Tanzania yaendeleza mikakati kufikia usawa wa kijinsia

Tanzania yaendeleza mikakati kufikia usawa wa kijinsia

Dar es Salaam. Ili kufikia usawa wa kijinsia nchini kupitia Programu ya Jukwaa la Kizazi chenye Usawa (GEF), Tanzania imejizatiti kutekeleza uwiano sawa kati ya wanaume na wanawake.

Kamati ya Kitaifa ya Ushauri (GEF) ilianzishwa na Rais Samia Suluhu Hassan Desemba 2021 kwa ajili kufuatilia na kushauri kuhusu maendeleo ya utekelezaji wa jukwaa hilo.

Akizungumza leo Jumatano Septemba 18, 2024 jijini Dar es Salaam kwenye mkutano wa ulioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la uwezeshaji wanawake (UN Women), mshauri wa Rais na Mwenyekiti wa GEF, Angellah Kairuki amesema Tanzania inatekeleza mpango wa malezi na makuzi kwa kuhakikisha baba na mama wanafanya biashara ili kutokwamishwa suala la malezi.

“Ili kuhakikisha hayo yanatekeleza ndio maana tunahusisha sekta binafsi na asasi nyingine za kiraia. Tunataka tuone katika ngazi za uongozi kuwe na wanawake na wanaume akitolea mfano bodi za wakurugenzi,” amesema Kairuki.

Amesema waliandaa mpango kazi huo wa miaka sita na Serikali itahakikisha kila hatua inashirikisha sekta binafsi.

“Wanavyotoa fursa za ajira kwa wanawake, uongozi, umiliki wa wanawake kwenye hisa na tunaamini tutaendelea kupiga hatua zaidi kimataifa huku ikiwa ni faida kwa uchumi wa nchi,” amesema Kairuki.

“Tanzania imeahidi kuinua programu za kitaifa katika sekta mbalimbali za malezi ya watoto na kuanzisha vituo vya kulelea watoto katika ngazi ya kijiji, sehemu za kazi na sokoni,” amesema.

Katika programu hiyo, Tanzania imetekeleza ahadi nne kwa kuteua vituo vya GEF katika mikoa yote 26 ya Tanzania bara, mikoa mitano ya Zanzibar na ndani ya mamlaka za Serikali za mitaa nchi nzima.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa UN Women, Dk Mitra Sadananda amesema ahadi ya Tanzania ya kuendeleza usawa wa kijinsia imewezesha wanawake kiuchumi.

“Lengo letu ni kukuza sekta ya binafsi inayowajibika kwa kuhakikisha upatikanaji sawa wa wanawake, ushiriki, sauti, wakala na usalama katika sera na desturi zote mahali pa kazi, sokoni na jamii,”amesema  Dk Sadananda.

Aidha, Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Suzanne Ndomba-Doran, amesema wanataka kutengeneza usawa wa kijinsia katika maeneo ya kazi.

“Chama chetu kina programu maalumu inayotoa mafunzo kwa wanawake waliopo sekta binafsi na hadi sasa wamehudhuria takribani 497.

“Tunafundisha uongozi, mawasiliano, kuingia katika vikao vya bodi lengo ili wapate nafasi mbalimbali za uongozi katika sehemu zao za kazi,” amesema Ndomba-Doran.

Mkurugenzi Mkuu Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Raphael Maganga amesema wanahakikisha usawa wa kijinsia ni suala linalopewa kipaumbele katika taasisi za sekta binafsi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading

High Court rejects Transworld’s application
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

High Court rejects Transworld’s application

The High Court in Dar es Salaam has struck out an application in which Transworld Aviation, a ground handler at the Abeid Aman Karume International Airport (AAKIA) was seeking permission to sue the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA).Continue Reading