Serikali yajitenga na ripoti ya awali ya ajali ya ndege Bukoba
Serikali ya Tanzania imekanusha kutoa ripoti ya awali juu ya ajali ya ndege ya Precision Air iliyoanguka katika Ziwa Victoria Novemba sita na kuua watu 19, akiwemo rubani na msaidizi wake.
Ripoti inayokanushwa imesambaa mitandaoni toka Jumanne na kuripotiwa na vyombo mbali mbali vya ndani na nje ya Tanzania, na BBC News.
Serikali ya Tanzania sasa kupitia msemaji wake Gerson Msigwa inasema ripoti rasmi itatolewa itakapokuwa tayari na umma utataarifiwa.
Hata hivyo majibu hayo ya Msigwa yameibua mjadala na kupingwa na baadhi ya watu akiwemo Zitto Kabwe kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT Wazalendo.
Zitto aliandika kupitia mtandao wa twitter, akisema yuko tayari kupelekwa Mahakamani kama taarifa ya ripoti hiyo ya awali ni ya uongo.
Social embed from twitter
Ndege hiyo ya ATR 42-500 yenye namba PW 494 iliyokuwa na watu 43 ilianguka kwenye ziwa Victoria mita chache kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba, ikijiandaa kutua ikitokea jijini Dar es Salaam kupitia Mwanza. Watu 24 walinusurika katika ajali hiyo.
Tangu kutokea kwa ajali hiyo, mjadala umekuwa nani aliyeokoa watu hao 24, baada ya taarifa kinzani zikimtaja Majaliwa Jackson mkazi wa Nyamkazi, Bukoba kama shujaa na nyingine zikitaja muhudumu wa ndege na abiria ndio waliofungua mlango wa ndege kuokoa watu.
Serikali pia imekuwa ikinyooshewa kidole kwa kinachotajwa uzembe uliosababisha vifo vya waliokuwemo, huku ripoti kamili ikisubiriwa kwa hamu.
James Mbatia, alipozungumza na BBC baada ya ajali hiyo, alishangazwa kutumika kwa teknolojia dunia ya uokoaji, licha ya kukua kwa teknolojia ulinganisha na miaka 26 iliyopita ilipotokea ajali kubwa ya meli ya MV Bukoba, akigusia teknolojia ya kutumia kamba kuivuta ndege kutoka kwenye ziwa.
‘Yaani unavuta ndege kana kwamba ndoano unavua samaki kwenye bahari, ni jambo la fedheha sana’ alisema Mbatia na kuongeza ‘wale wavuvi wao ndio wanafanya kazi hiyo (uokoaji) wakati vikosi vipo , hakujawa na utashi wa kisiasa wa kufanya kazi hiyo’.
Waziri Bashungwa, akizungumza kwenye uwanja wa Kaitaba wakati wa kuaga miili ya watu 19 waliofariki kwenye ajali hiyo alihaidi kwamba serikali imesikia na itafanyia kazi maoni ya wananchi ya kuboresha vifaa vya uokoaji.
‘Katika janga hili lenye majonzi makubwa pia tumepokea maoni ya wananchi ya namna tunavyohitaji kujipanga vyema zaidi katika kuboresha mifumo ya uokoaji na kwa serikali hii sikivu inayoongozwa na rais wetu mpendwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na tunakwenda kuyafanyia kazi’, alisema Bashungwa.
Habari Asili za BBC za Ripoti ya Awali (20 November 2022)
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
Muslims in Pemba conduct special prayer against ZAA decision
ZANZIBAR: More than 200 Muslims in Vitongoji Village, South Pemba Region over the weekend conducted a special prayer to condemn the Zanzibar Airports Authority (ZAA) move to appoint DNATA as the sole ground handler in Terminal III of the International Airport of Zanzibar. Abeid Amani Karume.Continue Reading
New lawsuit as Zanzibar airport controversy continues
Another company joins the list as they file a petition challenging the exclusive rights granted to Dnata by Zanzibar Airports Authority.Continue Reading
Mwinyi lashes out at Zanzibar Airport, Port inefficiency claims
Zanzibar President Hussein Mwinyi has lashed out at the Opposition ACT Wazalendo, saying that the claims it raised about inefficiency in three areas within his Government were only meant to mislead the publicContinue Reading