Sh350 milioni zakusanywa CRDB Bank Marathon, Dk Biteko atoa ujumbe

Sh350 milioni zakusanywa CRDB Bank Marathon, Dk Biteko atoa ujumbe

Dar es Salaam. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko ameipongeza taasisi ya CRDB Bank Foundation kwa kuendelea kuandaa mbio za CRDB Bank Marathon ambazo zimejielekeza kusaidia jitihada za Serikali kuboresha sekta ya afya, kusaidia wenye uhitaji pamoja na kukuza ustawi wa jamii.

Dk Biteko ametoa pongezi hizo wakati wa kilele cha msimu wa tano wa CRDB Bank Marathon ambazo zimekusanya Sh350 milioni kwa ajili ya kusaidia watoto wenye uhitaji wa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Jakaya Kikwete (JKCI), huduma za afya kwa wakinamama wenye ujauzito hatarishi Hospitali ya CCBRT na uwezeshaji wa vijana.

“Niwapongeze kwa kuendelea kusaidia matibabu ya kinamama na watoto wetu. Kinamama ndio wamebeba uchumi wa Taifa letu, pia ndio waangalizi wa familia zetu hususan watoto,” amesema.

Amesema ukiimarisha afya ya mama na mtoto umeimarisha afya ya Taifa.

Akizungumzia mbio hizo, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro amesema imesaidia kuchochea ari ya michezo nchini.

Amesema zimekuwa jukwaa muhimu kwa wanariadha nchini kuonyesha vipaji vyao katika jukwaa la kimataifa, kwani mbio hizo zimesajiliwa kimataifa na Shirikisho la Upimaji Mbio Kimataifa (AIMS) na Shirikisho la Riadha Duniani (World Athletic).

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema katika fedha kilichokusanywa, Sh100 milioni zitasaidia watoto wenye uhitaji wa upasuaji wa moyo JKCI.

Amesema kitita kingine kama hicho kitasaidia huduma za afya kwa kinamama wenye ujauzito hatarishi waliopo Hospitali ya CCBRT na Sh150 milioni zitasaidia uwezeshwaji kwa vijana.

Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bank Foundation, Martin Warioba amesema mbio hizo zimeshirikisha wanamichezo zaidi ya 8,000.

Amesema washindi wamezawadiwa Sh98.7 milioni katika mbio za kilomita 42, 21, 10 na kilomita 5, pamoja na wa mbio za baiskeli za kilomita 65.

Amesema lengo lao mwakani ni kupata washiriki 10,000 wa Tanzania, huku malengo ya washiriki wa Burundi na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo (DRC) yakiwa ni 3,000 kila nchi.

Katika mbio hizo, Joyloyce Kemuma alishinda kwa wanawake wakati kwa wanaume, Moses Nengichi alishinda wote kutoka Kenya.

Katika mbio ya Kilomita 21 upande wa wanawake ni Sara Ramadhan na Joseph Panga wote Watanzania.

Kwenye kilomita 10, Hamida Nasoro wa aliibuka mshindi na kwa upande wa wanaume, Mao Hindo Ako alishinda ambapo wote ni Watanzania.

Kwenye mbio za baiskeli, Paul Lumoria alishinda na kufuatiwa na Richard Laizer na Joseph Thuku ambapo kwa upande wa wanawake mshindi alikuwa Jamila Abdallah na kufuatiwa na Monica Jelimo na Julia Miringu.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading