Siri ya Uhuru wa Tanganyika

Siri ya Uhuru wa Tanganyika

Siri ya Uhuru wa Tanganyika

Wakati Tanzania Bara ikiadhimisha miaka 63 ya Uhuru, ni wazi kuwa uwezo wa kujenga hoja wa Mwalimu Julius Nyerere ulikuwa kiini cha kufanikisha Uhuru wake kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza Desemba 9, 1961.

Katika kitabu “Tanganyika’s Independence Struggle” kilichoandikwa na Pius Msekwa, Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania na Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Msekwa anaelezea jinsi uwezo wa kipekee wa Nyerere wa kujenga hoja ulivyowashawishi viongozi wa chama cha Tanu kumtuma kwenda Baraza la Wadhamini la Shirikisho la Umoja wa Mataifa (UNO), ambalo sasa linafahamika kama Umoja wa Mataifa (UN).

Msekwa anasema mwaka 1954, wajumbe wa Baraza la Wadhamini la UNO walipokuja Tanganyika walitoa mapendekezo ya ratiba ya kuipa nchi uhuru ndani ya kipindi cha miaka 20 hadi 25. Wakati huo, Nyerere alikuwa mwalimu katika Shule ya Mtakatifu Francis, Pugu, ambayo sasa inajulikana kama Shule ya Sekondari Pugu.

Hata hivyo, viongozi wa Tanu walipinga ratiba hiyo wakiona ni kuchelewesha maendeleo ya nchi. Walimkabidhi Nyerere jukumu la kuwasilisha hoja ya Tanganyika kupata Uhuru haraka zaidi kwenye Baraza la Wadhamini la UNO huko New York, Marekani.

Nguvu ya hoja na matokeo ya haraka

Kwa ushawishi wa hoja za Nyerere, Tanganyika ilipata Uhuru ndani ya miaka saba tu, kutoka mwaka 1954 hadi 1961, tofauti na mapendekezo ya miaka 20-25. Mafanikio haya yalimfanya Nyerere kuwa kiongozi mwenye mvuto mkubwa kitaifa na kimataifa.

Changamoto ya uamuzi mgumu

Aliporejea kutoka UNO, Nyerere alikumbana na barua kutoka kwa Padri Walsh, mkuu wa Shule ya Mtakatifu Francis, akimtaka achague kati ya siasa na kazi ya ualimu.

Kwa maoni ya Walsh na wamisionari wenzake, Nyerere alionekana kuwa mwanaharakati wa kisiasa zaidi kuliko mwalimu wa kawaida.

Tatizo hilo liliwasilishwa kwa Clement Mtamila, Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Tanu. Kamati hiyo iliku-tana nyumbani kwa Mtamila kmtaa wa Kipata, na baada ya mjadala, ilimshauri Nyerere kujiuzulu. Machi 23, 1955, Nyerere aliacha rasmi kazi ya ualimu na kujitosa kikamilifu kwenye siasa.

Mwalimu na uzalendo

Uamuzi huo wa Nyerere uliashiria mwanzo wa safari yake kama kiongozi wa kitaifa. Siku hiyo, alisafiri kutoka Pugu hadi Dar es Salaam akiwa si mwalimu tena, bali kiongozi aliyejitoa kikamilifu kuikomboa Tanganyika.

Miaka 63 baadaye, mchango wa Mwalimu Nyerere unabaki kuwa mfano wa uzalendo na uongozi wa maono, akiwahamasisha Watanzania kuendeleza azma ya kujitegemea na maendeleo.

Safari ya Nyerere UNO

Mwanahistoria Mohammed Said, mwandishi wa kitabu kuhusu Abdulwayde Sykes, anasimulia tukio hili kupitia simulizi aliyosikia kutoka kwa mtoto wa Iddi Faiz Mafungo, aliyekuwa mweka hazina wa Tanu kabla ya uhuru. Said anaeleza jinsi mipango ya safari ya Nyerere ilivyopangwa sebuleni nyumbani kwa Mafungo.

Mafungo, akiwa mweka hazina wa Tanu, alihusika kukusanya fedha. Mwanahistoria huyo anasema jioni moja ya Februari, kikao muhimu kilifanyika nyumbani kwa Mafungo, kikihusisha viongozi wengine mashuhuri wa Tanu, akiwemo Oscar Kambona na John Lupia, aliyekuwa Makamu wa Rais wa Tanu.

Katika kikao hicho, Kambona na Lupia walimweleza Mafungo changamoto za kifedha zilizokuwepo.

“Sheikh, kama unavyoelewa bado hatujapata pesa za kutosha kumpeleka Mwalimu UNO.”

Mafungo asafiri Tanga

Kwa mujibu wa simulizi hiyo, Mafungo alipewa jukumu la kwenda Tanga kuchukua fedha zilikusanywa na wanachama wa Tanu chini ya uongozi wa Mwalimu Kihere.

Fedha hizo zilikusanywa kufanikisha safari ya Nyerere kwenda Umoja wa Mataifa, safari ambayo ingekuwa ya kwanza kwake kuzungumza mbele ya Baraza la Wadhamini la UNO.

Safari hiyo ilifanikiwa kutokana na mshikamano wa viongozi wa Tanu na wanachama wake, licha ya changamoto za kiusalama kutoka kwa watawala wa kikoloni wa Uingereza.

Kwa Said, simulizi hii inaakisi mchango wa watu kama Mafungo na viongozi wa Tanu waliojitolea kwa hali na mali kuhakikisha ndoto ya uhuru inakaribia kutimia.

Katika kikao cha Tanu kilichofanyika nyumbani kwa Iddi Faiz Mafungo, John Lupia alimweleza Mafungo kuhusu taarifa walizopokea kutoka Tanga kwamba mwanachama wa Tanu, Mwalimu Kihere, aliripotiwa kuwa amekusanya fedha kutoka kwa wanachama wa chama hicho, fedha ambazo zilikuwa muhimu kufanikisha safari ya Mwalimu Nyerere kwenda Umoja wa Mataifa.

Mafungo, akiwa mweka hazina wa Tanu, alipewa jukumu la kwenda Tanga kuchukua fedha hizo.

Mafungo alisafiri kwenda Tanga salama na kukabidhiwa fedha hizo, lakini hakujua kuwa alikuwa akifu-atiliwa kwa karibu na maofisa wa ‘Special Branch’, idara ya ujasusi ya polisi wa kikoloni wa Uingereza.

Wakati huo, Waingereza walijua kuhusu mipango ya Nyerere kwenda UNO na walikuwa wakifanya kila jitihada kufuatilia harakati za Tanu.

Mafungo aokoa fedha

Akiwa na wasiwasi kuhusu usalama wa fedha hizo, Mafungo alibuni mpango wa kuzilinda. Akiwa ndani ya basi lililokuwa likielekea Dar es Salaam, alimkabidhi begi lenye fedha binti mdogo aliyekuwa akisafiri kwenye basi hilo. Kwa busara, hakukaa karibu na binti huyo na alihakikisha hawakujulikana kuwa wali-husiana.

Safari yao ilipofika katikati ya njia, basi lilisimamishwa na Land Rover ya polisi wa kikoloni. Mafungo alishushwa pamoja na mizigo yake kwa ukaguzi wa kina, huku abiria wengine wakiruhusiwa kuendelea na safari. Polisi walimpekua Mafungo na mizigo yake kwa makini, lakini hawakupata chochote.

Hawakujua kuwa binti mdogo aliyekuwa kwenye basi hilo ndiye aliyekuwa na begi lenye fedha. Baada ya kuwasili Dar es Salaam, binti huyo alizifikisha fedha hizo salama makao makuu ya Tanu, eneo ambalo sasa linafahamika kama ofisi ndogo za makao makuu ya CCM Lumumba.

Mafungo alikamatwa na kuhojiwa Kituo Kikuu cha Polisi kilichokuwa karibu na ofisi za reli (sasa eneo la stesheni ya SGR). Baada ya uchunguzi, hakufunguliwa mashtaka kwa sababu hapakuwa na ushahidi wowote wa kumtia hatiani.

Wanaharakati waliojitoa muhanga

Mwanahistoria Mohammed Said anasema mafanikio ya harakati za uhuru yalitokana na juhudi za watu waliotoa muda, mali na hata kuhatarisha maisha yao kwa ajili ya Tanganyika.

Anamtaja Sheikh Mohamed Rania wa Bagamoyo, ambaye ushawishi wake ulihamasisha wanachama wa Tanu katika eneo hilo. Mafungo alimpeleka Mwalimu Nyerere kwa sheikh huyo ambaye alikuja ku-wa sehemu muhimu ya harakati hizo.

Mwanaharakati mwingine aliyetoa mchango alikuwa Mwamtoro binti Chuma, ambaye nyumba yake jijini Dar es Salaam iliunganishwa na ofisi za Tanu ili kurahisisha mikutano ya usiku na kupanga mikakati ya ukombozi.

Wanaharakati wa kike wengine kama Nyange binti Chande wa Tabora, Halima Selengia wa Kaskazini, na Lucy Lameck walitoa mchango katika nyanja mbalimbali za harakati hizo.

Vijana watukutu walinzi Siku ya Uhuru

Katika shamrashamra za kutangaza uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, hofu ilikuwepo kwamba huenda siku hiyo ingetibuliwa na vitendo vya uhalifu. Hata hivyo, kupitia ujasiri na mbinu za ubunifu za viongozi wa Tanu, hali hiyo ilidhibitiwa kwa njia ya kipekee.

Said anaeleza jinsi Kamanda Rajabu Diwani, aliyekuwa Kamanda wa Vijana wa Tanu, alivyochukua hatua ya kuwajumuisha vijana watukutu wa Dar es Salaam katika mpango wa kulinda mji.

Vijana hao, ambao awali walijulikana kwa tabia zao za kuleta vurugu, walipewa sare rasmi na kibarua cha kusimamia amani. “Diwani aliwakusanya vijana waliokuwa maarufu kwa utukutu na kuwapa juku-mu la kuhakikisha mji unakuwa salama siku ya sherehe za Uhuru,” anasema Said.

Katika siku hiyo muhimu, vijana hao walifanya kazi ya kuigwa.

Miaka 63 baadaye: Undugu umepungua

Huku akiangalia historia ya Tanganyika, Said anasema moja ya mambo ya kipekee yaliyokuwepo wakati huo ni mshikamano wa undugu uliowajumuisha Watanganyika wote.

Anahuzunika kuona mshikamano huo umepungua kwa kiasi kikubwa sasa. Licha ya maendeleo katika miundombinu na sekta nyingine, undugu uliochochea harakati za uhuru hauonekani kwa nguvu ile ile.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading