Serikali: Sampuli zilizochukuliwa hazijathibisha virusi vya Marburg

Serikali: Sampuli zilizochukuliwa hazijathibisha virusi vya Marburg

Serikali: Sampuli zilizochukuliwa hazijathibisha virusi vya Marburg

Dar es Salaam. Wakati Shirika la Afya Duniani (WHO) likisema watu wanane wamefariki dunia kutokana na ugonjwa unaoshukiwa kuwa wa virusi vya Marburg (MVD) mkoani Kagera, Wizara ya Afya ya Tanzania imesema sampuli zilizochukuliwa hazijathibitisha uwepo wa virusi hivyo.

Taarifa hiyo ya Wizara ya Afya imetolewa leo Januari 15, 2025 na waziri wake, Jenista Mhagama saa chache tangu WHO watoe taarifa ya kushukiwa kwa virusi hivyo.

“Wizara ya Afya imepokea tetesi za uwepo wa ugonjwa wa Marburg katika Mkoa wa Kagera.

“Kufuatia tetesi hizo, Wizara imechukua hatua kadhaa za haraka ikiwemo: kutuma timu ya wataalamu; kufanya uchunguzi wa suala hili; kuchukua sampuli na kufanya vipimo vya maabara. Mpaka leo, Januari 15, 2025, majibu ya uchunguzi wa kimaabara kutoka kwa wahisiwa wote waliochukuliwa sampuli hizo hayajathibisha uwepo wa virusi vya Marburg,”imeeleza taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo imeongeza kuwa Serikali imeimarisha mifumo ya ufuatiliaji kuhusu uwepo wa mlipuko huo.

“Wizara inapenda kuwahakikishia wananchi pamoja na jumuiya ya kimataifa, likiwemo WHO kuwa imeimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa na itaendelea kutoa taarifa zaidi,”imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Waziri Jenista.

Iwapo itathibitika kwamba kuna mlipuko wa ugonjwa huo nchini, itakuwa mara pili, ya kwanza ilikuwa Machi 16, 2023 Serikali kupitia Wizara ya Afya ilipotangaza uwepo wa ugonjwa usiojulikana katika Kata ya Maruku na Kanyangereko, vijiji vya Bulinda na Butayaibega mkoani Kagera ambapo watu tisa walibainika kuathirika na Marburg.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading