Shule iliyosababisha mkandarasi kutimuliwa Zanzibar yafunguliwa

Shule iliyosababisha mkandarasi kutimuliwa Zanzibar yafunguliwa

Unguja. Shule ya Sekondari iliyosababisha mkandarasi kuzuiwa kufanya kazi Zanzibar imekamilika na kufunguliwa rasmi.

Sekondari hiyo iliyopewa jina la Hassan Khamis Hafidh yenye ghorofa tatu ina madarasa 41.

Mwonekano wa Shule ya Sekondari  Hassan Khamis Hafidh.

Ujenzi wake umegharimu Sh5.4 bilioni ambao ulianza Februari 2022.

Kwa mujibu wa mkataba ilitakiwa kukamilika Agosti mwaka 2022.

Hata hivyo, alipotembelea ujenzi wa shule hiyo Julai 17, 2022, Rais wa Zanzibar,  Dk Hussein Mwinyi alikasirishwa kutokana na kusuasua kwa ujenzi uliokuwa ukitekelezwa na kampuni ya Associated Investiments Ltd ya Dar Salaam.

Dk Mwinyi aliagiza mkandarasi asitishiwe mkataba na asipwe zabuni yoyote Zanzibar.

Baadaye ujenzi wa shule hiyo  ulikabidhiwa kwa Chuo cha Mafunzo cha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kusimamiwa na kitengo cha ujenzi cha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali.

Akizungumza Aprili 22, 2024 wakati wa ufunguzi wa shule hiyo, Rais Mwinyi amesema licha ya mradi huo kukabiliwa na changamoto mbalimbali wakati wa utekelezaji, hatimaye umefanikishwa.

Amesema huo ni mradi pekee uliotekelezwa kwa fedha za Uviko-19 uliochelewa kuzinduliwa.

“Nipongeze chuo cha mafunzo kwa kukamilisha mradi huu, nia ya Serikali ni kupunguza msongamano wa wanafunzi wengi madarasani na kubakisha wastani wa wanafunzi 45 kwa kila darasa moja, sambamba na kuweka mkondo mmoja kwa skuli zote za Unguja na Pemba,” amesema Dk Mwinyi.

Amesema hali hiyo itasaidia matokeo mazuri kwa kuwepo mazingira mazuri ya kujifunzia.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Lela Muhamed Mussa, ameahidi kuisimamia kwa ufanisi wa hali ya juu miradi yote inayotekelewa na kusimamiwa na wizara.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Khamis Abdalla amesema ujenzi wa shule hiyo umejumuisha madarasa 41, ofisi nne za walimu, ofisi ya mwalimu mkuu, matundu 52 ya vyoo, maktaba, maabara, chumba cha kompyuta, stoo na ukumbi mkubwa wa mikutano.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading