Siku ya Bia duniani inayowagusa Watanzania, watumiaji waeleza ‘vibe’ lake

Siku ya Bia duniani inayowagusa Watanzania, watumiaji waeleza ‘vibe’ lake

Dar es Salaam. Wanywaji wa bia nchini Tanzania, leo Ijumaa Agosti 2, 2024 wanaungana na wenzao duniani kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Bia inayolenga kuwaleta pamoja marafiki katika kufurahia ladha ya bia.

Siku ya Kimataifa huadhimishwa Ijumaa ya kwanza ya Agosti kila mwaka ambapo kwa mwaka huu imeangukia Agosti 2.

Maadhimisho ya siku hii yalianzia huko Santa Cruz, California nchini Marekani, mwaka 2007. Hadi sasa siku hii inasherehekewa katika miji 207 katika nchi 50 duniani zilizotawanyika katika mabara sita.

Lengo la kuanzishwa kwa kilevi hiki lilikuwa ni kuwaleta pamoja kufurahia ladha ya bia, kuwapongeza wanaozalisha bia na wanaohudumia pamoja na kuwaunganisha watu wa mataifa yote duniani kupitia kinywaji hiki pendwa.

Kila jamii duniani ina aina yake ya bia na historia inaonyesha kinywaji hiki kilianza kutengenezwa kisasa katika karne ya 18, hata hivyo, kabla ya hapo zilikuwepo pombe mbalimbali zilizokuwa zikitengenezwa kienyeji kutokana na teknolojia kuwa duni.

Tanzania pia ina wanywaji wengi wa bia ambao kuanzia siku za mwisho wa wiki kama Ijumaa, Jumamosi na Jumapili, wanakusanyika kwenye baa mbalimbali na kujumuika na watu tofauti.

Akizungumzia siku hii, mnywaji wa bia, Gaston Kimario amesema anapenda kunywa bia kwa sababu inampa ujasiri wa kuzungumza na watu na kwa njia hiyo amekuwa akikutana na watu wapya wanaomfungulia fursa mbalimbali.

“Bia inanipa vibe (msisimko), nakuwa najiamini kumfuata mtu, nikaongea naye na tukawa marafiki. Nimepata dili nyingi kwa watu niliokutana nao baa tu. Nafurahi kama kuna siku hii, nitasherehekea pia,” amesema Kimario ambaye ni mfanyabiashara.

Mwandishi mmoja wa habari ambaye hakutaka kutajwa jina lake, amesema anakunywa bia ili kupunguza msongo wa mawazo unaosababishwa na kazi anayoifanya. Amesema anapenda kinywaji hicho kwani kinampa furaha hasa anapokutana na marafiki.

“Nakunywa kwa kujumuika na watu, pombe hainywewi nyumbani, baa ndiyo kuna burudani. Sijui nitaacha lini, lakini naendelea kunywa bia,” amesema mwanamke huyo.

Mmiliki wa baa moja iliyopo Pugu, jijini Dar es salaam,  Onesmo Lyanga amesema hafahamu kama kuna siku ya kimataifa ya bia, hata hivyo, amesema kinywaji hicho hakiepukiki na kutokana na hilo aliona fursa na kuanzisha baa ili kujiingizia kipato.

“Miaka ijayo nitakuwa naifanya siku hii kuwa kubwa, mie nafanya biashara, siku kama hii ni fursa kwangu. Nitawawekea wateja wangu burudani itakayosindikiza unywaji wao,” amesema Lyanga.

Mkazi wa Katoro, Mkoa wa Geita, Frank John anasema kinywaji hicho kinapotumika vizuri kinachangia mapato ya nchini na jamii kwa ujumla.

“Kuna watu wanategemea uuzaji wa vinywaji, wanasomesha, wanajenga na kuendesha maisha yao kwa hiyo ni jambo jema kutambua siku hii muhimu na kwa kweli pombe tamu asikwambie mtu,” amesema John.

Akizungumzia mtazamo wa kiimani, Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Viongozi wa Dini, Askofu William Mwamalanga amesema Biblia inaelezwa ulevi unakaribisha uvivu, hivyo haoni umuhimu wa kuwa na siku ya bia duniani.

Amesema watu wanaolewa hawafanyi kazi na hawezi kutoa majibu kwenye changamoto zinazomkabili yeye au jamii yake, hivyo ameiomba serikali kupiga vita siku hiyo kuadhimishwa hapa nchini kwani ulevi ni laana.

“Mapato ya bia ni ya laanaa, huwezi kupata maendeleo kwa pesa za bia. Kuna nchi zimepiga marufuku ulevi na zimefanikiwa kimaendeleo, mfano nchi za Kiarabu kama Qatar, wana maendeleo na hawanywi pombe,” amesema Askofu Mwamalanga.

Askofu huyo amehoji kwamba kwanini kusiwe na siku ya kuhamasisha amani duniani badala ya ulevi wa bia. Amesema imani inakataza unywaji wa pombe kwa misingi kwamba Taifa la walevi haliwezi kufanikiwa.

“Mungu anasema mkalewe katika roho na siyo katika mwili. Watu wanaolewa hawawezi hata kutunza familia zao, pesa zote wanazopata zinaishia kwenye bia. Wanaonufaika ni kampuni za bia tu, mlevi hanufaiki chochote,” amesema askofu huyo.

Wakati wadau walieleza hayo, tahadhari mbalimbali zimekuwa zikitolewa na kampuni zinazotengeneza bia kuhusu matumizi ya kinywaji hicho. Kwanza, kuna tahadhari isemayo “Kinywaji hiki hakipaswi kuuzwa kwa walio chini ya miaka 18”.

Pia, tahadhari nyingine inayotolewa ni “Unywaji kupitia kiasi ni hatari kwa afya yako. Kadhalika, wanywaji wanaonywa kupitia usemi wa kimombo “Don’t drink and drive” (usinywe pombe na kuendesha).

Tahadhari hizi zote tatu zinaandikwa kwenye chupa ya bia ili kumkumbusha mnywaji kuchukua tahadhari kuhusu matumizi ya kilevi hicho pendwa hasa kwa vijana. Kupuuzwa kwa tahadhari hizo, mnywaji anaweza kujikuta akipata madhara kwa namna tofauti yatakayomfanya ajutie kutumia bia maishani mwake.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading