Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amewasihi Wakristo na Watanzania kutoa heshima ya pekee kwa watoto kwa kuwa ni zawadi kubwa kutoka kwa Mungu.
Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amewasihi Wakristo na Watanzania kutoa heshima ya pekee kwa watoto kwa kuwa ni zawadi kubwa kutoka kwa Mungu.
Dk Mpango amesema sasa hivi katika nchi yanasikika mambo ya hovyo na dhuluma dhidi ya watoto ikiwemo watoto kunyanyaswa, kuuwawa na kulawitiwa.
“Tumuombe Mungu msamaha na atujalie neema ya kutambua jinsi yeye alivyowapenda watoto na sisi tufanye mengi ya kuwatunza hawa watoto na kumrudishia Mungu wakiwa weupe kama tunavyoweka ishara ya kitambaa cheupe kumrudishia Mungu,’amesema Makamu huyo wa Rais.
Katika hatua nyingine, Dk Mpango amewataka waamini hao kumshangilia Mungu kwa mvua aliyoileta na kueleza kuwa sehemu nyingine kumekuwa na hali ngumu ya ukame iliyosababisha mifugo kuanza kufa.
“Sasa Mwenyezi Mungu ametuletea neema ya mvua tuitumie vizuri, tulime mazao yetu sasa, tupande ili tuweze kupata chakula.
“Vilevile kila familia tutumie nafasi kupanda miti, tupande miti ya matunda, tupande miti ya kivuli, kila familia walau miti mitatu, miti miwili ya matunda na mmoja kwa ajili ya kivuli kwani nchi yetu imeharibika sana,”amesema.
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
Zanzibar terminates land lease offered to British developer
The Revolutionary Government of Zanzibar (SMZ) has terminated a land lease held by British property developer Pennyroyal Limited in Matemwe, the developer has announced.Continue Reading
Ali Hassan Mwinyi, Former President of Tanzania, Dies at 98
Ali Hassan Mwinyi, a schoolteacher turned politician who led Tanzania as its second post-independence president and helped dismantle the doctrinaire socialism of his predecessor, Julius K. Nyerere, died on Thursday in Dar es Salaam, the country’s former capital. He was 98.Continue Reading
Mwinyi lashes out at Zanzibar Airport, Port inefficiency claims
Zanzibar President Hussein Mwinyi has lashed out at the Opposition ACT Wazalendo, saying that the claims it raised about inefficiency in three areas within his Government were only meant to mislead the publicContinue Reading