Tanzania kusaka Sh261 bilioni kila mwaka nchini Uturuki

Tanzania kusaka Sh261 bilioni kila mwaka nchini Uturuki

Dar es Salaam. Tanzania imeweka lengo la kuvutia mitaji ya Sh261 bilioni kila mwaka kutoka kwa wawekezaji nchini Uturuki kupitia sekta kadhaa za uwekezaji, ikiwamo kilimo.

Ili kufikia malengo hayo, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimeingia mkataba wa makubaliano ya ushirikiano na Kampuni ya Africapital Investiment Holding Limited ambayo itafanya kazi ya kuvutia mitaji na kuiweka pamoja kwa ajili ya kufanya uwekezaji nchini.

Kampuni hiyo itakuwa ikitafuta wawekezaji kutoka maeneo ya Uturuki na nchi jirani kabla ya kuwaleta nchini.

Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa TIC, Gilead Teri alisema Uturuki ni nchi yenye mtaji mkubwa katika maeneo ambayo yanaendana na mahitaji ya Tanzania kama teknolojia rahisi katika kilimo.

“Vitu kama bidhaa za kielektroniki za majumbani, bidhaa za ujenzi, sekta ya dawa inayojumuisha hospitali na sekta ya utalii, wenzetu wamepiga hatua. Tungependa kujifunza kutoka kwao na kampuni zao zije kuwekeza nchini,” amesema Teri.

Amesema makubaliano yaliyoingiwa ni ya kimkakati kwa sababu kampuni hiyo inajua mitandao ya kiuwekezaji.

Amesema awali taasisi za Serikali kama TIC zilikuwa zikifanya makubaliano na taasisi za uwekezaji za nchi mbalimbali lakini kutokana na kufanya kazi zinazofanana ilikuwa ngumu kufikia malengo.

“Hali hiyo ilikuwa ikifanya kushindwa kufikia lengo kwa sababu wote mnaenda kutafuta wawekezaji walewale wachache ambao wapo duniani, sasa tuliamua kushirikiana na kampuni binafsi ambazo zina fursa za kuleta wawekezaji,” amesema Teri.

Amesema ushirikiano wa kwanza kufanyika ulikuwa kati ya TIC na kampuni ya Sheria nchini China ambayo ina wafanyakazi zaidi ya 5,000 na wateja zaidi ya 50,000 na kati yake kuna kampuni ambazo zinataka kuwekeza nje ya China.

Amesema kushirikiana nao kunaweka urahisi wa wawekezaji kutoka eneo hilo kujua sheria na taratibu za uwekezaji nchini na inaweka urahisi kwao kuwashauri wawekezaji.

“Kuanzia hapo tulianza kuangalia baadhi ya nchi za kimkakati ambazo tunaweza kushirikiana nazo, pia kampuni ambazo zina mitandao mipana ili ziweze kuvutia uwekezaji nchini,” amesema Teri.

Mkurugenzi Mtendaji wa Africapital Investiment Holding Limited, Burak Kuyuksarac amesema ni makubaliano ya kwanza kufanywa na taasisi ya Serikali nchini.

Amesema mkakati ni kwenda kusaini mkataba kama huo na Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (Zipa).

“Mbali na kuangalia wawezekaji pia tutaangalia namna ya kuwezesha mawazo bunifu (startups), huku baadhi ya watu wanavutiwa zaidi katika teknolojia za kifedha, kilimo na hata wanaofanya biashara kwa njia ya mtandao,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income

Insurer and financial services provider Britam posted a 22.5 percent jump in net earnings for the half-year ended June 2024, to Sh2 billion, buoyed by increased investment income.

The rise in half-year net profit from Sh1.64 billion posted in a similar period last year came on the back of net investment income rising 2.5 times to Sh13.27 billion from Sh5.3 billion.

“We are confident in the growth and performance trend that Britam has achieved, supported by its subsidiaries in Kenya and the region. Our business is expanding its revenue base while effectively managing costs,” Britam Chief Executive Officer Tom Gitogo said.

“Our customer-centric approach is fueling growth in our customer base and product uptake, particularly through micro-insurance, partnerships, and digital channels.”

The investment income growth was fueled by interest and dividend income rising 34 percent to Sh9.1 billion, which the insurer attributed to growth in revenue and the gains from the realignment of the group’s investment portfolio.

Britam also booked a Sh3.79 billion gain on financial assets at a fair value, compared with a Sh1.8 billion loss posted in a similar period last year.

The increased investment income helped offset the 12.7 percent decline in net insurance service result to Sh2.13 billion in the wake of claims paid out rising at a faster pace than that of premiums received.

Britam said insurance revenue, which is money from written premiums, increased to Sh17.8 billion from Sh16.6 billion, primarily driven by growth in the Kenya insurance business and regional general insurance businesses, which contributed 30 percent of the revenue.

The group has a presence in seven countries in Africa namely Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, South Sudan, Mozambique, and Malawi.

Britam’s insurance service expense hit Sh13.6 billion from Sh11.3 billion, while net insurance finance expenses rose 2.6 times to Sh12.3 billion during the same period.

“Net insurance finance expenses increased mainly due to growth in interest cost for the deposit administration business driven by better investment performance. This has also been impacted by a decline in the yield curve, which has led to an increase in the insurance contract liabilities. The increase has been offset by a matching increase in fair value gain on assets,” said Britam.

Britam’s growth in profit is in line with that of other Nairobi Securities Exchange-listed insurers, which have seen a rise in profits.

Jubilee Holdings net profit in the six months increased by 22.7 percent to Sh2.5 billion on increased income from insurance, helping the insurer maintain Sh2 per share interim dividend.

CIC Insurance Group posted a 0.64 percent rise in net profit to Sh709.99 million in the same period as net earnings of Liberty Kenya nearly tripled to Sh632 million from Sh213 million, while Sanlam Kenya emerged from a loss to post a Sh282.2 million net profit.

Continue Reading