu.

“Kwa kawaida spirit huwa haiwekwi kwenye maleo yam bao lakini hii imeweka, imepikwa kwa miezi mitatu ndiyo maana ina radhi ya dhahabu na radha ya kipekee,” alisema na kuongeza kuwa sasa itapatikana maduka hadi mapema mwaka 2025.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income

Insurer and financial services provider Britam posted a 22.5 percent jump in net earnings for the half-year ended June 2024, to Sh2 billion, buoyed by increased investment income.

The rise in half-year net profit from Sh1.64 billion posted in a similar period last year came on the back of net investment income rising 2.5 times to Sh13.27 billion from Sh5.3 billion.

“We are confident in the growth and performance trend that Britam has achieved, supported by its subsidiaries in Kenya and the region. Our business is expanding its revenue base while effectively managing costs,” Britam Chief Executive Officer Tom Gitogo said.

“Our customer-centric approach is fueling growth in our customer base and product uptake, particularly through micro-insurance, partnerships, and digital channels.”

The investment income growth was fueled by interest and dividend income rising 34 percent to Sh9.1 billion, which the insurer attributed to growth in revenue and the gains from the realignment of the group’s investment portfolio.

Britam also booked a Sh3.79 billion gain on financial assets at a fair value, compared with a Sh1.8 billion loss posted in a similar period last year.

The increased investment income helped offset the 12.7 percent decline in net insurance service result to Sh2.13 billion in the wake of claims paid out rising at a faster pace than that of premiums received.

Britam said insurance revenue, which is money from written premiums, increased to Sh17.8 billion from Sh16.6 billion, primarily driven by growth in the Kenya insurance business and regional general insurance businesses, which contributed 30 percent of the revenue.

The group has a presence in seven countries in Africa namely Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, South Sudan, Mozambique, and Malawi.

Britam’s insurance service expense hit Sh13.6 billion from Sh11.3 billion, while net insurance finance expenses rose 2.6 times to Sh12.3 billion during the same period.

“Net insurance finance expenses increased mainly due to growth in interest cost for the deposit administration business driven by better investment performance. This has also been impacted by a decline in the yield curve, which has led to an increase in the insurance contract liabilities. The increase has been offset by a matching increase in fair value gain on assets,” said Britam.

Britam’s growth in profit is in line with that of other Nairobi Securities Exchange-listed insurers, which have seen a rise in profits.

Jubilee Holdings net profit in the six months increased by 22.7 percent to Sh2.5 billion on increased income from insurance, helping the insurer maintain Sh2 per share interim dividend.

CIC Insurance Group posted a 0.64 percent rise in net profit to Sh709.99 million in the same period as net earnings of Liberty Kenya nearly tripled to Sh632 million from Sh213 million, while Sanlam Kenya emerged from a loss to post a Sh282.2 million net profit.

Continue Reading