Tanzania kunufaika uwekezaji teknolojia ya fedha

Tanzania kunufaika uwekezaji teknolojia ya fedha

Dar es Salaam. Tanzania inatarajiwa kuwa miongoni mwa mataifa yatakayonufaika na uwekezaji wa teknolijia ya fedha (FinTech), baada ya wawekezaji 10 kutoka Afrika na Marekani kutua nchini.

Wawekezaji hao wanatarajiwa kutua kwenye kongamano la wadau wa sekta hiyo lililopangwa kufanyika hapa nchini kati ya Septemba 12 hadi 13, 2024 ambapo kwa jumla wadau zaidi ya 300 watakutana.

Kongamano hilo limelenga kuleta chachu na kuongeza wawekezaji, hasa katika teknolojia ya fedha hapa nchini na Afrika kiujumla kama anavyosema Makamu Mwenyekiti wa Tanzania Fintech Association (Tafina), Reuben Mwatosya alipokuwa na mkutano na waandishi wa habari jana Septemba 4, 2024 jijini Dar es Salaam.

“Kongamano hili litakwenda kuibua majadiliano baina ya wawekezaji na wawakilishi wa nchi mbalimbali zitakazohudhuria siku hiyo, ikiwa na lengo la mapinduzi ya kiteknolojia za pande zote,” amesema Mwantosya.

Aidha, kongamano hilo linatarajiwa kuwa mwanzo wa makongamano mengine na kujenga fursa kuwaleta wadau kutoka sekta mbalimbali kujadiliana na kuongea masuala ya kiteknolojia na namna gani waikuze kuendana na dunia ya sasa.

Katibu Mkuu wa Tafina, Shadrack Kamenya amesema katika kongamano hilo kutakuwa na midahalo iliyogawanyika katika aina tatu ambazo ni kiuwekezaji, kisera na ushirikiano baina ya watoa huduma.

“Kutakuwa na maonyesho ya teknolojia na namna wanavyozitoa huduma zao na pia ni eneo mahususi kwa serekali na wadau wengine kuona ni kitu gani kinafanyika duniani na kurahisisha maendeleo hasa katika sekta ya fedha hapa nchini,” amesema.

Miongoni mwa maazimio ya siku hiyo amesema ni kurahisisha mchakato wa ujumuishaji wa kifedha na urejeshaji fedha ambayo yote msingi wake ni uwezeshajiwa teknolojia ya Fintech.

Amesema kongamano hilo pia limelenga kuwakutanisha wasomi kutoka mataifa mbalimbali watakaobadilishana uzoefu kwaajili ya huduma endelevu za kifedha.

Teknolojia ya kifedha (FinTech) inashika nafasi za juu zaidi duniani katika zile teknolojia zinazokuwa kwa kasi na kuwa na matumizi mengi zaidi duniani, huku ikitanguliwa na taknolojia ya kimtandao.

Teknolojia nyingine zinazotarajiwa ni zile za matumizi ya akili bandia (AI).

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Popular
Swahili News Editor

MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.Continue Reading