Serikali yaweka mikakati kuendeleza wabunifu

Serikali yaweka mikakati kuendeleza wabunifu

Dar es Salaam. Serikali na wadau wa teknolojia wamedhamiria kuziinua kampuni changa bunifu (startups), ili kufikia malengo ya kuwawezesha vijana kujiajiri na kutatua changamoto zinazoikabili jamii.

Hayo yamesemwa jijini Dar es     Salaam kwenye hafla ya utoaji zawadi kwa washindi watatu wa mashindano ya ubunifu kwenye teknolojia (U.S Tanzania Tech Challenge 2024) iliyoandaliwa na ubalozi wa Marekani na kuwakutanisha vijana 100 kwenye mashindano hayo yaliyoanza Juni mwaka huu.

Akizungumza Meneja wa Ubunifu na Teknolojia kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk Gerald Kafuku amesema Serikali ina programu za kuwafikisha hatua kubwa wabunifu hapa nchini ambayo inaendelea kuzitekeleza.

“Kama nchi tunaweka mazingira ambayo matumizi ya Tehama yaweze kwenda katika kila sekta ikiwemo uchumi na matumizi ya akili mnemba yasiwe ya kuogopa tena,” amesema.

Katika kusaidia ukuaji wa kampuni changa za kiteknolojia, Dk Kafuku amesema Tanzania ina wabunifu karibu 200 na wenye kampuni za kiteknolojia wako 33 zinazosaidiwa na Serikali.

“Serikali tuna wabunifu karibu 200 na walio na kampuni wako 33 na wengine wanazo kampuni hadi Dubai na Jamhuri ya Kidemokrasua ya Congo.  Tunazidi kusaidia kampuni changa nyingi hadi zinakua kubwa,” amesema.

Amesema katika kuwawezesha vijana, wapo 20 waliopitishwa jana na sasa wamefikia uwezo wa kuanza kuzalisha fedha.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Jamii Forums, Maxence Melo amesema kupitia Jamii Check wanasaidia jamii kwa kuwawezesha wananchi kupata taarifa sahihi ili waweze kufanya maamuzi.

“Jamii Forums kama taasisi inayosaidia jamii iliamua kuja na Jamii Check ili wananachi wafanye maamuzi sahihi kupitia taarifa sahihi baada ya kufanya tafiti,” amesema.

Amesema waliamua kuanzisha Jamii Check ili kutatua changamoto za wananchi na si kwa ajili ya kupata pesa, hivyo ameshauri wanaoanzisha bunifu wawe na lengo la kusaidia jamii kwanza kabla ya kuwaza kupata fedha.

Loth Makuza kutoka kampuni ya Smart Foundry miongoni mwa washindi hao watatu amesema wanawasaidia watu na kampuni mbalimbali kusoma magazeti kupitia progamu yao maalumu waliyoianzisha kwa ajili ya kurahisisha wasomaji hao.

“Tumerahisisha watu na kampuni kusoma magazeti kupitia application yetu na wameacha kusoma magazeti ya karatasi kisha kuyatupa,” amesema.

Balozi wa Marekani hapa Tanzania Dk Michael Battle amesema ni wakati wa vijana wa Tanzania kutumia fursa ya teknolojia kujiajiri huku akisema ni wakati wao kufanya vizuri.

“Kwa wale ambao wanataka kuwa wabunifu na kubadilisha uchumi, basi pata mshirika mwenye mawazo kama yako, mtu ambaye anataka kuleta mabadiliko na kuisadia jamii.

Awali Waziri wa Habari, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Jerry Silla amesema ubunifu wa kidijitali ndio njia pekee itakaowezesha vijana kujiajiri na kutatua changamoto zinazoikabili jamii.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading