Shirika la Umeme Zanzibar ZECO likiwa halifanyi kazi

Shirika la Umeme Zanzibar ZECO likiwa halifanyi kazi

Shirika la Umeme Zanzibar ZECO likitumbuiza

Utendaji kazi katika Shirika la Umeme umeporomoka kwa kiwango kikubwa huku wananchi wakilalamikia huduma zisizoridhisha.

Habari kutoka ZECO zinasema kuwa wateja wanaoomba kufungiwa mita katika mitaa yao wanasuburi kwa muda mrefu wengine miezi miwili, mitatu hadi sita.

Mbali na mita, huduma nyengine ambazo wananchi wanalalamikia ni pamoja na matengenezo ya dharura pale panapotokea hililafu, mafundi wa ZECO inawachukua muda mkubwa kurekebisha.

Habari zaidi kutoka shirika hilo zinasema kuwa kumekuwa na makundi yanayotishia ufanisi wa kazi huku wafanyakazi hasa wa ngazi ya chini wakilalamikia maslahi duni wanayopata na kuchelewa kushughulikia kwa madai yao mbalimbali.

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar na kiongozi wa wafanyabiashara wa serikali katika Baraza hilo mwezi Disemba alisema kuwa serikali inafanya juhudi kuhakikisha kunakuwepo na fursa sawa katika kutoa huduma za umma.

Hivi karibuni, serikali ya Zanzibar ilipunguza gharama za kuunganishiwa umeme, mpango ambao ulikuwa na lengo mahususi kuweka mazingira ya wateja kupata huduma ya umeme.

“Serikali imepunguza gharama za umeme kwa wananchi wake. Sasa ni jukumu la Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) kuhakikisha wananchi wanaohitaji umeme wanaunganishwa mara baada ya kufanya malipo. Kusiwe na ucheleweshaji usio wa lazima,” alisema na kuwataka wafanyakazi kuachana na rushwa, wizi na urasimu, badala yake wafanye kazi kwa uadilifu,” Hemed Suleiman Abdulla alisema.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla amefanya ziara ya kushtukiza Makao Makuu ya ZECO Gulioni ambapo hakuridhishwa na haki ya utendaji kazi.

Katika ziara yake hiyo, Makamu wa Pili wa Rais alionekana kama vile hakuridhishwa na uendeshaji hatua ambayo inapelekea kuonesha kushindwa kujiendesha ipasavyo.

Akizungumzia suala la uungwaji umeme kwa wananchi, Makamu wa Pili wa Rais alisema kuna zaidi ya watu 3000 wanasubiri kuunganishiwa umeme.

Ametoa muda wa Mwezi Mmoja Wananchi hao wawe tayari wameunganishiwa huduma hiyo.

Amesema suala la ucheleweshaji kuungiwa umeme wananchi hao inaonesha wazi uwepo wa mianya ya Rushwa kwa watendaji na kueleza kuwa Serikali haitamvumilia mtendaji yoyote atakaejaribu kujihusisha na aina yoyote ya Rushwa.

Pamoja na hayo Mhe. Hemed ameonesha kutoridhishwa na masuala ya kifedha hasa ukusanyaji na kuwataka kuziba mianya iliyokuwepo ili kudhibiti ukusanyaji huo na kuongeza pato la Taifa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameushauri Uongozi wa Shirika la Umeme Zanzibar kuandaa Mfumo mzuri wa Malipo mfumo ambao utapelekea kuwajua wenye madeni.

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year’s Most Read News Stories

Top News
Investment News Editor

ZSSF money not for projects, says Ali Karume

Unguja. Veteran politician and diplomat Ali Karume has called on authorities of the Zanzibar Revolutionary Government (SMZ) to refrain from using the Zanzibar Social Security Fund money for establishing commercial projects.Continue Reading

Popular
Chief Editor

Zanzibar airport operators decry job losses over Dubai deal

Tanzania air operators say over 600 workers are set to lose their jobs after the semi-autonomous government of Zanzibar awarded a Dubai-based company exclusive rights to handle ground services at a refurbished airport.

The Tanzania Air Operators Association (Taoa) said in a statement that the contract awarded to Dnata, which is registered at the London Stock Exchange, was in breach of the law banning any company from having exclusive rights to ground-handling services at major airports.Continue Reading