Simulizi ya padri aliyepanda miti zaidi ya milioni 1.7 katika miaka 65

Simulizi ya padri aliyepanda miti zaidi ya milioni 1.7 katika miaka 65

Simulizi ya padri aliyepanda miti zaidi ya milioni 1.7 katika miaka 65

Mwanza. “Tangu nimeanza kupanda miti mwaka 1959 nikiwa darasa la kwanza mpaka sasa nimepanda zaidi ya miti 1,700,000 kiasi kwamba sasa kila ninapokwenda huwa nakutana na watu wananiambia huu ni mti wangu nilipanda.”

Hayo ni maneno ya Padri wa Kanisa la Katoliki Jimbo la Geita, Thomas Bilingi wakati akisimulia namna alivyopanda miti zaidi ya 1,700,000 katika kipindi cha miaka 65.

Akizungumza na Mwananchi leo Disemba 7, 2024 baada ya kufanya matembezi ya kuhamasisha watu kutumia nishati safi jijini Mwanza, Padri Bilingi mwenye miaka 76 sasa, amesema alivutiwa kuanza kupanda miti baada ya kubaini miti ya matunda huleta ujirani mwema.

“Tangu kuzaliwa kwangu nyumbani nilikuta kuna mti wa matunda ambao kwa kilugha chetu unaitwa Sungwi, sasa watoto wa majirani walikuwa wakija nyumbani kula matunda hayo, nikaona kumbe miti ya matunda inaleta ujirani mwema na huduma mbalimbali,” amesema.

“Nilianza kupanda miti nikiwa na umri wa miaka 11 wakati naingia darasa la kwanza, mwaka 1959, katika shule ya msingi Kasisa iliyopo Buchosa, Mwanza, nikaja kuendelea nikiwa darasa la tano ambapo hapo nilianza kupanda miti kwa wingi,” ameongeza.

Padri Bilingi amesema miti hiyo ameipanda katika maeneo mbalimbali ambayo amekuwa akipita, mfano kwenye taasisi za elimu, dini, Serikali na maeneo binafsi.

“Baadhi ya shule nilizowahi kupanda miti ni shule ya msingi Kasisa, St Ambrose Mitere baada ya hapo nikaenda Nsumba sekondari, kila sehemu nilipokuwa naenda nilikuwa napanda miti na mara nyingi nilikuwa peke yangu, japo baadaye niliamua kushirikisha wenzangu tukawa kama kikundi nikishirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS),” amesema.

Ameongeza: “Changamoto kubwa ambayo nilikuwa nikikumbana nayo ni kuchekwa, uharibifu wakati mwingine mifugo inapelekwa kwenye maeneo ambayo nimepanda miti. Changamoto nyingine ni wizi, japo hii wakati mwingine nilikuwa na furahia kwamba kama wanaiba mti ina maana anaenda kupanda nyumbani kwake, kitu ambacho ni kizuri,” amesema.

Hata hivyo, amesema mbali na kupanda miti, pia, huwa anahamasisha watu kupanda kupitia mahubiri, mafundisho na kuongea na mtu binafsi akiwaeleza umuhimu wake.

“Nikiwa nafundisha mfano leo Jumamosi, nina vipindi vya ndoa kanisani huwa nawapatia mti na kuwaambia wakapande, endapo ikitokea mti huo ukakauka basi na ndoa yao itakuwa imeishia hapo, huwa wanakuja wananiambia ndoa haijavunjika na mti wenyewe haujakauka,” amesema Padri Bilingi.

Kiongozi huyo wa kiroho amesema moja ya siri ya kuendelea kuwa hai mpaka sasa,ni kutokana na yeye kupanda miti ambayo inamsaidia kiafya na wakati mwingine kujitibu.

“Kupanda miti ipo kwenye damu ndio maana kuna muda huwa nakula majani ya miti hiyo kwa sababu inanisaidia kusafisha na kutibu kifua, mfano badala ya kutumia majani ya dukani mimi nachuma majani ya mti wa mchachai, nakunywa,” amesema.

Akizungumzia maisha ya padri huyo, mmoja wa wadau wa mazingira jijini Mwanza, William Missanga, mbali na kumpongeza amesema kwake kama kijana inamtia nguvu ya kuendelea kupambana kuhakikisha jamii inaondokana na matumizi ya nishati chafu, huku suala la upandaji miti akilipa kipaumbele.

“Ni jambo la kusisimua kwa mimi kama kijana, linanifunza mambo mengi na kunifanya nione bado dunia inanitaka. Bado nina safari ndefu ya kufikia rekodi ya mtu kama huyo kwa sababu sio jambo la kawaida linahitaji kujituma na kuwa moyo,” amesema Missanga.

Balozi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya MR Tree Foundation, Mrisho Mabanzo (Mr Tree) amesema siku 10 zilizopita amempoteza mama yake, chanzo kikiwa ni moshi uliokuwa unatokana na matumizi ya kuni na mkaa.

“Mama yangu alikuwa mfanyabiashara mkubwa sana wa mkaa mpaka ikawa inafikia wakati analipia miti ili kukata na kupata kuni,  lakini madhara yake miaka 30 mbele tumejikuta tunatumia gharama kubwa kumtibu mpaka kumpoteza kwa sababu ya athari zilizobainika kuwa zimetokana na matumizi ya nishati isiyo salama kwa maana ya moshi wa kuni na mkaa,” amesema Mr Tree.

Akizungumzia takwimu, Mr Tree Amesema: “Asilimia 16 ya ardhi ya Tanzania imeelekea kuwa jangwa, zaidi ya ekari 469,000 zinaharibiwa kila mwaka kutokana na matumizi ya kibinadamu hasa matumizi ya kuni na mkaa, hivyo ni viashiria vinatuonyesha hali ya hatari ndiyo maana hali ya hewa haitabiriki.”

Askari mhifadhi misitu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Kanda ya Ziwa, Maija Mkomwa amewataka wananchi kufika kwenye ofisi zao kwa ajili ya kujipatia miti bure ya matunda ya kupanda, huku akihimiza jamii kuachana na nishati chafu.

“TFS tunatoa wito kwa wananchi kwanza kutumia nishati safi kwa maana ya umeme na gesi lakini pia waondokane na nishati zinazoleta uharibifu wa mazingira, mfano kuni na mkaa,. Pia wananchi wapande miti kwa wingi kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi,” amesema Mkomwa.

Naye Mkurugenzi wa Watengenezaji wa KuniSmart na JikoSmart kutoka kampuni ya Chabri Energy, Bernard Makachia ametoa wito kwa kampuni za gesi kupunguza gharama za mitungi ya gesi ili kuwawezesha Watanzania wengi kumudu kununua.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns

Several airports have since locked Air Tanzania, dealing a severe blow to the Tanzanian national carrier that must now work overtime to regain its certification or go the wet lease way

The European Commission has announced the inclusion of Air Tanzania on the EU Air Safety List, effectively banning the airline from operating in European airspace.

The decision, made public on December 16, 2024, is based on safety concerns identified by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), which also led to the denial of Air Tanzania’s application for a Third Country Operator (TCO) authorisation.

The Commission did not go into the specifics of the safety infringement but industry experts suggest it is possible that the airline could have flown its Airbus A220 well past its scheduled major checks, thus violating the airworthiness directives.

“The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards for passengers in Europe and worldwide,” said Apostolos Tzitzikostas, EU Commissioner for Sustainable Transport and Tourism.

“We strongly urge Air Tanzania to take swift and decisive action to address these safety issues. I have offered the Commission’s assistance to the Tanzanian authorities in enhancing Air Tanzania’s safety performance and achieving full compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania has a mixed fleet of modern aircraft types including Boeing 787s, 737 Max jets, and Airbus A220s.

It has been flying the B787 Dreamliner to European destinations like Frankfurt in Germany and Athens in Greece and was looking to add London to its growing list with the A220.

But the ban not only scuppers the London dream but also has seen immediate ripple effect, with several airports – including regional like Kigali and continental – locking out Air Tanzania.

Tanzania operates KLM alongside the national carrier.

The European Commission said Air Tanzania may be permitted to exercise traffic rights by using wet-leased aircraft of an air carrier which is not subject to an operating ban, provided that the relevant safety standards are complied with.

A wet lease is where an airline pays to use an aircraft with a crew, fuel, and insurance all provided by the leasing company at a fee.

Two more to the list

The EU Air Safety List, maintained to ensure passenger safety, is updated periodically based on recommendations from the EU Air Safety Committee.

The latest revision, which followed a meeting of aviation safety experts in Brussels from November 19 to 21, 2024, now includes 129 airlines.

Of these, 100 are certified in 15 states where aviation oversight is deemed insufficient, and 29 are individual airlines with significant safety deficiencies.

Alongside Air Tanzania, other banned carriers include Air Zimbabwe (Zimbabwe), Avior Airlines (Venezuela), and Iran Aseman Airlines (Iran).

Commenting on the broader implications of the list, Tzitzikostas stated, “Our priority remains the safety of every traveler who relies on air transport. We urge all affected airlines to take these bans seriously and work collaboratively with international bodies to resolve the identified issues.”

In a positive development, Pakistan International Airlines (PIA) has been cleared to resume operations in the EU following a four-year suspension. The ban, which began in 2020, was lifted after substantial improvements in safety performance and oversight by PIA and the Pakistan Civil Aviation Authority (PCAA).

“Since the TCO Authorisation was suspended, PIA and PCAA have made remarkable progress in enhancing safety standards,” noted Tzitzikostas. “This demonstrates that safety issues can be resolved through determination and cooperation.”

Another Pakistani airline, Airblue Limited, has also received EASA’s TCO authorisation.

Decisions to include or exclude airlines from the EU Air Safety List are based on rigorous evaluations of international safety standards, particularly those established by the International Civil Aviation Organization (ICAO).

The process involves thorough review and consultation among EU Member State aviation safety experts, with oversight from the European Commission and support from EASA.

“Where an airline currently on the list believes it complies with the required safety standards, it can request a reassessment,” explained Tzitzikostas. “Our goal is not to penalize but to ensure safety compliance globally.”

Airlines listed on the EU Air Safety List face significant challenges to their international operations, as the bans highlight shortcomings in safety oversight by their home regulatory authorities.

For Air Tanzania, this inclusion signals an urgent need for reform within Tanzania’s aviation sector to address these deficiencies and align with global standards.

The path forward will require immediate and sustained efforts to rectify safety concerns and regain access to one of the world’s most critical aviation markets.

Source: allafrica.com

Continue Reading