Taarifa ya awali ripoti ya ajali ya ndege Ziwa Victoria: ‘Vikosi vya uokoaji vingefika haraka, watu wengi wangetoka hai’’
Taarifa ya awali ya ripoti ya ajali ya ndege ya shirika la precision iliyotokea katika eneo la Ziwa Victoria Tanzania, imetolewa na wizara ya usafirishaji nchini Tanzania, na kuonesha kuwa vikosi vya uokoaji vilichelewa kufika katika eneo la tukio.
Ajali hiyo ilitokea majira ya saa 2 asubuhi saa za Tanzania, lakini kwa mujibu wa ripoti hiyo inaeleza kuwa boti ya kitengo cha polisi wa majini, ilifika majira ya saa saba saa za Tanzania.
‘’ Boti ilifika saa saba eneo la tukio, baada ya kufika walikua na changamoto ya kuishiwa mafuta na oksijeni, kabla hawajafika, mvuvi mmoja tayari alianza kutoka maiti zilokua ndani ya ndege’’ taarifa ya ripoti inasema
Taarifa ya ripoti hiyo pia haijatoa sababu kamili ya nini kilisababisha kutokea kwa ajali, ikisema kuwa uchunguzi bado unaendelea.
Mamlaka ya usafiri wa anga Tanzania awali ilibainisha kuwa baada ya ripoti ya awali itafuatia ripoti ya uchunguzi wa awali inayotarajiwa kuchapishwa mwezi mmoja baada ya ajali na kisha ripoti kamili baada ya mwaka mmoja.
Ndege hiyo ya shirika la precision ATR 42-500 yenye namba PW 494 ilianguka kwenye ziwa Victoria mita chache kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba, ikijiandaa kutua ikitokea jijini Dar es Salaam kupitia Mwanza. Ajali hiyo imeua watu 19 kati ya 43 waliokuwemo akiwemo rubani na msaidizi wake.
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
How diplomatic intervention kept Air France, KLM in Zanzibar
It has, however, emerged, that the Netherland and France sought a diplomatic solution to a standoff at the Abeid Aman Karume International Airport, warning that it could disrupt Air France and KLM flights into Zanzibar, and later Dar es Salaam.Continue Reading
Zanzibar, Tanzania: Inflation hits five-year high
With Covid-19 and the war in Ukraine being blamed after inflation in Tanzania and Zanzibar rose to 4.5 this year and is climbing – the highest rate since November 2017Continue Reading
Zanzibar Airports Authority enforces Dnata monopoly
. Airlines that have not joined the Zanzibar Airports Authority’s (ZAA) preferred ground handler, Dnata, at the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA) face eviction from the Terminal Three building Dnata is the sole ground handler authorised to provide services for flights that operate at Terminal 3.Continue Reading