Tanzania yajipanga kuwa kinara teknolojia ya Metaverse Afrika

Tanzania yajipanga kuwa kinara teknolojia ya Metaverse Afrika

Dar es Salaam. Tanzania imejipanga kuwa kitovu cha teknolojia mpya ya intaneti iliyoibuka duniani ya Metaverse inayotokana na intaneti ya vitu iitwayo (IOT).

Intaneti ya Metaverse inaunganisha dunia halisi na dunia isiyo halisi (virtual) ambayo kwa ujumla inatumika maeneo muhimu, ikiwemo elimu, afya, takwimu, viwanda na uchumi.

Kwa tafsiri, Metaverse inatengeneza uhalisia wa kitu kama kilivyo, lakini kwa njia ya kidijitali hivyo kuondoka gharama mbalimbali, ikiwemo usafiri na vifaa husika.

Akizungumza leo Jumatatu, Agosti 5, 2024 baada ya kupokea ugeni wa Rais wa Chuo cha Turku cha Finland, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama, Dk Nkundwe Mwasaga amesema fursa katika teknolojia hiyo zipo nyingi, hivyo Tanzania inakwenda kujenga umahiri katika eneo hilo.

“Intaneti tunayoitumia sasa inatumika kubadilshana taarifa katika namna ya kurasa, picha, video na imetupatia mafanikio makubwa.

“Sasa hivi teknolojia imekua na ipo hii mpya ya Metaverse ambayo inatumika duniani, ikiwemo katika kuunda meli, kufundishia wanafunzi kwa uhalisia. Tumeona tutumie fursa tuwe kitovu kwa bara letu,” amesema Dk Mwasaga.

Amesema kwa sasa Afrika hakuna nchi inayosema ni mahiri katika teknolojia hiyo, hivyo ni fursa kwa Tanzania kuanza na kwa sasa mipango iliyopo ni kujenga maabara ya kisasa ya teknolojia hiyo.

“Serikali kupitia bajeti ya mwaka jana na mwaka huu tumepewa fedha ya kujua tunajenga maabara ya aina gani ya Metaverse. Kwa sasa tunafanya upembuzi yakinifu na wenzetu wa Turku watatupa ushauri ya namna gani ya kufanya,” amesema.

Amesema maabara za Metaverse inatakiwa iwe katika muundo wa namna ya shule, au sehemu kama Mlima Kilimanjaro, Mbuga kama Ruaha, Ngorongoro hivyo inategemea na wapi inahitajika.

Kwa upande wa elimu, amesema teknolojia hiyo itaondoa uhaba wa vifaa hususani vya maabara, kwani mwanafunzi atajifunza kwenye Metaverse kwa kuwa atatumia vifaa kama vilivyo lakini kwa kidijitali, kisha akishapata uelewa ndipo anakwenda kwenye uhalisia.

Ameongeza kuwa hayo yote yanafanywa kwa sababu ya vijana wapate jukwaa la kujiajiri kupitia kuanzisha kampuni changa bunifu (start-ups) waweze kupambana katika soko la dunia.

Amesema Tume ya Tehama ipo kwa ajili ya teknolojia ibuka, hivyo Metaverse itaingizwa katika Wizara ya Elimu ili iwe faida kwa nchi.

Aidha, Serikali inataka hadi mwaka 2030 iwe kitovu cha uchumi wa digitali Afrika, ikiwa ni njia ya kuelekea katika dira ya mwaka 2050.

Katika kuhakikisha hilo, ndio maana Serikali inafanya jitihada kuchukua teknolojia ibuka zitakazofanya suala hilo kutimia.

Katika upande mwingine, Serikali ina mpango wa kujenga chuo cha kidijitali cha (DTI) Nala, jijini Dodoma ambacho kitatumia mikono zaidi ya nadharia kama anavyosema Mshauri Mwandamizi wa dijitali, Dk George Mulamula.

Amesema, DTI itafundisha kwa kutumia mitaala ya Metaverse, ili kuwafanya wanafunzi kuwa wabunifu. Amesema Ushirikiano na Chuo cha Turku ni mwanzo wa mwelekeo mpya katika gurudumu la kidijitiali.

DTI itajikita kutoa mafunzo ya Akili Mnemba (AI), IOT, usalama wa kimtandao na zote zinatumika kitengeneza Metaverse.

Faida zake amesema ni kutengeneza ajira, kutatua changamoto za kibiashara, jamii na serikalini ili kuendelea kiuchumi.

Kwa upande wake, Rais wa Chuo cha Turku, Profesa Vesa Taatila amesema teknolojia ya Metaverse ni muhimu zaidi katika dunia ya sasa, akitolea mfano katika elimu ya mafunzo.

Amesema teknolojia inatumika katika elimu, viwanda, afya na hata mafunzo ya kiusalama. Pia inaongeza thamani ya nchi.

Akithibitisha hilo amesema nchini kwao wanatengeneza dawa kupitia teknolojia hiyo, “Metaverse ni uti wa mgongo wa mapinduzi yajayo ya kiviwanda,” amesema Profesa Taatila.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading