Sheria mpya ya madini itakavyodhibiti utoroshaji madini, vito

Sheria mpya ya madini itakavyodhibiti utoroshaji madini, vito

Dar es Salaam. Baada ya mabadiliko ya sheria ya madini yaliyofanyika mwaka 2017, Serikali ya Tanzania imedhamiria kufanya mabadiliko mengine ili kuimarisha udhibiti wa matendo maovu katika sekta hiyo, ukiwemo utoroshaji madini.

Dhamira ya mabadiliko hayo ni kuhakikisha vitendo vya utoroshaji madini na vito vilivyokithiri katika migodi mbalimbali nchini vinadhibitiwa.

Akizungumzia hayo hivi karibuni, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo amesema pamoja na mambo mengine, sheria hiyo inatarajiwa kumpa waziri mamlaka ya kuamua gharama za kodi na kwa kuanzia itakuwa asilimia 20 kwa kila anayezalisha madini.

“Kufanya hivi kutasaidia kutatua changamoto zilizopo kwenye masuala ya uchimbaji madini ambapo kuna kipengele kinawataka wachimbaji na wafanyabiashara kufuata taratibu za kisheria, lakini hawafanyi hivyo kwa madai ya utitiri wa kodi,” amesema.

Amesema Tanzania haipo tayari kuruhusu madini yake yatakatishwe katika mataifa mengine, akidokeza kufanya hivyo kunaiondolea nchi sifa yake.

“Kutokana na uaminifu ambao Tanzania imejiwekea, ni ngumu kutumia njia zisizofaa. Hivyo kutumia njia wanazotumia wengine ni kujiondolea sifa ya uaminifu ambayo tumejiwekea kimataifa,” amesema.

Mratibu Mkuu wa Miradi SwissAid, Alice Swai, amesema usafirishaji wa dhahabu usio na mfumo rasmi ndiyo chanzo cha kukosekana kwa taarifa za wachimbaji wadogo.

Kwa mujibu wa Swai, taarifa hizo hazijahusishwa katika ulinganisho wa taarifa za Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI), hivyo kuondolewa kwenye taarifa za kila mwaka za fedha.

“Kukosekana kwa taarifa za wachimbaji wadogo kumepelekea kuwepo na mianya ya kuruhusu usafirishaji wa dhahabu kwa mfumo usio rasmi,” amesema Alice.

Amesema kuna haja ya makubaliano ya nchi zinazopokea na kufanya biashara za madini kama uchakataji ili kuwa na mfumo wa pamoja kwa ajili ya kufuatilia taarifa za ugani katika mnyonyoro wa biashara ya kuuza na kununua madini.

“Kuna haja ya kupunguza mlolongo na kurahisisha mfumo wa kusafirisha madini nje ya nchi na kupunguza matamko, ili kukabiliana na usafirishwaji wa vipande vidogo vidogo kwa mtu binafsi kwa njia ya mabegi na ndege,” amesema.

Kwa mujibu wa Swai, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) inapaswa itoe bei ya ushindani ili kuhamasisha wafanyabiashara licha ya kuwepo kwa muswada wa sheria ya fedha ya mwaka 2024, unaopunguza mrahaba kutoka asilimia sita hadi asilimia mbili na msamaha wa kibali cha kodi kwa asilimia moja.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading