Serikali yafuatilia meli yenye bendera ya Tanzania iliyozama Taiwan

Serikali yafuatilia meli yenye bendera ya Tanzania iliyozama Taiwan

Dar es Salaam. Meli ya mizigo iliyodaiwa kupeperusha bendera ya Tanzania imezama karibu na bandari ya Kusini ya Kaohsiung nchini Taiwan baada ya kupigwa na kimbunga Gaemi.

Akizungumza na Mwananchi leo Julai 26, 2024, Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga amesema wanafuatilia tukio hilo kupitia ubalozi wa Tanzania nchini China.

Kwa mujibu wa mtandao wa Vessel Finder, meli hiyo ya mizigo ya kawaida iliyojengwa mwaka 1999, inamilikiwa na kampuni ya XIN LI, ikiwa na namba IMO 8685260, MMSI 677016900 na kwa sasa inatumia bendera ya Tanzania.

Taarifa zilizochapishwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), meli hiyo ilikuwa na wafanyakazi tisa ambao bado wanatafutwa.

Meli nyingine

BBC imesema: “Kimbunga hicho pia kimeleta mvua kubwa isiyokoma nchini Ufilipino, ambako meli ya mafuta yenye takriban lita milioni 1.5 za mafuta ya viwandani imepinduka. Wafanyakazi 16 wa meli ya MT Terra Nova iliyobeba bendera ya Ufilipino wameokolewa, huku mmoja akiwa bado hajapatikana,” imesema taarifa ya BBC ikimnukuu Katibu wa Usafiri, Jaime Bautista.

“MT Terra Nova ilipinduka na hatimaye kuzama,” walinzi wa pwani wa Ufilipino walisema katika ripoti, wakiongeza kuwa walikuwa wakichunguza kama hali mbaya ya hewa ilikuwa sababu.

Kimbunga Gaemi, kilichoingia pwani ya Mashariki ya Taiwan Jumatano, kimeua watu watatu na kujeruhi mamia zaidi kwenye kisiwa hicho, maafisa nchini humo walisema.

Kabla ya kufika Taiwan, Gaemi ilizidisha hali ya mvua huko Ufilipino, ambako watu wanane walifariki dunia.

Mamlaka ya Walinzi wa Pwani ya Taiwan imesema Fu Shun, meli ya mizigo iliyopinduka kwenye pwani yake, ilikuwa na raia tisa wa Myanmar ndani. Iliongeza kuwa meli nyingine tatu za kigeni zimekwama wakati wa kimbunga hicho, japo ziko salama.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, nchini Ufilipino, meli ya mafuta imepinduka katika Bahari ya Manila, ikiwa inaelekea katika jiji la kati la Iloilo na kuzama. Ilimwaga mafuta yaliyoenea kwa kilomita kadhaa, mamlaka zimesema. Maofisa waliongeza kuwa upepo mkali na mawimbi makubwa yanakwamisha mwitikio katika uokoaji.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading