Taarifa ya awali ripoti ya ajali ya ndege Ziwa Victoria: ‘Vikosi vya uokoaji vingefika haraka, watu wengi wangetoka hai’’
Taarifa ya awali ya ripoti ya ajali ya ndege ya shirika la precision iliyotokea katika eneo la Ziwa Victoria Tanzania, imetolewa na wizara ya usafirishaji nchini Tanzania, na kuonesha kuwa vikosi vya uokoaji vilichelewa kufika katika eneo la tukio.
Ajali hiyo ilitokea majira ya saa 2 asubuhi saa za Tanzania, lakini kwa mujibu wa ripoti hiyo inaeleza kuwa boti ya kitengo cha polisi wa majini, ilifika majira ya saa saba saa za Tanzania.
‘’ Boti ilifika saa saba eneo la tukio, baada ya kufika walikua na changamoto ya kuishiwa mafuta na oksijeni, kabla hawajafika, mvuvi mmoja tayari alianza kutoka maiti zilokua ndani ya ndege’’ taarifa ya ripoti inasema
Taarifa ya ripoti hiyo pia haijatoa sababu kamili ya nini kilisababisha kutokea kwa ajali, ikisema kuwa uchunguzi bado unaendelea.
Mamlaka ya usafiri wa anga Tanzania awali ilibainisha kuwa baada ya ripoti ya awali itafuatia ripoti ya uchunguzi wa awali inayotarajiwa kuchapishwa mwezi mmoja baada ya ajali na kisha ripoti kamili baada ya mwaka mmoja.
Ndege hiyo ya shirika la precision ATR 42-500 yenye namba PW 494 ilianguka kwenye ziwa Victoria mita chache kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba, ikijiandaa kutua ikitokea jijini Dar es Salaam kupitia Mwanza. Ajali hiyo imeua watu 19 kati ya 43 waliokuwemo akiwemo rubani na msaidizi wake.
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
Ground handling firms in Zanzibar start cutting jobs
ZAT and Transworld, companies providing ground handling services at Abeid Amani Karume International Airport, have to lay off workers to stay afloat.Continue Reading
Will Tanzania agree to Starlink Internet Service?
Will the Tanzania government let Starlink, the world-famous internet service provider, operate in the country?Continue Reading
Shock waves hit Zanzibar’s Real Estate industry
The revocation of British developer Pennyroyal’s leasehold for the construction of Blue Amber Resort by the Revolutionary Government of Zanzibar has sent shock waves in the nascent property market on the Isles.Continue Reading