SMZ yaja na ‘ada ya nyongeza’ elimu ya juu

SMZ yaja na ‘ada ya nyongeza’ elimu ya juu

Unguja. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeanzisha mfumo wa malipo ya ada ya nyongeza (Top up tuition fees) ambayo itawasaidia wanafunzi kukamilisha gharama za masomo vyuoni kwa kufidia asilimia iliyopungua baada ya kupata mikopo.

Pia, Serikali imeimarisha huduma kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, ikiwemo bima ya afya na kuongeza fedha za matumizi kutoka Sh1.3 milioni hadi Sh1.5 milioni kwa wanafunzi wa Zanzibar.

Akizungumza wakati akifungua maonyesho ya tano ya wiki ya elimu ya juu katika uwanja wa Maisara kisiwani hapa leo Alhamisi, Julai 18, 2024, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla amesema mfumo huo utawawezesha wanafunzi kukamilisha masomo yao.

“Serikali inafanya kila jitihada kuhakikisha kila mwanafunzi anayefaulu kwenda chuo kikuu hakosi masomo kwa sababu ya kushindwa kulipa ada,” amesema.

Amesema wanafunzi wanaosoma Tanzania Bara wameongezewa fedha za matumizi kutoka Sh1.5 milioni hadi kufikia Sh1.8 milioni ili waweze kumudu gharama wanapokuwa vyuoni.

Sambamba na hayo, Hemed amesema Serikali imeongeza bajeti ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu Zanzibar (ZHESLB) kutoka Sh26.93 bilioni mwaka 2023/24 hadi Sh30.5 bilioni mwaka 2024/25.

Amesema fedha hizo zitawanufaisha wanafunzi 7,367, wakiwemo 4,297 wanaoendelea na masomo, wapya 3,070 na 1,000 wa stashahada.

“Kupitia maonyesho ya wiki ya elimu ya juu wanafunzi hupatiwa taarifa mbalimbali za kimasomo zikiwemo za upatikanaji wa mikopo, namna ya kujiunga na vyuo vya ndani na nje ya nchi na kutoa hamasa kwa wanafunzi kusoma kwa bidii,” amesema Abdulla.

Awali, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohamed Mussa amesema kazi inayofanywa na Serikali ya kuimarisha miundombinu ya elimu inasababisha ongezeko la ufaulu na kuiletea heshima Zanzibar.

Miongoni mwa mafanikio amesema ni kuongezeka kwa ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha sita kutoka wanafunzi 2,570 mwaka 2023 sawa na asilimia 99.3 hadi wanafunzi 3,387 sawa asilimia 99.5 kwa mwaka 2024.

Amesema wanafunzi hao wamepata ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu na wote wanatarajiwa kujiunga na vyuo vikuu ndani na nje ya nchi.

“Maonyesho ya elimu ya juu yatawasaidia wanafunzi katika kufanya udahili wa vyuo na kupata taaluma ya juu, kupata mikopo ya elimu juu itakayowezesha kusoma pasipo na changamoto ya aina yoyote,” amesema Lela. 

Akisoma taarifa ya kitaalamu, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali (Utawala), Khalid Masoud Waziri amesema lengo kuu la maonyesho hayo ni kuimarisha ushirikiano baina ya taasisi za elimu, vyuo na benki ili kuhakikisha sekta ya elimu inaendelea kuimarika na ufaulu kuongezeka. 

Hata maonyesha yenyewe, Khalid amesema yanazidi kuimarika kwani mwaka 2020  washiriki kutoka taasisi za elimu walikuwa 17, mwaka 2023 wakafikia 54 na mwaka huu wapo 77. 

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading