Tanzania, Marekani kupambana kichaa cha mbwa, watoto watajwa kuwa hatarini

Tanzania, Marekani kupambana kichaa cha mbwa, watoto watajwa kuwa hatarini

Tanzania, Marekani kupambana kichaa cha mbwa, watoto watajwa kuwa hatarini

Mwanza. Wakati ugonjwa wa kichaa cha mbwa ukitajwa kusababisha vifo vya zaidi ya watu 59,000 duniani kila mwaka, Serikali ya Tanzania na Marekani zimeamua kuungana ili kupambana nao ikiwemo kuelimisha umma juu ya ugonjwa huo.

Hatua hiyo inakuja ikiwa kichaa cha mbwa bado ni tishio kubwa la afya ya umma nchini Tanzania hasa katika jamii zenye uelewa mdogo na upatikanaji hafifu wa huduma za mifugo.

Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), kupitia Mradi wa Breakthrough Action kwa kushirikiana Ofisi ya Waziri Mkuu sehemu ya Afya Moja, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Afya, na Ofisi ya Rais (Tamisemi), wametumia fursa ya maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kupambana na ugonjwa huo.

Kupitia kampeni ya kitaifa ya “Holela-Holela Itakukosti,” yenye lengo la kuiwezesha jamii kupambana na ugonjwa huo, Usaid na Serikali ya Tanzania inawakumbusha wananchi kuwajibika na kuondoa vikwazo ili kushinda vita dhidi ya hatari ya ugonjwa huo.

Awali, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa, ambayo hufanyika kila mwaka Septemba, 28 kampeni ya “Holela-Holela Itakukosti,” ambayo tafsiri yake ni uzembe ni gharama, ilichukua nafasi kubwa katika kuongeza uelewa kuhusu kichaa cha mbwa, ugonjwa unaosababisha vifo vya zaidi ya watu 59,000 duniani kila mwaka.

Tukio hilo la kitaifa liliongozwa na Abdul Mhinte, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye amesisitiza umuhimu wa elimu kwa jamii na mikakati ya chanjo katika kupambana na ugonjwa.

Aidha amehimiza kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya maofisa wa afya ya umma na jamii za mitaa ili kuimarisha mwitikio wa pamoja.

“Kichaa cha mbwa kinaweza kuzuilika. Lengo letu ni kuhakikisha kila mbwa nchini Tanzania anapatiwa chanjo, na kila mwananchi anajua cha kufanya endapo atang’atwa na mbwa. Kila jamii inapaswa kuchukua jukumu lake katika vita hivi.”

Msisitizo wake juu ya elimu na ushirikiano ulipeleka ujumbe wa matumaini kwa waliohudhuria. Kampeni hiyo inalenga jamii kwa kutoa ujumbe muhimu kuhusu kichaa cha mbwa, kuwachanja na kutafuta huduma za afya mara baada ya tukio la kung’atwa na mbwa.

Watoto, ambao ni miongoni mwa walio hatarini zaidi kuathiriwa na kichaa cha mbwa, wanapewa elimu juu ya kuepuka mwingiliano kama kuwachokoza mbwa hasa wasiowafahamu na wanyama wenye uwezekano wa kuwa na maambukizi.

Shuhuda kadhaa zinaonensha umuhimu wa kampeni hii. Revina, mama wa watoto watatu kutoka Mwanza:”Kabla ya kampeni, sikuwa najua hatari ya kichaa cha mbwa. Tulipojifunza kuwa mbwa wetu wanapaswa kuchanjwa, tulichukua hatua mara moja. Sasa, nina amani kuwaacha watoto wangu kucheza nje.”

Kampeni ya Holela-Holela pia inalenga kupambana na sababu zote zinazochangia kuwepo kwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa kama vile uelewa mdogo, juhudi hafifu za chanjo, na usimamizi usio salama wa wanyama.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal

Ruling party Chama Cha Mapinduzi-Zanzibar has said it is ready to task state organs to investigate some of the claims against its government that have been raised by opposition politicians on the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA).Continue Reading

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading