Tanzania yapanda viwango vya uhuru wa habari

Tanzania yapanda viwango vya uhuru wa habari

Tanzania yapanda viwango vya uhuru wa habari

Dar es Salaam. Tanzania imepanda katika viwango vya uhuru wa habari kutoka nafasi ya 143 mwaka 2023 hadi nafasi ya 97 mwaka huu.

Takwimu hizo ni kwa mujibu wa ripoti ya Taasisi ya Waandishi wa Habari wasio na Mipaka (RSF).

Hata hivyo, Serikali ya Tanzania ina kila sababu ya kuongeza nguvu ya kuwalinda waandishi wa habari dhidi ya madhila kutokana na kuongezeka dhidi yao kwa mwaka huu 2024 ukilinganisha na miaka miwili iliyopita.

Hayo ni kwa mujibu wa Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura katika taarifa kwa umma aliyoitoa leo Novemba 2, 2024 katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya waandishi wa habari (IDEI).

Sungura pia ni Mwenyekiti wa umoja wa haki ya kupata taarifa nchini Tanzania (CoRI) na Mtandao wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika.

Kaulimbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu ni ‘Usalama wa waandishi wa habari wakati wa migogoro na dharura.

Amesema kati ya mwaka 2012 hadi Oktoba 2024 waandishi wa habari 316 walipatwa na madhila nchini, 44 kwa mwaka huu pekee ikiwa ni sawa na madhila 33.

Madhila hayo amesema yanahusisha kukamatwa kwa waandishi 31, vitisho (8), kutekwa na watu wasiojulikana (1), onyo kwa vyombo vya habari (4), chombo cha habari kufungiwa (4), kipindi kukatishwa kikiwa hewani (1), kusumbuliwa (1), kunyimwa taarifa (1), uhuru wa mahakama kuingiliwa (1) na kunyang’anywa vifaa (1). Kati ya hayo amesema wanaume ni 36 na wanawake ni wanane.

Sungura amesema mwaka 2022 madhila 19 yalirekodiwa, mwaka jana (23) na mwaka huu hadi leo Novemba 2, mwaka huu (33) yamerekodiwa.

“Madhila husika ni ya waandishi wa habari kukamatwa, kupewa vitisho, vyombo vya habari kupewa onyo, kufungiwa kufanya kazi, kuingilia uhuru wa mahakama na kuahirisha kipindi kwenda hewani,” amesema.

Sungura amesema CoRI inaunga mkono mazungumzo kati ya Serikali na wadau wa habari katika kujenga mwafaka wa kukabiliana na ukatili dhidi ya waandishi wa habari hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2025.

Kwa mujibu wa taarifa za ufuatiliaji za Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) kuhusu ukatili dhidi ya waandishi wa habari, kiwango cha ukatili ni kikubwa.

Kati ya mwaka 2006 hadi 2024 zaidi ya waandishi 1,700 wameuawa duniani na kesi za mauaji hayo asilimia 90 hazijatatuliwa mahakamani.

“Sote tunajua umuhimu wa waandishi wa habari, hivyo ukatili dhidi yao una madhara makubwa katika kukuza na kulinda demokrasia ya kila taifa duniani,” amesema Sungura.

Amesema Mtandao wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika (NIMCA) na CoRI, kwa pamoja yanapinga ukatili dhidi ya waandishi wa habari kote duniani.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading