Siku tisa kuelekea uchaguzi, zinahitaji haya

Siku tisa kuelekea uchaguzi, zinahitaji haya

Siku tisa kuelekea uchaguzi, zinahitaji haya

Dar es Salaam. Wakati sekunde zikizidi kuyoyoma, saa zikikimbia na siku tisa tu zikisalia kabla ya Watanzania kuelekea kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa, kila mmoja  ana wajibu wa pekee kuhakikisha anashiriki kikamilifu kwenye mchakato huu wa kidemokrasia.

Uchaguzi huo, uliopangwa kufanyika Novemba 27, 2024 una nafasi kubwa ya kubadili mustakabali wa jamii zetu kwa miaka mitano ijayo.

Hii ni nafasi ya kuandaa daraja la maendeleo au kujiweka katika mahangaiko na changamoto za kijamii na kiuchumi. 

Kwa siku tisa zilizosalia kuelekea uchaguzi huo, kuna mambo ya msingi unayopaswa kuzingatia.

Ulijiandikisha?

Ni muhimu kila mpiga kura kuhakikisha majina yake yameorodheshwa kwenye daftari la wapiga wakazi.

Daftari hilo, ndilo linalotumika kuorodhesha majina ya wakazi wa maeneo husika na ndilo linalokuhalalisha kushiriki kupiga au kupigiwa kura.

Kwa mujibu wa Tume Huru ya TaiFa ya Uchaguzi (INEC) mwaka 2019, zaidi ya wapiga kura milioni sana walijiandikisha, lakini takriban asilimia 15 hawakujitokeza kupiga kura kwa sababu ya changamoto za kutothibitisha majina yao mapema.

Katika siku hizi chache, ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha hana vikwazo vya kiutaratibu na sheria vinavyomzuia kushiriki mchakato huo.

Wagombea na sera zao

Kwa siku zilizobaki Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na vyama vya siasa vina jukumu la kuhakikisha wananchi wanapata taarifa za kina kuhusu wagombea.

Kwa sababu tayari uteuzi umeshafanyika na pazia la kampeni linaenda kufunguliwa, sera ndizo zitakazoamua ushindi wa mgombea.

Uchaguzi si sherehe ya majina maarufu bali ni mchakato wa kuchagua viongozi wenye uwezo wa kuleta maendeleo.

Katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2019, utafiti wa Repoa ulionyesha asilimia 45 ya wapiga kura hawakujua kikamilifu sera za wagombea wao, jambo lililochangia uchaguzi wa viongozi wasiowajibika kwa jamii.

Mpiga kura anapaswa kutumia siku hizi tisa zilizobaki kuhudhuria mikutano ya kampeni, zitakapozinduliwa, kusoma ilani za vyama na hata kuuliza maswali magumu ili kufanya maamuzi sahihi. 

Amani na utulivu

Historia ya Tanzania imejaa mifano ya mafanikio ya kuendesha chaguzi kwa amani.

Lakini tunapaswa kuwa waangalifu dhidi ya kauli na vitendo vinavyoweza kuchochea vurugu.

Mwaka 2020, ripoti ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), ilionyesha asilimia 20 ya vurugu za uchaguzi zilitokana na mivutano ya kidini na kikabila, hasa wakati wa kampeni.

Sasa ni wakati wa kudumisha mshikamano, kuelekeza mijadala kwenye hoja badala ya chuki na kuhakikisha tunaacha mfano bora kwa kizazi kijacho. 

Hamasa kwa wapiga kura

Ushiriki wa wananchi katika uchaguzi ni ishara ya nguvu ya kidemokrasia.

Katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2019, ni asilimia 65 tu ya waliojiandikisha walijitokeza kupiga kura.

Takwimu hizo zinaonyesha bado kuna kazi kubwa ya kuwahamasisha watu kushiriki.

Familia, marafiki na majirani wanapaswa kushirikiana kuhamasishana ili ifikapo Novemba 27 kila mmoja awe sehemu ya mabadiliko. 

Kuimarisha maandalizi ya siku ya uchaguzi

Kwa wapiga kura, kuhakikisha wanajua vituo vyao vya kupigia kura ni hatua muhimu.

Hii husaidia kuepuka msongamano na kuchanganyikiwa siku ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa ripoti ya INEC 2019, asilimia 10 ya wapiga kura walishindwa kupiga kura kwa wakati kwa sababu ya kushindwa kufika vituoni mapema. 

Kwa mamlaka zinazohusika, hatua hizi chache zilizobaki ni fursa ya kuhakikisha vifaa vyote vya uchaguzi vipo tayari, watumishi wamepewa mafunzo ya kutosha, na mazingira ya vituo vya kura ni rafiki kwa wapiga kura wote, wakiwemo wazee, wanawake wajawazito na watu wenye ulemavu. 

Kujiepusha na rushwa, uvunjifu maadili

Rushwa imeendelea kuwa changamoto katika chaguzi mbalimbali.

Transparency International iliripoti mwaka 2020 kwamba asilimia 18 ya wapiga kura walirubuniwa kwa njia ya rushwa ili kuwachagua wagombea fulani.

Wakati huu tunapokaribia siku ya uchaguzi, ni muhimu kuhakikisha maamuzi ya wananchi hayashawishiwi na zawadi za muda mfupi, bali yanatokana na utashi wa kweli wa mabadiliko. 

Kulinda haki za wengine

Kila mmoja ana haki ya kupiga kura kwa uhuru na usalama.

Mikutano ya kampeni inapaswa kuheshimu sheria za uchaguzi na wapiga kura wanapaswa kuacha tabia ya kuwakatisha tamaa wengine kushiriki.

Kwa mujibu wa sheria za uchaguzi nchini, vitendo vya kuwatishia wapiga kura vinaweza kusababisha kifungo cha hadi miaka mitatu jela.

Kujiandaa kisaikolojia na kifamilia

Katika siku hizi chache, ni muhimu kuhakikisha kwamba familia zimetayarishwa kwa siku ya uchaguzi.

Hakikisha watoto wapo salama, na ratiba ya siku hiyo imepangwa vizuri ili kuepusha mizozo.

Uchaguzi ni suala la kijamii linalohitaji mshikamano wa kifamilia na kijamii. 

Siku tisa zinaweza kuonekana kuwa chache, lakini zinaweza kuwa msingi wa kuleta mabadiliko makubwa.

Kama Taifa, tunapaswa kutumia kila saa iliyobaki kuhakikisha tunajiandaa kwa njia sahihi kushiriki katika zoezi hili muhimu.

Huu ni wakati wa kuonyesha uzalendo kwa kuchagua viongozi wanaostahili na kuhakikisha kuwa demokrasia yetu inazidi kuimarika. 

Tukumbuke kwamba kila kura ina uzito mkubwa. Kwa kila mmoja wetu anayejitokeza kupiga kura, tunaandika ukurasa mpya wa historia ya Taifa letu.

Tafakari, jipange na uhakikishe siku ya Novemba 27 inakuwa ya kipekee kwa maendeleo yetu.

Vyombo vya habari pia vina nafasi muhimu ya kuhakikisha vinaripoti taarifa bila kuegemea upande wa chama chochote cha siasa.

Kwa mujibu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), uandishi wa uchaguzi unapaswa kuwa wa uwiano, kuzingatia maadili na kutoa fursa sawa kwa wagombea wote.

Katika siku hizi tisa, vyombo vya habari vina jukumu la kuelimisha wapiga kura, kufichua changamoto za kiutaratibu, na kupaza sauti za wananchi wanaotafuta mabadiliko.

Huu ni wakati wa kuonyesha uzalendo kwa kuchagua viongozi wanaostahili na kuhakikisha kuwa demokrasia yetu inazidi kuimarika.

Tukumbuke kila kura ina uzito mkubwa. Kwa kila mmoja  anayejitokeza kupiga kura, anaandika ukurasa mpya wa historia ya Taifa.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading