TAEC ilivyookoa maisha ya watu dhidi ya mionzi

TAEC ilivyookoa maisha ya watu dhidi ya mionzi

Dar es Salaam. Tume ya Nguvu za Atomic Tanzania (TAEC) imezuia matukio 17 yaliyohusiana na mionzi ambayo yalikuwa na uwezekano wa kuleta madhara makubwa kwa jamii, endapo wasingeingilia kati.

Matukio ambayo wameyazuia ni utumikaji wa urani kwenye mazao kwa ajili ya kuua wadudu na uingizwaji wa kifaa kizito cha mionzi ambacho hakijatajwa, kilichokuwa kinatafutiwa mteja.

Hayo yameelezwa leo Aprili 29, 2024 na Mkurugenzi Mtendaji wa TAEC, Profesa Lazaro Busagala kwenye mkutano wa wahariri na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam.

“Ilitokea mwananchi fulani akapata urani kutoka mahali fulani akaanza kuuza kwa wakulima ili waweke kwenye mazao ya nafaka kwa lengo la kuzuia uharibifu wa mazao, ikawa ni biashara inayoendelea kwa hiyo kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama tulizima hili, ina maana watu wangekula mionzi na kupata madhara makubwa,” amesema.

Akielezea kisa kingine Profesa Busagala amesema: “Ilitokea mtu fulani akakamatwa na kifaa kizito kinachotoa mionzi, halafu akitafuta wateja awauzie. Akalala na kifaa hicho, baada ya siku chache kama wiki mbili vyombo vya usalama na ulinzi wakakikamata kwa kushirikiana na sisi. Yule mtu akafariki baada ya wiki mbili, ina maana angewauzia watu wengine, kingeendelea kuketa madhara.”

Amasema, “tumepewa dhamana ya kuwakinga wananchi na madhara ya mionzi, hivyo tunafanya jitihada kubwa kwa kushirikiana na vyombo vya usalama kuhakikisha hakuna madhara yanayotokana na mionzi kwa jamii.”

Amesema katika kudhibiti matumizi salama ya mionzi TAEC imefanikiwa kuongeza idadi ya wanaopewa leseni za kutoa huduma za mionzi kwa asilimia 102, yaani kutoka leseni 297 kwa 2016/17 hadi wastani wa 767 kwa mwaka 2022/23.

“Tumesajili wataalamu wa mionzi 1,289 wa kutoa huduma ya mionzi kwa wagonjwa, kutengeneza, kukarabati na kuendesha vifaa vya nyuklia, jambo ambalo halikufanyika kipindi cha nyuma,” amesema Profesa Busagala.

Pia amesema wamekuwa na juhudi za kusimamia udhibiti wa matumizi salama ya mionzi ili kuepuka madhara yake.

Amesema mwaka 2022/23 jumla kaguzi 971 zilifanyika ukilinganisha na kaguzi 244 kwa mwaka 2016/17 ikiwa ni ongezeko la asilimia 298, ambazo ni kaguzi nyingi kuliko kiwango cha kimataifa.

Amesema wataendelea kuboresha udhibiti wa matumizi salama ya mionzi na miundombinu ya teknolojia ya nyuklia, kuweka na kuboresha kanuni na sheria ili kuwaweka Watanzania salama zaidi dhidi ya madhara ya mionzi na teknolojia ya nyuklia.

Vilevile, tume hiyo imedhamiria kuongeza usalama kwenye kilimo kama vile uboreshaji wa mbegu kwa kutumia teknolojia ya atomu.

Kuhusu matumizi ya nyuklia katika uzalishaji wa umeme, Profesa Busagala amesema endapo kutakuwa na umuhimu wa kuitumia kwenye nishati hiyo, maamuzi yanaweza kufanyika na wakaingiza kwenye mradi.

Katika kupata fursa zaidi za sayansi na teknolojia ya nyuklia na kuwalinda wananchi na mazingira dhidi ya madhara ya mionzi, Serikali imeongeza bajeti ya utafiti kwa TAEC hadi kufikia Sh450 milioni katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Kuhusu matumizi ya microwave, amesema wataalamu wanasema aina yoyote ya kupika chakula iwe ni kuchemsha kwa kawaida au kuoka inaathiri virutubisho vya chakula na aina ya upikaji huo inaweza kuathiri sana au kidogo na inategemeana ni chakula gani unakipika.

Akitoa mfano wa mboga za majani almesema zina vitamini C nyingi zaidi na inayeyuka kirahisi kwenye maji, kwa hiyo kitaalamu inatakiwa kukaangwa, ikichemshwa Vitamini C inapotea.

“Kwa hiyo matumizi ya ‘microwave’ inatumia mionzi sambayo ina tabia ya kutoa joto, kwa hiyo inapotoa joto ni sawasawa na maji yangetoa joto, kwa hiyo itaharibu virutubisho kwa namna yoyote,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading