Mbeya, Tanzania:
Serikali imeshauriwa kufanya mabadiliko ya jina la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe (SIA) uitwe jina la mkoa husika (Mbeya) ili kuondoa mkanganyo kwa wageni wanaoingia na kutoka mkoani humo kwa shughuli mbalimbali.
Ombi hilo limetolewa leo Jumatatu Januari 9, 2023 na Spika wa Bunge ambaye pia ni mbunge wa Mbeya Mjini, Dk Tulia Ackson aliposhiriki kikao cha bodi ya barabara mkoa kilichoongozwa na mkuu wa mkoa, Juma Homera.
“Uhalisia wa viwanja vya ndege duniani ni lazima utaitwa jina la mahali husika kijografia au jina la mtu, huwezi kutumia jina la Songwe ambalo ni mkoa mwingine kwenye eneo la mkoa wa Mbeya, jambo hili linawachanganya watu wengi, hivyo unahitaji mabadiliko,” amesema Dk Tulia.
Kwa upande wake, mbunge wa Lupa, Masanche Kasaka ameunga mkono hoja huku akisisitiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kuboresha miundombinu ya barabara.
Mfanyabishara wa duka la jumla jijini Mbeya, Atupakisye John amesema ni vyema Serikali kulipokea wazo hilo na kufanya mabadiliko ya jina la uwanja wa ndege wa Songwe na kuitwa uwanja wa mkoa husika.
“Hata sisi tunapowapokea wafanyabishara wenzetu kutoka mataifa mengine uwa wanahoji sababu za uwanja uliopo mkoa wa Mbeya kuitwa uwanja wa ndege wa Songwe, jambo ambalo linaleta kigugumizi,” amesema.
Source: mwananchi.co.tz
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
For years, a UK mining giant was untouchable in Zambia for pollution until a former miner’s son took them on
For years, the people in the villages around Chingola in Zambia endured frequent health challenges and dead fish floating around in their water source, but that was just the beginning of their nightmare.Continue Reading
Top US investor sells 600m Safaricom shares in dividend protest
An American multinational investment management firm is selling millions of shares held in Safaricom in protest over delays in dividend repatriation amid the fall of the telco’s valuation to below Sh600 billion.Continue Reading
ZSSF money not for projects, says Ali Karume
Unguja. Veteran politician and diplomat Ali Karume has called on authorities of the Zanzibar Revolutionary Government (SMZ) to refrain from using the Zanzibar Social Security Fund money for establishing commercial projects.Continue Reading