Tanzania kupata Sh33 bilioni za mabadiliko tabianchi

Tanzania kupata Sh33 bilioni za mabadiliko tabianchi

Tanzania kupata Sh33 bilioni za mabadiliko tabianchi

Dar es Salaam. Kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi zinazoikumba dunia, Tanzania inatarajia kupata msaada wa Sh33 bilioni ili kukabiliana na changamoto hiyo.

Fedha hizo zimelenga kusaidia ngazi ya jamii na Serikali za mitaa ikiwa ni moja ya mkakati wa utekelezaji wa mfuko huo wa mabadiliko ya tabianchi mwaka 2021-2026.

Moja ya maeneo yaliyotajwa katika mkakati huo ni kuhakikisha jamii zinahimili athari za mabadiliko hayo, ikiwamo ukame, mafuriko, kuongezeka kwa kina cha bahari na maji ya chumvi.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano, Mazingira), Kemila Mutesa wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia ya nchi (UNCDF) leo Jumanne Oktoba mosi, 2024 jijini Dar es Salaam.

“Leo tumezindua awamu ya pili ya mradi unaolenga kuleta matokeo chanya hasa katika athari za mabadiliko ya tabianchi katika jamii zilizoathirika zaidi, kulingana mkataba ya Umoja wa Mataifa na nchi zinazoendelea,” amesema Mutesa.

Mratibu wa UNCDF Aine Mushi amesema halmashauri tatu zilizonufaika na fedha hizo kwa mwaka 2023 ni  Chamwino katika Kijiji cha Chiboli, Kondoa (Kijiji cha Kisasendisa) na Mpwapwa (Kijiji cha Kisisi).

“Miradi tuliyoifanya katika kijiji hicho ni pamoja na kuchimba visima vya maji na kuhakikisha baadhi familia na wanyama wanaondokana na adha ya maji, bila kusahau kilimo,” amesema Mushi.

Pia, amesema awamu hiyo ya pili watapeleka huduma katika halmashauri na mikoa iliyopo karibu na Pwani.

“Tukiachana na faida hizo, tunaangalia athari wanazopata wanajamii waliyopo katika mikoa mbalimbali na kutoa misaada, tulianza na Dodoma kutokana na hali ya ukame wanayokabiliana nayo, hivyo ilitulazimu kuhakikisha wanapata visima kwa ajili ya maji, mifugo na kilimo,” ameeleza Mushi.

Amesema ili kuendelea kupambana na mabadiliko ya tabianchi wanapanua wigo kwa wadau wengine kuendelea kujitokeza mbali na wale waliokuwepo awamu ya kwanza ambao ni European Union (EU), Chuo cha Mipango na Chuo cha Serikali ya Mitaa.

Amesema, awamu ya pili ina ongezeko la wadau mbalimbali kama Obelgiji, Ubalozi wa Norway, Ubalozi Ireland na taasisi za utafiti kuhusu mabadiliko ya tabianchi huku mashirika yasio ya kiserikali yakishiriki katika mpango huo.

“Tumefanya vizuri awamu ya kwanza kwa kufikia wilaya tatu na sasa tunategemea kufanya vizuri zaidi katika awamu ya pili kwa kufikia wilaya zaidi ya tano na kufikisha jumla ya wilaya nane,” ameeleza.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading