Taarifa ya awali ripoti ya ajali ya ndege Ziwa Victoria: ‘Vikosi vya uokoaji vingefika haraka, watu wengi wangetoka hai’’
Taarifa ya awali ya ripoti ya ajali ya ndege ya shirika la precision iliyotokea katika eneo la Ziwa Victoria Tanzania, imetolewa na wizara ya usafirishaji nchini Tanzania, na kuonesha kuwa vikosi vya uokoaji vilichelewa kufika katika eneo la tukio.
Ajali hiyo ilitokea majira ya saa 2 asubuhi saa za Tanzania, lakini kwa mujibu wa ripoti hiyo inaeleza kuwa boti ya kitengo cha polisi wa majini, ilifika majira ya saa saba saa za Tanzania.
‘’ Boti ilifika saa saba eneo la tukio, baada ya kufika walikua na changamoto ya kuishiwa mafuta na oksijeni, kabla hawajafika, mvuvi mmoja tayari alianza kutoka maiti zilokua ndani ya ndege’’ taarifa ya ripoti inasema
Taarifa ya ripoti hiyo pia haijatoa sababu kamili ya nini kilisababisha kutokea kwa ajali, ikisema kuwa uchunguzi bado unaendelea.
Mamlaka ya usafiri wa anga Tanzania awali ilibainisha kuwa baada ya ripoti ya awali itafuatia ripoti ya uchunguzi wa awali inayotarajiwa kuchapishwa mwezi mmoja baada ya ajali na kisha ripoti kamili baada ya mwaka mmoja.
Ndege hiyo ya shirika la precision ATR 42-500 yenye namba PW 494 ilianguka kwenye ziwa Victoria mita chache kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba, ikijiandaa kutua ikitokea jijini Dar es Salaam kupitia Mwanza. Ajali hiyo imeua watu 19 kati ya 43 waliokuwemo akiwemo rubani na msaidizi wake.
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
Zanzibar land lease controversy with British Developer
Zanzibar investment lease controversy rumbles on after President Hussein Mwinyi claims the land lease was terminated following a court case which the developer lost Contradictory details come to light.Continue Reading
Zanzibar liquor importers face fresh hurdle despite court order
The liquor shortage in Zanzibar is far from over, even after a court order granted relief to the three importers.Continue Reading
Mbeto on Mwinyi: He created today’s affluent people
The CCM Secretary of Ideology and Publicity (Zanzibar), Mr Khamis Mbeto Khamis, said the late President Ali Hassan Mwinyi was the architect of the current class of affluent people.Continue Reading