Tanzania yajipanga kuwa kinara teknolojia ya Metaverse Afrika

Tanzania yajipanga kuwa kinara teknolojia ya Metaverse Afrika

Dar es Salaam. Tanzania imejipanga kuwa kitovu cha teknolojia mpya ya intaneti iliyoibuka duniani ya Metaverse inayotokana na intaneti ya vitu iitwayo (IOT).

Intaneti ya Metaverse inaunganisha dunia halisi na dunia isiyo halisi (virtual) ambayo kwa ujumla inatumika maeneo muhimu, ikiwemo elimu, afya, takwimu, viwanda na uchumi.

Kwa tafsiri, Metaverse inatengeneza uhalisia wa kitu kama kilivyo, lakini kwa njia ya kidijitali hivyo kuondoka gharama mbalimbali, ikiwemo usafiri na vifaa husika.

Akizungumza leo Jumatatu, Agosti 5, 2024 baada ya kupokea ugeni wa Rais wa Chuo cha Turku cha Finland, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama, Dk Nkundwe Mwasaga amesema fursa katika teknolojia hiyo zipo nyingi, hivyo Tanzania inakwenda kujenga umahiri katika eneo hilo.

“Intaneti tunayoitumia sasa inatumika kubadilshana taarifa katika namna ya kurasa, picha, video na imetupatia mafanikio makubwa.

“Sasa hivi teknolojia imekua na ipo hii mpya ya Metaverse ambayo inatumika duniani, ikiwemo katika kuunda meli, kufundishia wanafunzi kwa uhalisia. Tumeona tutumie fursa tuwe kitovu kwa bara letu,” amesema Dk Mwasaga.

Amesema kwa sasa Afrika hakuna nchi inayosema ni mahiri katika teknolojia hiyo, hivyo ni fursa kwa Tanzania kuanza na kwa sasa mipango iliyopo ni kujenga maabara ya kisasa ya teknolojia hiyo.

“Serikali kupitia bajeti ya mwaka jana na mwaka huu tumepewa fedha ya kujua tunajenga maabara ya aina gani ya Metaverse. Kwa sasa tunafanya upembuzi yakinifu na wenzetu wa Turku watatupa ushauri ya namna gani ya kufanya,” amesema.

Amesema maabara za Metaverse inatakiwa iwe katika muundo wa namna ya shule, au sehemu kama Mlima Kilimanjaro, Mbuga kama Ruaha, Ngorongoro hivyo inategemea na wapi inahitajika.

Kwa upande wa elimu, amesema teknolojia hiyo itaondoa uhaba wa vifaa hususani vya maabara, kwani mwanafunzi atajifunza kwenye Metaverse kwa kuwa atatumia vifaa kama vilivyo lakini kwa kidijitali, kisha akishapata uelewa ndipo anakwenda kwenye uhalisia.

Ameongeza kuwa hayo yote yanafanywa kwa sababu ya vijana wapate jukwaa la kujiajiri kupitia kuanzisha kampuni changa bunifu (start-ups) waweze kupambana katika soko la dunia.

Amesema Tume ya Tehama ipo kwa ajili ya teknolojia ibuka, hivyo Metaverse itaingizwa katika Wizara ya Elimu ili iwe faida kwa nchi.

Aidha, Serikali inataka hadi mwaka 2030 iwe kitovu cha uchumi wa digitali Afrika, ikiwa ni njia ya kuelekea katika dira ya mwaka 2050.

Katika kuhakikisha hilo, ndio maana Serikali inafanya jitihada kuchukua teknolojia ibuka zitakazofanya suala hilo kutimia.

Katika upande mwingine, Serikali ina mpango wa kujenga chuo cha kidijitali cha (DTI) Nala, jijini Dodoma ambacho kitatumia mikono zaidi ya nadharia kama anavyosema Mshauri Mwandamizi wa dijitali, Dk George Mulamula.

Amesema, DTI itafundisha kwa kutumia mitaala ya Metaverse, ili kuwafanya wanafunzi kuwa wabunifu. Amesema Ushirikiano na Chuo cha Turku ni mwanzo wa mwelekeo mpya katika gurudumu la kidijitiali.

DTI itajikita kutoa mafunzo ya Akili Mnemba (AI), IOT, usalama wa kimtandao na zote zinatumika kitengeneza Metaverse.

Faida zake amesema ni kutengeneza ajira, kutatua changamoto za kibiashara, jamii na serikalini ili kuendelea kiuchumi.

Kwa upande wake, Rais wa Chuo cha Turku, Profesa Vesa Taatila amesema teknolojia ya Metaverse ni muhimu zaidi katika dunia ya sasa, akitolea mfano katika elimu ya mafunzo.

Amesema teknolojia inatumika katika elimu, viwanda, afya na hata mafunzo ya kiusalama. Pia inaongeza thamani ya nchi.

Akithibitisha hilo amesema nchini kwao wanatengeneza dawa kupitia teknolojia hiyo, “Metaverse ni uti wa mgongo wa mapinduzi yajayo ya kiviwanda,” amesema Profesa Taatila.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading