Serikali yajitenga na ripoti ya awali ya ajali ya ndege Bukoba

Serikali yajitenga na ripoti ya awali ya ajali ya ndege Bukoba

Serikali yajitenga na ripoti ya awali ya ajali ya ndege Bukoba

Serikali ya Tanzania imekanusha kutoa ripoti ya awali juu ya ajali ya ndege ya Precision Air iliyoanguka katika Ziwa Victoria Novemba sita na kuua watu 19, akiwemo rubani na msaidizi wake.

Ripoti inayokanushwa imesambaa mitandaoni toka Jumanne na kuripotiwa na vyombo mbali mbali vya ndani na nje ya Tanzania, na BBC News.

Serikali ya Tanzania sasa kupitia msemaji wake Gerson Msigwa inasema ripoti rasmi itatolewa itakapokuwa tayari na umma utataarifiwa.

Hata hivyo majibu hayo ya Msigwa yameibua mjadala na kupingwa na baadhi ya watu akiwemo Zitto Kabwe kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT Wazalendo.

Zitto aliandika kupitia mtandao wa twitter, akisema yuko tayari kupelekwa Mahakamani kama taarifa ya ripoti hiyo ya awali ni ya uongo.

Social embed from twitter

Ndege hiyo ya ATR 42-500 yenye namba PW 494 iliyokuwa na watu 43 ilianguka kwenye ziwa Victoria mita chache kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba, ikijiandaa kutua ikitokea jijini Dar es Salaam kupitia Mwanza. Watu 24 walinusurika katika ajali hiyo.

Tangu kutokea kwa ajali hiyo, mjadala umekuwa nani aliyeokoa watu hao 24, baada ya taarifa kinzani zikimtaja Majaliwa Jackson mkazi wa Nyamkazi, Bukoba kama shujaa na nyingine zikitaja muhudumu wa ndege na abiria ndio waliofungua mlango wa ndege kuokoa watu.

Serikali pia imekuwa ikinyooshewa kidole kwa kinachotajwa uzembe uliosababisha vifo vya waliokuwemo, huku ripoti kamili ikisubiriwa kwa hamu.

James Mbatia, alipozungumza na BBC baada ya ajali hiyo, alishangazwa kutumika kwa teknolojia dunia ya uokoaji, licha ya kukua kwa teknolojia ulinganisha na miaka 26 iliyopita ilipotokea ajali kubwa ya meli ya MV Bukoba, akigusia teknolojia ya kutumia kamba kuivuta ndege kutoka kwenye ziwa.

‘Yaani unavuta ndege kana kwamba ndoano unavua samaki kwenye bahari, ni jambo la fedheha sana’ alisema Mbatia na kuongeza ‘wale wavuvi wao ndio wanafanya kazi hiyo (uokoaji) wakati vikosi vipo , hakujawa na utashi wa kisiasa wa kufanya kazi hiyo’.

Waziri Bashungwa, akizungumza kwenye uwanja wa Kaitaba wakati wa kuaga miili ya watu 19 waliofariki kwenye ajali hiyo alihaidi kwamba serikali imesikia na itafanyia kazi maoni ya wananchi ya kuboresha vifaa vya uokoaji.

‘Katika janga hili lenye majonzi makubwa pia tumepokea maoni ya wananchi ya namna tunavyohitaji kujipanga vyema zaidi katika kuboresha mifumo ya uokoaji na kwa serikali hii sikivu inayoongozwa na rais wetu mpendwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na tunakwenda kuyafanyia kazi’, alisema Bashungwa.

Habari Asili za BBC za Ripoti ya Awali (20 November 2022)

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year’s Most Read News Stories

ZAA to audit ground handlers
Popular
Investment News Editor

Zanzibar Airport Authority to audit ground handlers

Unguja. The Zanzibar Airports Authority (ZAA) is set to conduct an audit on ground handling companies that currently operate at the Abeid Amani Karume Airport with effect from Monday. The week-long audit is set to include Transworld, ZAT and the newcomer Dnata Zanzibar who were licensed in June plus exclusive rights to manage Terminal 3 building by ZAA.Continue Reading