Serikali yaipa  MSD mtaji wa Sh100 bilioni

Serikali yaipa  MSD mtaji wa Sh100 bilioni

Dodoma. Bunge la Tanzania limepitisha Bajeti ya Wizara ya Afya ya Sh1.31 trilioni huku Bohari ya Dawa (MSD), wakipewa Sh100 bilioni ili kuwaongezea mtaji.

Kwa muda mrefu kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya Ukimwi, imekuwa ikilalamika kuhusu ukosefu wa mtaji kwa MSD na kuitaka Serikali iwape mtaji wa Sh561.5 bilioni ili kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya.

Leo jioni ya Jumatatu, Mei 13, 2024 akijibu hoja za wabunge waliochangia kwenye bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2024/25, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema fedha hizo zilitolewa wiki iliyopita.

“Kwa mara ya kwanza Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imetoa Sh100 bilioni kwa ajili ya mtaji wa MSD. Nimepata fedha hizi kutoka kwa Waziri wa Fedha wiki iliyopita,” amesema.

Amesema haijawahi kutokea katika miaka minne tangu alipoanza kuongoza wizara hiyo, Serikali kutoa fedha nyingi kama mtaji kwa MSD.

Amesema Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba amemweleza anaangalia kabla ya Juni 30, 2024, anaweza kutoa fedha nyingine.

Kuhusu ubora wa huduma, Ummy amesema Serikali imejenga vituo vya afya na kuwa Watanzania hawatawapima kwa vifaa tiba na majengo walioyajenga bali wanataka huduma bora za afya.

“Hiki ni kipengele cha pili katika vipaumbele vyetu (katika bajeti) tutazingatia weledi na maadili ya watumishi wa afya, nidhamu, upatikanaji wa dawa pamoja na huduma zote na hii inawezekana,”amesema.

Amesema hilo linawezekana kwa kuwa   Profesa Mohammed Janabi ameweza kulifanya hilo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Amesema pamoja na kuongeza upatikanaji wa dawa wanaenda kuangalia usimamizi wa utoaji huduma za afya kuanzia ngazi za chini.

Amesema wanafanya mapitio ya muundo wa kamati za uendeshaji afya za mikoa, halmashauri, kuangalia muundo, majukumu na ujuzi wao ili waweze kuwasimamia kikamilifu na kuweza kuwapima.

Kuhusu posho ya kuitwa kazini, Waziri Ummy amesema ni kweli mwaka jana Serikali ilibadilisha posho nyingine, isipokuwa hiyo.

“Tumeshamuandikia Waziri wa Utumishi analifanyia kazi, madaktari tunaamini posho ya kuitwa kazini, ya kuchunguza maiti itaongezwa pamoja na sare kwa ajili ya wauguzi,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading