Serikali: Sampuli zilizochukuliwa hazijathibisha virusi vya Marburg

Serikali: Sampuli zilizochukuliwa hazijathibisha virusi vya Marburg

Serikali: Sampuli zilizochukuliwa hazijathibisha virusi vya Marburg

Dar es Salaam. Wakati Shirika la Afya Duniani (WHO) likisema watu wanane wamefariki dunia kutokana na ugonjwa unaoshukiwa kuwa wa virusi vya Marburg (MVD) mkoani Kagera, Wizara ya Afya ya Tanzania imesema sampuli zilizochukuliwa hazijathibitisha uwepo wa virusi hivyo.

Taarifa hiyo ya Wizara ya Afya imetolewa leo Januari 15, 2025 na waziri wake, Jenista Mhagama saa chache tangu WHO watoe taarifa ya kushukiwa kwa virusi hivyo.

“Wizara ya Afya imepokea tetesi za uwepo wa ugonjwa wa Marburg katika Mkoa wa Kagera.

“Kufuatia tetesi hizo, Wizara imechukua hatua kadhaa za haraka ikiwemo: kutuma timu ya wataalamu; kufanya uchunguzi wa suala hili; kuchukua sampuli na kufanya vipimo vya maabara. Mpaka leo, Januari 15, 2025, majibu ya uchunguzi wa kimaabara kutoka kwa wahisiwa wote waliochukuliwa sampuli hizo hayajathibisha uwepo wa virusi vya Marburg,”imeeleza taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo imeongeza kuwa Serikali imeimarisha mifumo ya ufuatiliaji kuhusu uwepo wa mlipuko huo.

“Wizara inapenda kuwahakikishia wananchi pamoja na jumuiya ya kimataifa, likiwemo WHO kuwa imeimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa na itaendelea kutoa taarifa zaidi,”imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Waziri Jenista.

Iwapo itathibitika kwamba kuna mlipuko wa ugonjwa huo nchini, itakuwa mara pili, ya kwanza ilikuwa Machi 16, 2023 Serikali kupitia Wizara ya Afya ilipotangaza uwepo wa ugonjwa usiojulikana katika Kata ya Maruku na Kanyangereko, vijiji vya Bulinda na Butayaibega mkoani Kagera ambapo watu tisa walibainika kuathirika na Marburg.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

European Union Bans Air Tanzania Over Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

European Union Bans Air Tanzania Over Safety Concerns

European Union Bans Air Tanzania Over Safety Concerns

Kampala — The European Commission added Air Tanzania to the EU Air Safety List, banning the airline from operating within European Union airspace. This decision follows the denial of Air Tanzania’s Third Country Operator (TCO) authorization by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), citing significant safety deficiencies.

The EU Air Safety List includes airlines that fail to meet international safety standards. Commissioner Tzitzikostas emphasized the importance of passenger safety, stating: “The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards. We strongly urge Air Tanzania to take swift action to address these safety issues. The Commission has offered its assistance to Tanzanian authorities to enhance safety performance and achieve compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania joins several African airlines banned from EU airspace, including carriers from Angola, the Democratic Republic of Congo, Sudan, and Kenya. Notable names include Congo Airways, Sudan Airways, and Kenyan carriers Silverstone Air Services and Skyward Express. The ban reflects the EU’s strict approach to aviation safety worldwide.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading