Tanzania: Fedha za kukabiliana mabadiliko ya tabianchi ziwafikie wazawa

Tanzania: Fedha za kukabiliana mabadiliko ya tabianchi ziwafikie wazawa

Tanzania: Fedha za kukabiliana mabadiliko ya tabianchi ziwafikie wazawa

Dar es Salaam. Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Philip Mpango amesema ni muhimu kuhakikisha fedha za ufadhili wa miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi zinawafikia wazawa ili waweze kubuni miradi ya kukabiliana na hali hiyo kwa kuwa wanafahamu zaidi changamoto za maeneo yao.

Dk Mpango anayasema haya akisisitiza uwajibikaji wa nchi zilizoendelea kutoa fedha kwa nchi zinazoendelea ili kukabiliana na athari za mabadiliko hayo.

Hata hivyo, fedha za ufadhili zilizotolewa ahadi ya kila mwaka kutoka nchi zilizoendelea zikiwa ni Dola 100 bilioni ambazo ni zaidi ya Sh250 trilioni ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Ameyasema hayo wakati alipomwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika kukabidhi tuzo kwa kwa washindi wa miradi ya ubunifu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi inayotekelezwa na jamii za asili (wazawa) kutoka sehemu mbalimbali duniani katika shindano linaloratibiwa na Taasisi ya Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi Duniani (GCA).

Hafla hiyo imefanyika pembezoni mwa Mkutano wa 29 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP-29) unaofanyika katika Mji wa Baku nchini Azerbaijan.

“Tanzania inaendelea na uwekezaji ili kuongeza upatikanaji wa nishati mbadala kama vile jotoardhi, nishati ya jua na upepo huku ikiendelea kukabiliana na nishati chafu ya kupikia ambayo imekua chanzo cha ukataji miti na upotevu wa hifadhi ya kaboni inayopelekea uharibifu wa rasilimali za kijani,” amesema.

Dk Mpango amesisitiza umuhimu wa viongozi kuwatambua na kuwawezesha wabunifu wa miradi inayotekelezwa na wanajamii wa asili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Aidha ametoa wito kwa jamii kuendelea kuanzisha miradi ya ubunifu itayosaidia katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Halikadhalika, Makamu wa Rais ametoa wito kwa Taasisi ya GCA kuongeza wigo wa mashindano hayo ili kuwafikia wabunifu wengi zaidi ikiwemo wanaofanya shughuli zinazohusiana na uchumi wa buluu.

Amesema Tanzania ina mifano ya miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kutoka kwa wananchi wazawa ambapo wanawake katika ukanda wa bahari Zanzibar wanajishughulisha na kilimo cha mwani ambacho ni matokeo ya kuongezeka kwa kina cha bahari kunakosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Tanzania ambayo ni miongoni mwa washiriki imeazimia kuwa na mikakati ya pamoja na nchi wanachama ikiwa ni hatua za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayoshuhudiwa maeneo mbalimbali duniani.

Mshauri wa nishati mpito Afrika kutoka Shirika la Kufuatilia Usimamizi wa Rasilimali za Asili (NRGI), Silas Olang’ anasema dhana ya fedha kuwafikia wazawa ni nzuri amesema jambo la msingi ila inahitaji uratibu wa kuwafikia walengwa halisi.

“Uratibu wa Serikali kwa kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha azma hiyo inafikiwa. Amesema kuliko fedha hizo kupitia mikono mingine ni jambo jema kama zitafika moja kwa moja kwa wahusika,” amesema Olang’.

Aidha amesema katika kuhakikisha fedha za wafadhili zinatolewa kwa wakati amesema inahitajika sauti na nguvu ya pamoja ambayo itaeleta ushawishi kwa wafadhili kutimiza ahadi zao.

“Nchi zinazoendelea zinapaswa kuwa na sauti ya pamoja kuweza kuwafanya walioendelea wanatimiza ahadi zao ingawa kuna mashaka kama watatimiza kwa asilimia miamoja,” amesema. 

Mdau na Mwanaharakati wa Mazingira, Clay Mwaifwani amesema ni suluhisho ijapokuwa mabadiliko ya tabianchi kuwa na athari za muda mrefu hivyo suala la kupewa fedha linapaswa kuendana na kujengewa wazawa uwezo wa shughuli wanazozifanya kulingana na mabadiliko hayo.

Amesema fedha zitolewe ingawa zinasuasua kutoka kwa wafadhili ila amesema ijengwe utaratibu kwa wazawa namna ya kukabiliana na athari hizi ikiwemo wakulima.

“Wakijengewa uwezo wa kupambana itakuwa jambo la msingi zaidi kwani fedha huisha. Ila uwezo utafanya kilimo kiwe himilivu,” amesema.

Kuhusu suala la bunifu amesema ni wazo zuri kwani nchi za zinazoendelea zina uwezo mdogo wa kukabiliana na mabadiliko hayo hivyo suala la bunifu linapaswa kushikiliwa kwa namna ya kuwa na watu wengi.

Amesema ubunifu unahahakishwa unawanufaisha watu wengi na kuwafikia watu wengi kila siku kuweza kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading