Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amewasihi Wakristo na Watanzania kutoa heshima ya pekee kwa watoto kwa kuwa ni zawadi kubwa kutoka kwa Mungu.
Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amewasihi Wakristo na Watanzania kutoa heshima ya pekee kwa watoto kwa kuwa ni zawadi kubwa kutoka kwa Mungu.
Dk Mpango amesema sasa hivi katika nchi yanasikika mambo ya hovyo na dhuluma dhidi ya watoto ikiwemo watoto kunyanyaswa, kuuwawa na kulawitiwa.
“Tumuombe Mungu msamaha na atujalie neema ya kutambua jinsi yeye alivyowapenda watoto na sisi tufanye mengi ya kuwatunza hawa watoto na kumrudishia Mungu wakiwa weupe kama tunavyoweka ishara ya kitambaa cheupe kumrudishia Mungu,’amesema Makamu huyo wa Rais.
Katika hatua nyingine, Dk Mpango amewataka waamini hao kumshangilia Mungu kwa mvua aliyoileta na kueleza kuwa sehemu nyingine kumekuwa na hali ngumu ya ukame iliyosababisha mifugo kuanza kufa.
“Sasa Mwenyezi Mungu ametuletea neema ya mvua tuitumie vizuri, tulime mazao yetu sasa, tupande ili tuweze kupata chakula.
“Vilevile kila familia tutumie nafasi kupanda miti, tupande miti ya matunda, tupande miti ya kivuli, kila familia walau miti mitatu, miti miwili ya matunda na mmoja kwa ajili ya kivuli kwani nchi yetu imeharibika sana,”amesema.
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
Fast Satellite Internet in Kenya by June
Elon Musk’s satellite Internet firm Starlink announced it will launch in Kenya in the second quarter of this year.Continue Reading
Rare megamouth shark found in Zanzibar for the first time – why so little is known about it
The recent sighting was only the sixth time a megamouth had ever been found off the coast of Africa.Continue Reading
Tanzania can benefit from strategic investment in national pride
Travelling to a few places so far, I discovered that the Tanzanian passport can change the way one is treated at airports and international bordersContinue Reading